GE2025 Bashe amlisha kiapo Mwaifunga jukwaani, amuahidi kiwanda cha tumbaku Tabora

GE2025 Bashe amlisha kiapo Mwaifunga jukwaani, amuahidi kiwanda cha tumbaku Tabora

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
844
Reaction score
1,607
Mgombea Ubunge Jimbo la Nzega mjini na Waziri wa Kilimo Hussein Bashe leo Septemba 19,2025 akiwa katika mkutano wa Kampeni kata ya Gongoni Jimbo la Tabora mjini amemlisha kiapo cha kuwatumikia Wananchi Mgombea Ubunge Jimbo la Tabora mjini Hawa Mwaifunga mbele ya wananchi waliohudhuria mkutano huo.

Bashe ameeleza kuwa Mwaifunga ni miongoni mwa wabunge waliokuwa wakimsumbua mara kwa mara kuhusu Kiwanda cha Tumbaku na Kiwanda cha Mbolea.

Bashe ameahidi kuwa viwanda hivyo cha mbolea ya Tumbaku na Kiwanda cha Tumbaku vitajengwa Tabora, hivyo amewataka wananchi wa Tabora kumpigia kura Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi Samia Suluhu, Mbunge Hawa Mwaifunga na Madiwani wa CCM.​

 
Kwamba atakuwa waziri wa kilimo tena?

USSR
 
Back
Top Bottom