Lowassa hakuonewa hata kidogo. Alikichukiza chama chake na hata Mungu wa mbinguni. Kitendo cha kuanza kampeni mapema kuanza kuwapa watu pesa halafu kuwaambia waje kujifanya wanakuomba ugombee urais kilikuwa ni maudhi kwa CCM. Halafu Januari 2015 alitoa shilingi 500,000 kwa kila mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM na shilingi 1,000,000 kwa kila mjumbe wa NEC ya CCM. Yeye alidai ni zawadi ya mwaka mpya lakini CCM waliona ni rushwa. Mambo mengine yote ya nyuma waweza kusahau. Lakini hayo mawili yalitosha kabisa kumtosa. Kumuudhi Mungu ni kule kuwarubuni watumishi wa Mungu wachungaji na mashehe na kuwapa pesa ili nao waende kwake kumwomba agombee urais. Mungu hawezi kufurahia mtu tajiri ambaye anatumia ufukara wa watumishi wake kufanikisha malengo yake ya kisiasa. Halafu kitendo cha Lowassa ambaye ni Mkristo kuingia msikitini na kuvalishwa kama Ustaadh ili tu apate kura za Waislam ni kumdhihaki Mungu kwa sababu leo huwezi kuwa Mwislam na Mkristo wakati huo huo. Ushenzi huu Mungu asingeruhusu ufanikiwe. Lowassa kapigwa chini na Mungu mwenyewe pamoja na CCM yake kwa makosa yake mwenyewe.