BASATA na adhabu ya Shilole

BASATA na adhabu ya Shilole

Kuna popote alipewa adhabu..??

Hawa wanaimbishwa wimbo wasioujua. Ndio maana na mzee mmoja ambaye alishaambiwa abadili jinsia apewe uspika naye kaja na mpya. Eti yeye anauhakika Lowasa ameiba kwenye Richmond kama wanabisha waitishe mdahalo.
Halafu anasema yeye ni mwanasheria! Hao aliosoma nao sii wanajisikia aibu?
 
Mbona UKAWA wanatembea na fisadi, mteja namba moja wa mahamaka maalum ya mjizi na mafisadi ya Magufuli?

Kumbuka kuna cyber crime law unakurupuka na tuhuma usizoweza kuthibitisha. Polisi au mahakama gani likofunguliwa mashitaka kwa tuhuma hizo?? Wakubwa wako wenyewe wanaogopa kuongea hayo hujui unacheza muziki usioujua
 
Shilole alishasamehewa kimya kimya..cz hata barua ya kumfungia sidhani km walimpa
 
Nilimuhurumia sana yule afisa habari wa basata. It is not fair kabisa. Imagine kama wewe ndo ofisa wa basata unakuwa kwenye situation gani
 
"Law is created to protect the rulling class"Plato
 
Mwezi wa sita Shilole alifungiwa na BASATA kutokushiriki shughuli yoyote ya kimziki na sanaa kwa mwaka mmoja, kwa kile kilichosemekana amewadharilisha watanzania pale alipokuwa anatumbuiza kule nchini Swedeni, cha kushangaza msanii huyo amekuwa akizunguza katika kampeni mojawapo za chama cha siasa na BASATA wamekaa kimya tu.

Je, kilikuwa kiini macho au?
 
BASATA ni nyoka wa kijani hawana sumu.
 
..magamba yanahitaji msaada wa kila mtu wkt huu yahurumie tuu
 
Kumbuka kuna cyber crime law unakurupuka na tuhuma usizoweza kuthibitisha. Polisi au mahakama gani likofunguliwa mashitaka kwa tuhuma hizo?? Wakubwa wako wenyewe wanaogopa kuongea hayo hujui unacheza muziki usioujua

Wewe subiri mahakama sisi wananchi tunamjua ni mwizi. Hapa Songea leo tumemuandalia mapokezi maalum ya mwizi.
 
basata zile ulofa na upumbavu tu...havina meno...ingekuwa ukawa balaa sasa..ndio hapo mjue sasa uhalifu ccm.
 
du sheria zinawekwa na wao na wao ndo wanavunja, hii nchi bana, dah
 
lowasa sijui kawakera nini jamani, anavyoshutumiwa, anavyotukanwa du, hiyo yote ni kumvunja nguvu yeye na watu wake, mie ni gamba lakini naona hapa usawa zero kabisa, hawamtendei haki manake wote wanamuandama yeye, ili akate tamaa
 
Mwezi wa sita Shilole alifungiwa na BASATA kutokushiriki shughuli yoyote ya kimziki na sanaa kwa mwaka mmoja, kwa kile kilichosemekana amewadharilisha watanzania pale alipokuwa anatumbuiza kule nchini Swedeni, cha kushangaza msanii huyo amekuwa akizunguza katika kampeni mojawapo za chama cha siasa na BASATA wamekaa kimya tu.

Je, kilikuwa kiini macho au?

Mkuu, alizuia kushiriki shughuli za siasa au sanaa?
 
Back
Top Bottom