Barua kwako dada Josephine Mushumbusi

Barua kwako dada Josephine Mushumbusi

Queen Esther

JF-Expert Member
Joined
Apr 5, 2012
Posts
2,206
Reaction score
1,464
Habari kwako dada Josephine.

Kwa muda mrefu sana umekuwa ukitajwa na vyombo vya habari kwa namna isiyopendeza. Aidha washabiki wa UKAWA wamekuwa mstari wa mbele kueneza propaganda kuwa wewe ndio sababu ya Dr. Slaa kujitoa UKAWA.

Ninavyokufahamu wewe ni mcha Mungu na pia umechukuliana na hawa watu kwa muda mrefu. Ila wamekosa shukrani na sasa kila siku umekuwa dustbin ya kutupa kila aina ya uchafu.

Mimi kama mwanamke mwenzio sijaridhika na yanayoendelea hasa mwanamke mwenzangu unavyodhalilishwa. Mwenzio Mama Slaa alijitokeza na kumchafua vizuri kabisa baba watoto wako. Mbona wewe uko KIMYA? Katika barua yangu hii nina kuomba mambo yafuatayo:-

1. Kuombewa na kutolewa mapepo ndio kazi kubwa ya Bwana wetu Yesu Kristo maana ni UKOMBOZI. Hata Gwajima kabla ya kuokoka alikuwa mganga wa kienyeji na yeye binafsi amekiri hilo mara nyingi. Iweje leo akutangazie hivyo hata kama ni kweli.

2. Inawezekana HUNA mapepo ila alikuwa anatumia nguvu zake za Giza kucheza na soul yako. Jikite kwenye maombi na neno la Mungu na kujifunika na Damu ya Yesu Kristo hasa kabla hujalala.

Huo ndio wakati adui hufanya "SPIRITUAL MANIPULATION" kwa kiasi kikubwa. Yanayotokea sasa yalikamilika katika ulimwengu wa roho kwanza.

3. Usipostopisha huu mchezo wa spiritual manipulation uko kwenye hatari nyingi. Vita yako sasa ni Gwajima na wewe na sio Dr. Slaa. Usipoangalia utapoteza kila kitu, Inuka mwanamke simama dai ukombozi kupitia Damu takatifu ya Yesu Kristo Ufunuo 12:11

3. Sinema za MAPEPO za Gwajima ndio kwanza zimeanza. Wakristo wanaoelewa maombi naomba tuliombee Taifa kuliko tulivyowahi kuomba. Hatuhitaji spiritual manipulation kuliongoza Taifa, kila mtu aombe na tusimame kwa UMOJA.

4. Wachungaji wote unaoshirikiana nao halafu wanatoa Siri zako, Kama zipo wapeleke msalabani SAWASAWA na ZABURI ya 35 na 109.

Mungu ni Mungu wa kweli na haki. Huwezi kuwa Mchungaji halafu ukifanya kinyume na maisha ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, that is abomination! Hili jambo sio la kushabikia ni la kukemea.

5. Gwajima anataka aende Ikulu akatawale nchi yetu kwa nguvu za Giza. Ni Damu takatifu ya Yesu Kristo tu, itatuokoa na mapepo haya. Ufunuo 12:11

6. Amka mwanamke, jifunge kibwebwe mauti inapiga hodi mlangoni pako.

7. Watanzania wote tuombe maombi ya kukataa spiritual manipulation yanayofanywa na Mchungaji Gwajima. Tunahitaji Mchungaji wa kutupeleka kwa Bwana Yesu Kristo sio Mchungaji wa kucheza na our souls and mind (mind control).

Josephine you have my prayers.

Mkono wa Bwana haukupunguka usiweze kuokoa na sikio lake sio zito asiweze kusikia kilio chetu. Wawili au watatu wakipatana na sisi ni zaidi ya watatu. Tuombe kwa siku saba kuanzia Leo na tumngoje Bwana kwa majibu.

Kama unaipenda Tanzania ungana nasi katika maombi haya.

MBONA SIKUONA MAHALI POPOTE MCHUNGAJI GWAJIMA AKIWAONGOZA UKAWA AKIWEMO JOSEPHINE NA DR. SLAA SALA YA TOBA KAMA MCHUNGAJI WA KIPENTEKOSTE.

JE AMEMSHAURI MHE. MBOWE AUZE CLUB BILLICANAS IWE KANISA KWANI VIJANA WENGI WANAHARIBIKIA HAPO?????

YEYE KAZI YAKE ALIYOITIWA NA KRISTO YESU NI USHENGA WA KWENDA IKULU TUU???

ALITUAHIDI ATAMFUFUA AMINA CHIFUPA MAANA AMECHUKULIWA MSUKULE - Je hiyo siyo spiritual manipulation????

Fungueni macho ndugu zangu. Maana imeandikwa watu macho lakini hawaoni, wana masikio lakini hawasikii.

HIVI HUYU MCH. GWAJIMA SI NDIO ALIMTUKANA KADINALI PENGO NA KULITUHUMU KANISA KATOLIKI. LEO HII AMEGEUKAJE KUWA MTETEZI WA VIONGOZI WA KANISA KATOLIKI????

MAOMBI NDIO DAWA YA HAYA YOTE... omba hivi!!!
"" EEEEE MUNGU MUUMBA MBINGU NA NCHI, FUNUA MARINDA WATANZANIA TUPONE""
wote tuseme AMEN. AMEN. AMEN mara 7.



QUEEN ESTHER
 
Kuwa tu na mume wa mtu ni kosa sana kiroho, ushauri wako ungefaa sana kama angekuwa na ndoa na huyo Dr Slaa. Mungu hakai sehemu chafu, mwambie kwanza atubu na amrudishe mume wa watu ndo apate baraka za Mungu.
 
