Bashir tells Sudan Youths: I won't run for reelection in Sudan

Bashir tells Sudan Youths: I won't run for reelection in Sudan

Ofisa mwandamizi wa Chama tawala cha Sudan cha National Congress (NCP) Bw. Rabie Abdel-Atti amesema, rais Omar al-Bashir wa nchi hiyo hatagombea tena urais kwenye uchaguzi utakaofanyika mwaka 2015.

Bw. Rabie amesema hii ni sehemu moja ya mkakati kuhusu mageuzi ya demokrasia na kupokezana madaraka unaotekelezwa na chama hicho. Chama cha NCP kinatarajia vijana wataweza kuonesha umuhimu wao katika mambo ya siasa.
Wakati huo huo maofisa wengine wa chama hicho walikanusha kuwa uamuzi wa rais Bashir unatokana na mabadiliko makubwa yanayotokea katika baadhi ya nchi za kiarabu. Rais Bashir aliingia madarakani mwaka 1989, mpaka sasa amekuwa rais wa nchi hiyo kwa miaka 22, ni mmoja kati ya viongozi ambao wamekaa madarakani kwa muda mrefu zaidi.
 
spacer.gif

Cairo-Misri yaziomba nchi mbalimbali kuzuia mali za Mubarak

(GMT+08:00) 2011-02-22 18:25:00

Ofisi ya mwendesha mashtaka mkuu ya Misri imemwagiza waziri wa mambo ya nje Bw. Abul Gheit kuziomba nchi mbalimbali kuzuia mali za aliyekuwa rais wa Misri Bw. Mubarak pamoja na jamaa zake. Shirika la habari la Uingereza BBC awali lilisema huenda mali za familia ya Mubarak zikafikia paundi bilioni 43.5, ikiwemo akiba na uwekezaji nje ya Misri, pamoja na nyumba za anasa mjini London, New York, Los Angeles na sehemu ya kando ya Bahari Nyekundu
 
Nitafurahi kama huo upepo utashuka chini ya jangwa la Sahara maana wenzetu waarabu muda mfupi ujao wataanza kufaidi democrasia ya kweli.

Naamini vitu kama JF vinasaidia kutujenga kifikra kwanza ndipo baadaye tutakapotambua kuwa nasi tunaweza.
 
Back
Top Bottom