Utetezi wako ni wa hovyo!
Hii ni biashara. Na hakuna aliyemlazimisha kuifanya. Kama ikimshinda anaacha watakuja wengine. Na kuna biashara ambayo siyo mchezo? Kwa hiyo watu wavumilie huduma mbovu na udanganyifu kisa biashara fulani "siyo mchezo?". Come on man!
Na katika biashara jaribu kila uwezalo kumridhisha mteja wako. Hata ukikosea au ukapatwa na dharula basi toa maelezo ya kueleweka na ikibidi muombe mteja wako msamaha. Jamaa wana kiburi utafikiri mmepanda bure. Siyo mtu anakuuliza kabisa wakati anakata tiketi kuwa hili basi ni jipya namba E unamjibu ndiyo na tiketi yake inaonyesha hivyo halafu unamletea basi limechoka kweli kweli. Huo sio udanganyifu katika biashara? Kwa nini tu usiseme ukweli?
Haya hilo basi C likashindwa kupanda Mlima Sekenke kidogo lirudi kinyume nyume likazimika hapo mbele tu. Abiria wakakaa hapo zaidi ya masaa matatu. Hakuna cha maelezo wala nini. Kumbe tatizo dogo tu filter mbovu. Akaja mwenzao akawapa filter mpya. Piga moto huku karibia na Dodoma basi likazima tena...
Aaaaaargh! [emoji706][emoji706][emoji706]