Safari hii mtaimba kila aina ya wimbo, hata huyo aliyepo magogoni naye anatumia nguvu za giza. Niambie ni mwana siasa yupi wa ccm aliyepo madarakani kuanzia ngazi ya udiwani mpaka uraisi hajapitia kwa kalumanzila?

Kwa kuanzia niakupe mfano mkubwa, mgombea wako wa uraisi aliisha pitia Samunge kwa babu kugonga kikombe.
 
Ina maana unabariki nyumba ndogo:-D, badala ya kumshauri slaa amrudie Rose  wewe unamshauri mushumbuzi atanue na mume wa mtu:-S, biblia na maombi ya wapi hayo

Naomba nakala ya cheti cha ndoa kati ya Slaa na Rose.

Pia hukumu ni ya Mungu. Hoja yangu hapa ni kiongozi wa dini kutumia spiritual manipulation.

Queen Esther
 
[h=1]Mithali 5[/h]1 Mwanangu, sikiliza hekima yangu; Tega sikio lako, mzisikie akili zangu;
2 Upate kuilinda busara, Na midomo yako iyahifadhi maarifa.
3 Maana midomo ya malaya hudondoza asali, Na kinywa chake ni laini kuliko mafuta;
4 Lakini mwisho wake ni mchungu kuliko pakanga; Ni mkali kama upanga wa makali kuwili.
5 Miguu yake inatelemkia mauti; Hatua zake zinashikamana na kuzimu;
6 Hata asiweze kuiona njia sawa ya uzima; Njia zake ni za kutanga-tanga wala hana habari.
7 Basi, wanangu, nisikilizeni sasa, Wala msiache maneno ya kinywa changu.
8 Itenge njia yako mbali naye, Wala usiukaribie mlango wa nyumba yake.
9 Usije ukawapa wengine heshima yako, Na wakorofi miaka yako;
10 Wageni wasije wakashiba nguvu zako; Kazi zako zikawa ndani ya nyumba ya mgeni;
11 Nawe ukaziombolea siku zako za mwisho, Nyama yako na mwili wako utakapoangamia;
12 Ukasema, Jinsi nilivyochukia maonyo, Na moyo wangu ukadharau kukemewa;
13 Wala sikuisikia sauti ya waalimu wangu, Wala sikuwategea sikio langu walionifundisha!
14 Nalikuwa karibu na kuingia katika maovu yote, Katikati ya mkutano na kusanyiko.
15 Unywe maji ya birika lako mwenyewe, Na maji yenye kububujika katika kisima chako.
16 Je! Chemchemi zako zitawanyike mbali, Na mito ya maji katika njia kuu?
17 Yawe yako mwenyewe peke yako, Wala si ya wageni pamoja nawe.
18 Chemchemi yako ibarikiwe; Nawe umfurahie mke wa ujana wako.
19 Ni ayala apendaye na paa apendezaye; Maziwa yake yakutoshe sikuzote; Na kwa upendo wake ushangilie daima.
20 Mwanangu! Mbona unashangilia malaya, Na kukikumbatia kifua cha mgeni?
21 Kwa maana njia za mwanadamu zi mbele za macho ya Bwana, Na mienendo yake yote huitafakari.
22 Maovu yake yeye yatampata mdhalimu, Naye atashikwa kwa kamba za dhambi zake.
23 Atakufa huyo kwa kukosa maonyo, Naye atapotea kwa wingi wa ujinga wake.
 
mwita ke mwita

Hata shetani analijua neno, tena kwa kutetemeka. Pia alimjaribu Yesu kwa neno!!!

Hoja hapa ni SPIRITUAL MANIPULATION'

Queen Esther

 
Last edited by a moderator:
Binti mleta hoja..huyo Yesu umsemae akuumbie moyo safi wakujifunza kujenga hoja..pole sana kwa kukaukiwa
 
Niliyoyapenda kwenye hotuba ya Ngwajima

1.Ni nini kinachosumbuwa? Kinachosumbuwa ni wakati na majira.

2.wakati wa baridi watu wanavaa makoti, sio kwamba unavaa koti ili iwe baridi, unavaa koti unajiajast na weather

3.Majira ya mtu yakifika huwezi kushindana naye

4.ukiizika kweli kama ni majira yake, kweli inafufuka kwenye majira yake,

Kweli ukiizika inatabia ya kufufuka na ikifufuka haiwezi kufa tena

5.Na mimi ninasema majira haya yaangalieni ni nani mtu wa majira

6.Nahitimisha kwa kusema,
Tanzania, ni kubwa, kuliko watanzania.
watu na matukio yatapita lakini Tanzania itabaki,
katika kupeleka harakati hizi tuhakikishe hatuigawi
Tanzania.

Na nasema tena na tena Mungu ibariki tanzania Mungu ibariki Africa Mungu wabariki watanzania.
 
Safari hii mtaimba kila aina ya wimbo, hata huyo aliyepo magogoni naye anatumia nguvu za giza. Niambie ni mwana siasa yupi wa ccm aliyepo madarakani kuanzia ngazi ya udiwani mpaka uraisi hajapitia kwa kalumanzila?
Kwa kuanzia niakupe mfano mkubwa, mgombea wako wa uraisi aliisha pitia Samunge kwa babu kugonga kikombe.
View attachment 284982
 
Sidhani kama atakusikiliza, mwenzio yupo kwenye mchakato wa kujenga hospitali na shule.
 
Ila kwa mtazamo wangu askofu gwajima kawadhalilisha wanawake kama vile wao hawana maamuzi ndani ya familia.

Josephine na Gwajima nani amewadhalilisha wanawake? Unataka kusema wanawake wana haki ya kuwa madikteta kwa waume zao kama alivyo Josephine?
 
Back
Top Bottom