Barua kwa Dr. W. Slaa

Hapa hakuna dawa nyingine, zaidi ya kukata rufaa. Lazima tuone HAKI inatendeka. Afadhari jimbo libaliki wazi kwa mwaka moja(wote tukose kuwa na Mbunge) kuliko kukimbilia uchaguzi huki tukikigawa chama. Kura 56,000 alizopata Lema ni nyingi sana. Hatua ya kwanza iwe ni kulinda HAKI ya wapiga kura hao wengi.

Tafadhari sana ndugu zanguni, hapa kitu cha kwanza kabisa ni kukata RUFAA.

Time Limitation ya rufaa: Rufaa ya uchaguzi inatakiwa isikilizwe ndani ya mwaka moja. Mwaka huo mmoja utaisha kabla ya 2015. Lazima tuwe principled ktk kulinda na kutetea HAKI, kuliko kukimbilia uchaguzi.
Note well: Tukumbuke kuwa hii HUKUMU isipotenguliwa na mahakama ya juu, basi itakuwa PRECEDENT ambayo itatumikaa kung'oa wabunge wengi wa upinzani hapo baadaye.
Kwenye kukigawa Chama hapo kina point. Kama hawatakata rufaa na Lema akawa amezuiwa kuna dalili za kukigawa Chama.
 
Tunakushukuru Luteni kwa barua yako unajua kwamba arusha ndio dunia na unajua kwamba arusha kila kitu wakubwa wote dunia ikitaka kushuka inashukia AICC sasa unafikiria nini kama sio ulafi wa CCM kwa kweli tunawaambia kwamba hawataipata arusha hata kwa dawa.Wanazidi kujikanyaga arusha sio tunawaambia hivi wamshukuru SLAA ALIYETUAMBIA KWAMBA TUNYAMAZE AMA ZAO AMA ZETU WATU WA ARUSHA TUNGEKUFA NA WAO WAO WANGEKUFA TU.UNAJUA CCM INAPESA WA WANANCHI NDIO WANACHEZEA KATIKA MAMBO YAO YA KIJINGAN HASA PESA YA MJI WA ARUSHA,MBUGA ZA WANYAMA,TANZANITE, NA MENGINEYO MENGI SANA.SEMA TU WANANCHI HAWAJUI HII NCHI TUMESHAUZWA PASIPO SISI KUJUA.WATANZANIA MNATAKIWA KUFIKIRIA MBONA HAWAKUNA MARAIS WANAOKUJA HAPA NCHINI KILA SIKU LAKINI RUTI ZA PRESIDENT WETU HAZIISHI NCHI ZA WEZETU TENA HIZI NCHI KUBWAKUBWA TU.HAKUNA ZINGINE.KWANII ASIWE ANAENDA SOMALIA AU MOZAMBIQUE AU MALAWI ANGALIA RUTI ZAKE ZOTE HALAFU HAKUNA CHOCHOTE ANACHOKWENDA KUFNAY HIZO PESA WANAZOPOTEZA KUSAFIRIA AU KUHARIBU KWENYE UCHAGUZI NI BORA WANGEWALIPA MADAKTARI NA WALIMU WA HAPA TZ WANAOPATA SHIDA.

ASANTENI MUNGU IBARIKI TANZANIA YEYOTE ANAYETAKA KUILETEA TANZANIA MATATIZO NA AKAFE KABLA HAJAMALIZA MDA WAKE.
 
Poleni sana, naona. Chadema mna mawazo. Mkate rufaa msikate yote tisa. Kumi ni kuwashawishi wananchi aw Arusha, mmechangia ni ni katika maendeleo ya Arusha tangu Lema achaguliwe Zanzibar ya fujo na mauajiq. Hata madiwani went hawafanyi kazi yeyote, mchaguliwe tena kwa shughuli gani fujo! Msifikri CCM inafanana makos a kila siku kisha ni nyi mfaidi,Kama mlivyofaidi Arumeru kutokana na makosa ya uteuzii. Ole wenu na kujeadili jiwe. People's itageuka ,kuwa popos.

kijana, 50yrz mmetufanyia nini Watanganyika??
 
Hakuna kitu hapa. Huyo jamaa katumwa na CCM. Rufaa ni muhimu kuliko mbio za kutaka kushika jimbo. Je, wakitumia polisi kutangaza mshindi mgombea wa CCM mtasemaje? Ni muhimu chama kikakata rufaa ili haki itendeke.

