Basi la Hekima Laanguka na kuua Tanangozi

Basi la Hekima Laanguka na kuua Tanangozi

Pengo

JF-Expert Member
Joined
Oct 15, 2009
Posts
579
Reaction score
10
Habari nilizozipata muda huu kutoka kwa abiria aliyemo katika basi la Superfeo ni kwamba basi la kampuni ya Hekima limeanguka katika kitongoji cha Tanangozi Iringa na kuua abiria wengi idadi ambayo bado kujulikana, kwa vile kuna wengine bado wamelaliwa na bodi la basi hilo.

Kuna majeruhi wengi sana na tayari akina mama wawili wameonekana wamekatika mikono yao vibaya, hali za majeruhi ni mbaya sana.
 
Terrible. Lakini why Tz things like these are daily on the increase?
 
This is seriously shocking as it's now the order of the day.... I guess SUMATRA need to look into this more clesely or else tutakwisha.
 
TZ tumeshaamua sub-standards ni sehemu ya maisha yetu.
Ina maana hatuna sheria!!!
 
ohhh my God....not again!!!!! Watanzania tutapata vilema na kupoteza maisha kwa hizi ajali mpaka lini??? My heart is aching...i feel soo helpless. Dear Lord, please come to our rescue, You are our only solution.

Maombi yangu yako kwa majeruhi for their quick recovery na wafiwa wote Mungu awape amani. Poleni watanzania wenzangu.
 
Hizi ajali chanzo chake ni hii serikali, for sure. Imeshindwa kudhibiti. Wanatafuta visingizio kibao, mara abiria wanachochea mwendo kasi kwa madereva!!!!!!! Hii haiingii akilini hata kidogo. Haiwezekani mtu akuambie kaibe kisha ukaenda iba kweli! Police na Ma RTO na RPC wamegeuza hii ni miradi.

Kudhibiti mwendo kasi hakuhitaji Speed Gavana za Afrika kusini, is just simple, ni kuwa na sheria kali, wasimamizi wasiopokea rushwa na kila gari liwe na Speed Control Sheet ambayo itakuwa ikikaguliwa na kujazwa muda wa kufika na kuondoka kituoni. Inajulikana ni Kilometer ngapi kutoka Iringa hadi Mikumi, dereva atajaziwa muda wa kuondoka Iringa na muda wa kufika Mikumi. Akiwahi Faini. Lakini kwa style hii watanzania wataendelea kuuawa huku trafiki wakineemeka kwa rushwa na vigogo wakiendelea kujitafutia source za income kama hiyo mi speed gavana.
 
hua naenda mby kikazi mara nyingi, m,abasi yaendayo huko yanakimbia sana na wanajua sehem wanazokaa trafic na tochi zao na wakifika ktk hayo maeneo wanapunguza mwendo na kuvuka salama. wakati mwingine wanapeana ishara ya tochi za matrafic wanapopishana, kwa kweli chanzo kikuu cha ajali ni mwendo mkali, watatuua hawa madereva jamani.
 
Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu pahali pema poeponi na awaponye majeruhi wote
 
Ni mengi sana ya kusema kuhusu utaratibu wa kudhibiti ajali katika nchi yetu, lakini kwa sasa tuungane pamoja kuwaombea majeruhi wapate afya njema, na wale waliopoteza maisha(kama wapo) basi wapate pumziko la milele!
Aftermath zingine tuzijadili kwa mapana baada ya tathimini ya ajali nzima, maana so far tunaongea bila data zozote za uharibifu uliotokea!
 
Inasikitisha sana... lakini ndani ya miezi mitatu tu, tumepata taarifa za ajali hizi nyingi, what's wrong?
 
Inasikitisha sana... lakini ndani ya miezi mitatu tu, tumepata taarifa za ajali hizi nyingi, what's wrong?
Hali ni mbaya kiasi hiki halafu utasikia wamiliki wa mabasi wanagoma kufunga speed governor!
 
Inasikitisha sana... lakini ndani ya miezi mitatu tu, tumepata taarifa za ajali hizi nyingi, what's wrong?

Tatizo watu wengi wanaweza kutembeza magari, wanaojua kuendesha ni wachache mno. Kitengo cha usalama barabarani kiko busy na misafara ya viongozi badala ya kushughulikia masuala ya raia. Mkuu wa traffic yupo walipo viongozi kila mahali nani atashughulikia masuala mengine?
 
Hali ni mbaya kiasi hiki halafu utasikia wamiliki wa mabasi wanagoma kufunga speed governor!

Hizo speed governor ni upumbavu mwingine tunaoletewa kwa ajili ya kutunisha mifuko ya wahuni wachache. kuwepo ni mikakti rahisi kutekelezeka na yenye gharama nafuu na urahisi wa kuisimamia. Rwanda wamewezaje?

Poleni Majeruhi wa Ajali hii.
 
Haya mambo yananitoa machozi sasa, jamani kuna mahali watendaji wame "expire" hawana jipya na wamefikia kikomo cha kubuni mbinu tofauti za kuzuia ajali hizi zinazotuua kila siku!
Mie bado nalia na kina Said Mwema.
 
Hali ni mbaya kiasi hiki halafu utasikia wamiliki wa mabasi wanagoma kufunga speed governor!

Hii ya speed governor ina mizengwe yake. Walifunga miaka ya 90 lakini mwendo ukawa uleule. Hatujaambiwa nini kilitokea na udhibiti gani ulifanyika. Kama ujuavyo, speed governor hulegezwa, hung'olewa au hata kutowekwa kabisa, in the first place. Na mshiko unapopenyezwa hakuna wa kuuliza.

Hata hivyo, mwendo sio sababu pekee ya ajali. Wasiwasi wangu mkubwa pia ni katika nidhamu ya matengenezo (service and repair) ya mabasi na vipuri vinavyotumika; manake tunaingiza bidhaa nyingi zisizo na viwango huku, kwa wateja, kinachoangaliwa ni bei tu. Ukijumlisha na utamaduni wa rushwa na ulaji tuliojijengea kwa miongo kadhaa hatuna tiba muafaka kwenye hili na mengine mengi. Amini nawaambia, bila uongozi (usimamizi) thabiti, hakuna teknolojia itakayotusaidia. Janja ya nyani imetuzidi kete katika nchi hii.
 
Mbona inasemekana hakuna aliyekufa mpaka sasa, rafiki yangu kapita eneo hilo mda mfupi, anasema imetokea tanangozi mita chache baada ya ile minara mingi ya simu, likiwa linatoka tunduma kwenda dar. Mungu awape faraja yake waliokutwa na tatizo hilo.
 
Mungu atusaidie na kutuepusha na mabalaa haya ya ajali!
Basi hilo lilikuwa likitokea wapi kuelekea wapi?
 
Mungu atusaidie na kutuepusha na mabalaa haya ya ajali!
Basi hilo lilikuwa likitokea wapi kuelekea wapi?
 
Back
Top Bottom