Basi la Happy Nation lapata ajali Mikese

Basi la Happy Nation lapata ajali Mikese

Happy Nation ni mabasi ya hovyo yanayoendeshwa hovyo hovyo tu. Ajali kwa hawa jamaa ni suala la muda tu!

Halafu wadanganyifu. Unamkatia mtu tiketi inasema basi E (jipya) linalokuja ni mkangafu namba C mpaka seat zimechakaa. Na lazima liharibike njiani.

Nadhani kampuni imekua kwa kasi na sasa wameanza kujaa kiburi na kutojali. Wataanguka wasipojiangalia! 🚮🚮🖐
Biashara ya mabasi ina changaamoto laiti kama na wewe ungekua unamiliki mabasi ungeona changamoto ya biashara hii na ungekua muelewa pindi zinapotokea dharura kama hizo,.
Ni bora uende na namba C nzima kuliko namba E ambayo imepata dharura na ina hitilafu.

Biashara ya magari siyo mchezo we endeleo tu kuona gari zinapita njiani na unatukana kuwa ni magari mabovu ila nyuma yake ujue kuna mwanaume anavuja jasho siyo mchezo
 
Kweli mkuu. Mtu ana safari usiki ya zaidi ya km 500, mchana kutwa anashinda anazurura, saa 2 usiku anakunywa kahawa/energy drink anaanza safari.
Mimi sioni sababu ya haya magari kusafiri usiku. Kwa mfano mtu unaenda Moshi , masaa 8 hadi tisa umeshafika, dereva analala vizuri tu saa 12 yuko barabarani. Kiherehere tu
 
Duuh....
1...Alpha-nzega
2...Baraka-uko kusini
3...Ally's-manyoni

Na hizi zote zmeondoka na watu zaidi ya 10

4..Leo tena Happy nation

Innalillah wainnailayh rajiuun
Ilipangwa wafe hawa raia ..... Hakuna kusingizia bus wala madereva ni mipango ya Malaika mtoa roho amewakutia kwenye bus, nyakat mwingine tuzielewe alama za nyakat
 
Safari za usiku kwa Tanzania bado ni hatari sana ,,,,, hatukujipanga …zitamaliza watu
 
Biashara ya mabasi ina changaamoto laiti kama na wewe ungekua unamiliki mabasi ungeona changamoto ya biashara hii na ungekua muelewa pindi zinapotokea dharura kama hizo,.
Ni bora uende na namba C nzima kuliko namba E ambayo imepata dharura na ina hitilafu.

Biashara ya magari siyo mchezo we endeleo tu kuona gari zinapita njiani na unatukana kuwa ni magari mabovu ila nyuma yake ujue kuna mwanaume anavuja jasho siyo mchezo
Utetezi wako ni wa hovyo!

Hii ni biashara. Na hakuna aliyemlazimisha kuifanya. Kama ikimshinda anaacha watakuja wengine. Na kuna biashara ambayo siyo mchezo? Kwa hiyo watu wavumilie huduma mbovu na udanganyifu kisa biashara fulani "siyo mchezo?". Come on man!

Na katika biashara jaribu kila uwezalo kumridhisha mteja wako. Hata ukikosea au ukapatwa na dharula basi toa maelezo ya kueleweka na ikibidi muombe mteja wako msamaha. Jamaa wana kiburi utafikiri mmepanda bure. Siyo mtu anakuuliza kabisa wakati anakata tiketi kuwa hili basi ni jipya namba E unamjibu ndiyo na tiketi yake inaonyesha hivyo halafu unamletea basi limechoka kweli kweli. Huo sio udanganyifu katika biashara? Kwa nini tu usiseme ukweli?

Haya hilo basi C likashindwa kupanda Mlima Sekenke kidogo lirudi kinyume nyume likazimika hapo mbele tu. Abiria wakakaa hapo zaidi ya masaa matatu. Hakuna cha maelezo wala nini. Kumbe tatizo dogo tu filter mbovu. Akaja mwenzao akawapa filter mpya. Piga moto huku karibia na Dodoma basi likazima tena...

Aaaaaargh! 🚮🚮🚮
 
Happy nation route ya mpanda huwa wanajitahidi kuendesha vizuri.
 
Utetezi wako ni wa hovyo!

Hii ni biashara. Na hakuna aliyemlazimisha kuifanya. Kama ikimshinda anaacha watakuja wengine. Na kuna biashara ambayo siyo mchezo? Kwa hiyo watu wavumilie huduma mbovu na udanganyifu kisa biashara fulani "siyo mchezo?". Come on man!

Na katika biashara jaribu kila uwezalo kumridhisha mteja wako. Hata ukikosea au ukapatwa na dharula basi toa maelezo ya kueleweka na ikibidi muombe mteja wako msamaha. Jamaa wana kiburi utafikiri mmepanda bure. Siyo mtu anakuuliza kabisa wakati anakata tiketi kuwa hili basi ni jipya namba E unamjibu ndiyo na tiketi yake inaonyesha hivyo halafu unamletea basi limechoka kweli kweli. Huo sio udanganyifu katika biashara? Kwa nini tu usiseme ukweli?

Haya hilo basi C likashindwa kupanda Mlima Sekenke kidogo lirudi kinyume nyume likazimika hapo mbele tu. Abiria wakakaa hapo zaidi ya masaa matatu. Hakuna cha maelezo wala nini. Kumbe tatizo dogo tu filter mbovu. Akaja mwenzao akawapa filter mpya. Piga moto huku karibia na Dodoma basi likazima tena...

Aaaaaargh! 🚮🚮🚮
Hata ndege huwa zina hairisha safari, unaweza kukatiwa ticket gari namba E na asubuhi ikakataa kuwaka au ikapata hitilafu alafu gari nyingine aliyobaki nayo ni namba C lazima atakuletea hiyo hiyo upande ili ufike safari yako, sasa ulitaka afanyaje akurudishie nauli au akufaullishe kwenye gari zingine?
 
Gari inayotembea zaidi ya masaa 12, taratibu za kupewa leseni LATRA zinataka awe na dereva wawili. Madereva akili zao fyatu tu, hasahasa hawa wa ma bus.
Uko sahihi mkuu, tatizo ni madereva na wasimamizi wa makampuni yao. Mf. haya basi ya saa 1 jioni Dar to Mwanza, madereva wanaamkia gereji, wakitoka hapo wanaanza misele mtaani, jioni wanakamata ndinga kuana safari.
 
Uamuzibwa latra kuruhusu safari za usiku haukuzingatia ubora wa barabara zetu.
Kuna vipande korofi kama kutoka mlandizi hadi morogoro tutashuhudia ajali nyinginewna za usiku
 
Hata ndege huwa zina hairisha safari, unaweza kukatiwa ticket gari namba E na asubuhi ikakataa kuwaka au ikapata hitilafu alafu gari nyingine aliyobaki nayo ni namba C lazima atakuletea hiyo hiyo upande ili ufike safari yako, sasa ulitaka afanyaje akurudishie nauli au akufaullishe kwenye gari zingine?
Ingekuwa ni dharura ya mara moja sawa (japo nayo kwa mtu anayejali wateja wake, lugha nzuri na hata kuomba msamaha ingefaa).

Kwa hawa ni malalamiko ya kawaida...unakatiwa basi namba E (nauli kubwa) unaletewa mkangafu. Siyo fair; na wanajiharibia biashara tu.

Hata kama unafanya kazi huko waambie hivyo!
 
Back
Top Bottom