Sijaisoma hukumu kamili, ispokuwa nimeongea na mawakili wa CDM, Kimomogoro, Marando, Lissu na Profesa Safari, wote wanaona kuwa kuna haja ya kukata rufaa. Nami nakubaliana nao na napingana na wote wanaosema CDM wasikate rufaa.

Uwezkeno wa rufaa kushinda unatokana na Jaji kushindwa kueleza kasoro za ushahidi. Kushindwa kwa Bartida kufika mahakamani; kushindwa kwa Lowassa kufika mahakamani kuliathiri vipi kesi ya msingi na ushahidi.
Hoja hapa siyo Lema kuwa mbunge, hoja hapa kwa nini Lema aenguliwe kwa mambo ya kijinga?

Pili, kwa hukumu ile Lema atalazimika kulipa gharama za kesi karibu Sh. 50 milioni. Sasa awalipe wahuini Sh. 50 milioni ili iweje?

Tatu, hata kama CDM hawataka rufaa, CCM watakata rufaa kwa kuwa hawataki kuendelea na uchaguzi mdogo. Watakatia yale mambo mengine mawili ambayo hayakuamuliwa.


CDM msikubali ushauri wowote wa kutokata rufaa. Kwanza, hiyo kesi itakwisha kabla ya mwaka huu kwa kuwa sheria inasema, "Rufaa ya kesi za uchaguzi zinatakiwa kumalizika ndani ya kipindi cha mwaka mmoja" tangu hukumu ilipotolewa.

pa1 mkuu. Hapa tusiangalie ubunge wa Lema,tuangalie sheria kama imepindishwa. Chadema kuweni makini msije maamuzi ya hovya,yakaja kukigharimu chama
 
kweli Luteni umenena kama mhimili tuliouamini umetuangusha hatuna aja ya kurudi huko ni walewale tu Lema wetu zunguka nchi kumwaga sumu na kuongeza na kuimalisha matawi tayari kwa 2015 tuangalie mtu makini asimame tutashinda mapambano haya yaliyoanza .kwa upande mwingne naona nuru mbele yetu kwakile walichofanya kwani tutajitangaza zaidi na kujiimalisha zaidi.
 
Ndugu Slaa,

Kwanza niruhusu nitoe pongezi zangu za dhati kabisa kwako binafsi na kwa chama chako cha CHADEMA kwa mafanikio mliyoyapata kwa kipindi kifupi. Natambua kazi mnayoifanya ni nzito na ya hatari maana wengi wanatamani kuwa kama ninyi lakini wanaogopa kutangulia ila nyie mmesema mnatangulia wengine watawakuta mbele ya safari. Kwa hilo hongera sana.

Bila kupoteza muda kutaja mafanikio mliyoyapata naomba nijikite moja kwa moja kwenye kiini cha barua hii.

Kabla sijasahau naomba chama kisikate rufaa kwa kesi ya Lema.

Naomba nikukumbushe tu kwamba kwenye uchaguzi mkuu wa 2010 CCM hawakutaka si tu nyie mshinde bali msiongeze wabunge wa kuchaguliwa. Utakumbuka matamshi ya aliyekuwa Katibu mkuu wa CCM ndugu Makamba alipowaambia wanachama wa CCM kwenda kutafuta sababu yeyote ile wafungue kesi kupinga ushindi wa wabunge wa Chadema na chama kitagharamia kesi? Yanayotokea sasa ni utekelezaji tumjiandae kwa makubwa.

Utekelezaji wa hukumu ya Lema ni mwanzo tu ya mipango mingi ya CCM kuihujumu Chadema. Mpango ulikuwa trh 1-4 washinde Arumeru Mashariki halafu trh 5-4 ushindi wa Lema utenguliwe na sherehe kubwa yakupongezana ilikuwa ifanyike weekend hii mjini Arusha. Najua hilo limeshindikana.

Hukumu ya kupinga ushindi wa Lema si kwamba Jaji kajichanganya ni mtego wa makusudi ili nyie mjichanganye waendelee na plan B,C. Lengo lao ni kuikamata Arusha kwa hali yeyote kwa vile wanajua fika hawawezi kuikamata kwa kutumia sanduku la kura, kwa hiyo njia iliyobaki ni kutumia mahakama na pingamizi. Narudia tena msikate rufaa.

