BASATA na adhabu ya Shilole

BASATA na adhabu ya Shilole

Mbona UKAWA wanatembea na fisadi, mteja namba moja wa mahamaka maalum ya mjizi na mafisadi ya Magufuli?

Mada inasema nini nawe unajibu nini? Soma tena.
 
Mbona UKAWA wanatembea na fisadi, mteja namba moja wa mahamaka maalum ya mjizi na mafisadi ya Magufuli?

Mpelekeni Mahakamani kama hamjaumbuka na huyo Fisadi kuu lillilojipangisha Magogoni kama halijanasa nalo. hata Magufuli mwenye fisadi hakuna aliyemsafi ndani ya ccm
 
Baraza la sanaa la Taifa (BASATA) ambalo lipo kisheria, majuzi lilimhukumu msanii Shilole asijihusishe na masuala ya sanaa kwa mwaka mmoja kutokana na kukiuka taratibu zilizowekwa na kuvunja maadili. Hivi tunapozungumza msanii huyo yuko kwenye adhabu hiyo.

Lakini jambo la ajabu ni kuwa CCM pamoja na kufahamu adhabu hiyo wao wameidharau na kumchukua Shilole ili aambatane na mgombea wao wa Urais na kupanda majukwaani kushiriki shughuli za muziki kinyume na adhabu yake. Jee hiyo sio dharau kwa mamlaka iliyotoa adhabu?

Basata nao kama jambo hilo lingefanywa na wengine wangekaa kimya kama walivyo sasa?

Nadhani sasa wasanii na watu wengine waelewe kuwa adhabu zinazotolewa na mabaraza haya ni za magazetini tuu hivyo hakuna haja ya kuziheshimu wao waendelee na mambo yao tuu.
View attachment 282612
 
Mbona UKAWA wanatembea na fisadi, mteja namba moja wa mahamaka maalum ya mjizi na mafisadi ya Magufuli?

Correct. Huyo fisadi unayemsema hajahukumiwa na hizo mahakama za kufikirika, tofauti na Shilole ambaye amehukumiwa na Baraza lililopo kisheria; huu utawala wa sheria mnaouhubiri kila siku ni maigizo au!!

Mkuu Nduka sidhani kama hili linapaswa kushabikiwa, kwani wasaniiwameisha, au ndo manawataka wanaomwaga razi... Maana kuna clip za jangwani siku ile ya 23/8 ilikuwa aibu tupu...
 
Last edited by a moderator:
Mbona UKAWA wanatembea na fisadi, mteja namba moja wa mahamaka maalum ya mjizi na mafisadi ya Magufuli?
Kutuhumiwa ni jambo moja na kuhukumiwa ni jambo lingine. Huyo dada kahukumiwa na mamlaka, huyo unayemsema wewe umemtuhumu. au hujui kutofautisha haya mambo?
 
Mbona UKAWA wanatembea na fisadi, mteja namba moja wa mahamaka maalum ya mjizi na mafisadi ya Magufuli?

Adhabu yake ni ipi?. Hoja yako ni tofauti na mada
 
hata waizi wote hujificha chichiemu.
mwizi hujua wapi pa kujificha nikwa mwizi mwenzie.
 
anaeheshimu sheria niyule KIONGOZI ANAESEMA atamwachia mbakaji?ili aje aendeleze kutuharibia watoto wetu?
 
Nyani haoni kundule.

Acha kujitoa ufahamu kwa vitu obvious, wewe unaona ni sawa kuwa na double standards.
mwaka huu mmefumaniwa mkioga uani.mlizoea sana kulaghai wananchi.
Ila niulize kitu kimoja mbona nimesikia Magufuli wenu naye ameanza kucheza ngoma inayopigwa na UKAWA ??!!Eti naye anadai wananchi wanahitaji mabadiliko teh teh teh teh .......... Mkumbusheni ilani ya CCM haisemi hivyo mama .
 
Back
Top Bottom