Basi la Extra Luxury limekamatwa na mirungi 55kg

Jun 20, 2023
54
51
Jeshi la polisi mkoani Kilimanjaro, limefanikiwa kukamata shehena ya dawa za kulenya aina ya mirungi ndani ya basi la Extra Luxuly lenye namba za usajili T643 DVL ikisafrishwa kutoka mkoani Arusha kwenda jijini Dar es salaam.

Habari kutoka ofisi ya kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro, zimedhibitisha kukamatwa kwa basi hili pichani chini eneo la majengo Mapya wilaya ya same baada ya askari wa usalama barabarani kulifanyia upekuzi basi hilo kwenye buti zake za kuhifadhi mizigo.

Kwa mujibu wa habari hizo,basi hilo lilikamatwa wakati likisafrisha wanafunzi wa shule ya Arusha sayansi kutoka Jijini Arusha kuelekea Dar es salaam wakirejea makwao baada ya muhula wa mwisho wa masomo kumalizika.

Kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa amedhibitisha kukamatwa kwa basi hilo likiwa na shehena hiyo ya mirungi ambako imekutwa misokoto 365 sawa na kilogram 55 kiwango ambacho kinatajwa kuwa ni kikubwa .

Mirungi imeingizwa kwenye sheria ya madawa ya kulevya na mtu anayepatikana na hati ya kusafrisha madawa hayo adhabu yake ni kifungo cha maisha jela huku anayekutwa akitumia adhabu yake ni kifungo cha miaka 30 jela.

Kosa la kusafrisha dawa kulevya linaangukia kwenye kifungu cha 15 kifungu kidogo cha kwanza(b) cha sheria namba 5 ya mwaka 2015 ya udhibiti wa usafrishaji wa dawa za kulevya kama ilivyofanyiwa marejeo madogo ya sheria namba 23 ya mwaka 2016.

Mwaka 2017 aliyekuwa mtumishi wa PPF mkoa wa Kilimanjaro,Anitha Oswald alikamatwa na shhena ya mirungi kilo 216 akifrisha kutoka Njia panda ya Himo akitumia gari lake aina ya Toyota CIENTA T674DLB,Anitha akihukumiwa kifungo cha maisha jela baada yakukuitwa na hatia ya kusafrisha dawa za kulevyas na gari lake likitaifishwa na serikali.

Tusubiri kuona je basi hilo litataifishwa na serikali baada ya watuhumiwa kushitakiwa na kisha kupatikana na hatia?

Mabasi ya usiku nayo yamulikwe, yanafanya hii biashara polisi mjue maana ukaguzi ni vituo vitatu tu toka Arusha, ni Same, Korogwe na Msata

EXTRA BUS.jpg

ANITHA OSWALD.jpg
 
Basi langu hilo jamani...Yatapita.

Hapo kuna mtu hajaridhika na mgao...Akawachomea...

Nakumbuka Dec. Mwaka jana maeneo hayo hayo.. kuna gari la Abiria lilikuwa linatoka Arusha.. nimelishahau jina...

Lilifika maeneo hayo likiwa mbele yetu.. lilisachiwa isivyo kawaida.. wale utingo wa basi letu wakawa wanasema kuna kitu kinatafutwa hapo... Dakika 20 Wakakutana na Begi limejaa mirungi...

Na ukitaka kujua kuna watu/ mtu amewachomea.. Hawasachi mbali na maeneo ulipo huo mzigo.
 
Basi langu hilo jamani...Yatapita.

Hapo kuna mtu hajaridhika na mgao...Akawachomea...

Nakumbuka Dec. Mwaka jana maeneo hayo hayo.. kuna gari la Abiria lilikuwa linatoka Arusha.. nimelishahau jina...

Lilifika maeneo hayo likiwa mbele yetu.. lilisachiwa isivyo kawaida.. wale utingo wa basi letu wakawa wanasema kuna kitu kinatafutwa hapo... Dakika 20 Wakakutana na Begi limejaa mirungi...

Na ukitaka kujua kuna watu/ mtu amewachomea.. Hawasachi mbali na maeneo ulipo huo mzigo.
Tulikuwa wote safarini siku hiyo...
 
Back
Top Bottom