Bashe anusurika kutekwa



hamna habari hapo. ni udaku tu wa bashe ili aendelee kuuza gazeti lake. njaa hizi balaa. kama walikutana uso kwa uso iweje asione namba za hilo gari?
 
kumbe nawe umeona..hawa jamaa wanatuchezea akili.ina maana hadi sasa hawana hata system ya kujihakikishia usalama wa wenyewe?mtu unafuatiliwa zaidi ya nusu saa unapitia grocery kuzuga,bado wako na wewe,kama haamini polis si angeomba watu pale grocery wamsaidie kuwakamata hao jamaa na kuwahoji?
 
Hapo nunua bastola

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 

hawa jamaa hata ukisema ung'oe kucha uwapelekee watakataa wanataka wafanye wenyewe.mzee wa madui 11 kwani unahitaji kucha za watu wangapi ili agenda yako ifanikiwe?
 
Naona akili yangu imegoma kuikubali hadithi hii, labda kama msimuliaji/mwandishi angetahadharisha kuwa "hadithi hii ni ya kubuni tu, haihusiani na mazingira wala tukio lolote la kweli".
Haiwezekani atoke tu ofisini astukie kuwa anafuatiliwa halafu aanze kuongozana nao akiwapeleka nyumbani kwake.
 
Bashe usituharibie tz yetu.
1: una marafiki kibao usalama tena wakubwa kwa nn hukuwapigia simu?
2:huna namba za marafiki zako polisi?
3:Kwa nn hukuwapigia hata jamaa zako? Mkeo .nk?
4:E N L mzee wa mvi swahiba wako ulimjulisha kabla?
5: Wafanyakazi wenzio hasa waandamizi ungewaambia wakufuate nyuma baada ya kuhisi hatari. Acha uzushi bashe una marafiik wengi .
 
Naanza kuwa na mashaka sasa, ila bashe atambue kuwa wakati mwingine itakapokuwa kweli watu bado watajua anatania. Kwanini asipige simu hata kwa watu wengine anaowaamini wajaribu kuwa nae karibu kujua hao ni nani? Hainijii akilini kusema eti hata baada ya kupark grocery bado alishindwa kusoma namba ya gari? Hata jamaa zake walioikuta gari pale pale wakati wanatoka kwake na kawasimulia yote ina maana hawakuwasha taa kuona namba ya hiyo gari? Naona sinema inachezwa hapa, some people are forcibly looking for public symphathy for their political good, let us be pretty careful please....
 
Mbona kama hii habari ya kutungwa? Janja ya kutaka kuuza magazeti yenu Uchwara,
 
Rwakatare huyu

Hawa Jamaaa wana akili za Kipoyoyo,kwa muda wiki mbili sasa wamekuwa waki iandama Chadema nadhani ni makusudi ili wajiteke waseme ni Chadema At Work.

Hivi huyu hata silaha hana? Anaogopa nini sasa? Kuanzia sinza hadi mwenge anafuatiliwa hana number ya pOlisi ya doria? Mbona pikipiki na defender za diria zinakuwa nyingi tu usiku? Si achukue number zao na siku ikitokea hivyo awapigie ili waweze kuwa ambush hao Magaidi ?
 
Rwakatare huyu

Kwa hiyo unataka kusema anatoa order toka mahabusu? Acha hizo, I guess wote bado tunasubiri ukweli.

Ila Duh inabidi awe na bodigadi sasa maana wana chama cha Malafi watamtafuta tena tu.
 
Hata mimi napatwa na mashaka na habari hii hasa ukiona alivyolishughulikia suala hili.
Siku kadhaa zilizopita tulisoma jinsi Bashe na Kibanda walivyofuatiliwa wakati wakitoka ofisini. Baada ya muda Kibanda akavamiwa na kujeruhiwa. Halafu leo Bashe anagundua kuwa anafuatiliwa na gari mbili halafu anakwenda kusimama kwenye glosary ili asome namba za hayo magari.
Ni kweli ni muhimu kujua namba lakini kwa insticts za kawaida kwa mwanadamu anayejikuta katika hali kama hii kujiokoa ndiko kunakuwa suala la kipaumbele na si kuanza kuwachunguza adui zako.
Kwa nini wakati alipofika kwake akawasimulia wageni yaliyomkuta na asitafute msaada wa vyombo vya dola? Ana namba ya Nchimbi, 0mwema na Kova lakini hakutaka kuwasiliana nao.
Nadhani unahitajika ufafanuzi ili kuifanya habari iaminike zaidi


Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Kama alifuatwa muda wote huo na yeye kama mhusika na chombo cha habari ana njia nyingi tu za mawasiliano na vyombo vya usalama, kwa nini hakufanya hivyo?
 
Bashe ni usanii huo, yuko kazini kuendesha propaganda dhidi ya Membe wakati huohuo akimfagilia EL
 
Wa Tz Tuache unafiki matukio haya yapo TZ na tukubali Kuwa serikali au inayapuzia au imeshindwa mbinu na hawa magaidi.h
UBinafsi wetu ndio utafanya vitendo hivi vya kiovu vindelee.

Leo kwa kibanda, kesho BAshe na keshokutwa yaweza Kuwa Kwako.

TUache ushabiki wa kisiasa tuweke utaifa Mbele na ubinadam.
Kwa kifupi Tz inatisha sana sasa hivi, kwani vitendo vya ute kaji nyara na kuteswa vinazidi kupamba moto Siku hadi Siku!
 
Sinema nyingine hii.Kwani Lwakatare yuko nje kwa dhamana?Bashe bashe!unataka kukimbia kivuli chako mwenyewe!Nafikiri kigwangala atakuwa amecheka sana baada ya kusoma habari hii.
Nunua dawa ya ganzi utembee nayo ndani ya gari.Jamaa huwa hawatumii ganzi
 
Last edited by a moderator:
Mambo madogo sana haya wananchi tukiamua kushughulika nao.tatizo ni hili naliongea mara kwa mara humu,wapo wananchi wa aina hii wenye uthubutu wa kula sahani moja na serikali?
 
Bashe kapika SINEMA hii ili ku-draw attention ya watu.Kwanza amejuaje kama wanakuja kumteka?Je kama lengo ni kumpiga risasi na kuishia, wangempata vizuri aliposhuka hapo glossary.Ni ishara gani zilizoonyesha kwamba wanamfuata ili wamteke?
Kama alifuatwa muda wote huo na yeye kama mhusika na chombo cha habari ana njia nyingi tu za mawasiliano na vyombo vya usalama, kwa nini hakufanya hivyo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…