Gazeti la leo la Mwanahalisi limepambwa na kichwa cha habari "Nape amgeukia Kikwete" likimnukuu Nape akisema kwamba JK ndiye chanzo cha matatizo ndani ya CCM na kumtaka naye ajivue gamba. La ajabu maneno hayo yanadaiwa Nape aliyatoa akiwa kwenye chumba cha habari cha New Habari (2006) Ltd, mahasimu wakubwa wa Mwanahalisi ambao walichafuana kwa kupakana matope kupitia magazeti yao.
Mazungumzo yaliyochapishwa inaonekana yalikuwa majibishano kati ya Nape na Bashe. Lakini baada ya majibishano hayo kwa lengo la kufanya 'Character assasination' Bashe ameamua kuongeza chumvi aliyoyasema Nape na kuwapa mahasimu wake (Mwanahalisi) ambao wamekuwa wakimwandika vibaya bosi wake (Rostam) ili amgombanishe na Mwenyekiti wake JK.
Bashe anaonyesha haja komaa kisiasa, pamoja na tofauti walizonazo (Nape na Bashe), Nape alimua kuitembelea New Habari bili kujali kwamba wana uhasimu wa kisiasa lakini alichokifanya Bashe ni utoto unaolenga kumwaribia Nape.
Mwandishi wa Mwanahalisi aliingiaje kwenye chumba cha habari cha New habari?
Bashe acha siasa za maji taka.
Mazungumzo yaliyochapishwa inaonekana yalikuwa majibishano kati ya Nape na Bashe. Lakini baada ya majibishano hayo kwa lengo la kufanya 'Character assasination' Bashe ameamua kuongeza chumvi aliyoyasema Nape na kuwapa mahasimu wake (Mwanahalisi) ambao wamekuwa wakimwandika vibaya bosi wake (Rostam) ili amgombanishe na Mwenyekiti wake JK.
Bashe anaonyesha haja komaa kisiasa, pamoja na tofauti walizonazo (Nape na Bashe), Nape alimua kuitembelea New Habari bili kujali kwamba wana uhasimu wa kisiasa lakini alichokifanya Bashe ni utoto unaolenga kumwaribia Nape.
Mwandishi wa Mwanahalisi aliingiaje kwenye chumba cha habari cha New habari?
Bashe acha siasa za maji taka.