Lema amehukumiwa kwa kifungu 108 ‘Illegal Campaign' kinachomruhusu kugombea lakini kwenye majumuisho ya hukumu imeandikwa kahukumiwa kwa kifungu 114 "Illegal Practice" kinachomuzuia kugombea kwa miaka 5. Wanataka mkate rufaa au muombe ku review case na hapo itacheleweshwa mwisho mtaambiwa muda ni mfupi wa kuitisha uchaguzi.

CCM imeanza kuhaha baada ya kuona hamna mpango wa kukata rufaa, wanachosubiri ni Lema ateuliwe kugombea wamuwekee pingamizi, believe me or not lazima ataondolewa hata kama mtakuwa na hukumu mkononi.

Ndugu Slaa, CCM wameshafanya kosa wanajishauri endapo waingie kwenye uchaguzi ama la. Ushauri wangu ni kuwa, whatever the case, nendeni kwenye uchaguzi hata kama Lema hatogombea najua mtapata mgombea mwingine makini. Kama chama kitaona Lema asigombee, apewe kazi makao makuu ya kukiimarisha chama, akusaidie kuzunguka nchi nzima hasa katika kuimarisha matawi tayari kwa uchaguzi wa ndani na wa serikali za mitaa.

Nawatakia mafanikio mema katika ukombozi, najua kadritaabu zinavyozidi ndivyo ukombozi unavyokaribia.


Luteni.
Kwa kuongezea tu na kwa msisitizo mkubwa kwako Mh Dr.Slaa...kama unasoma huu ujumbe...please please......kesi hii ina mambo mengi kwani hata kama hamtakata rufaa na mkaamua kumsimamisha Lema...bado kutakuwa na mizenge tele ya delaying tactics.....USHAURI KWAKO DR.SLAA...TAFADHALI WAKUSIMAMISHE WEWE UGOMBEE UBUNGE ARUSHA.CHADEMA WASIMSIMAMISHE MTU MWINGINE ARUSHA ZAIDI YA DR.SLAA.IKUMBUKWE KUWA ARUSHA INA MATATIZO MENGI YA MADIWANI AMBAYO HAYAJAPATIWA UFUMBUZI......PIA ARUSHA NI JIMBO KUBWA TZ.....NA NDIO MAANA CCM WANALITAKA...HASWA JK....HIVYO ASIMAME DR.SLAA MWENYEWE ARUSHA ACHUKUE JIMBO TAFADHALI...ATASAIDIA KUONDOA MIGOGORO ARUSHA KWA KIPINDI HIKI MPAKA 2015....
ANGALIZO: HATA MH.MBOWE ILIBIDI AGOMBEE HAI ILI KULINUSURU JIMBO PAMOJA NA KUWA YEYE NI CHAIRMAN NA ALISHAWAHI KUGOMBEA URAIS...HIVYO SHIME MSIKATE RUFAA NA MSIMAMISHENI DR.SLAA ARUSHA MUIMALIZE CCM.ARUSHA INAHITAJI MTU MZITO KAMA DR.SLAA......LEMA ATAENDELEA KUFANYA KAZI ZA dR.SLAA WAKATI DR.SLAA YUKO BUNGENI........this is my very important suggestion to CDM
 
Mwendo ni uleule wa farasi kamanda 'pipa kura linda kura'kama unaweza unaweza tu hata pasipo mvua radi zitapiga tu... Kwani CDM waende mahakamani umeambiwa wao ni magamba?make CDM inachaguliwa na nguvu ya umma na si nguvu ya mahakama
 
Iwapo ikishindikana.kamanda lema azunguke nchi nzima kutoa elimu,chondechonde Dr.slaa mtume Lema Bukoba vijijini,wanataka mabadiliko ila bado hamjawekeza kule.kwanini!!?
 
Mimi kwa uelewa wangu mdogo tu ningeona Chadema ikate rufaa kwa sababu hukumu inamapungufu mengi sana
 
Hakuna kitu hapa. Huyo jamaa katumwa na CCM. Rufaa ni muhimu kuliko mbio za kutaka kushika jimbo. Je, wakitumia polisi kutangaza mshindi mgombea wa CCM mtasemaje? Ni muhimu chama kikakata rufaa ili haki itendeke.

Sijaisoma hukumu kamili, ispokuwa nimeongea na mawakili wa CDM, Kimomogoro, Marando, Lissu na Profesa Safari, wote wanaona kuwa kuna haja ya kukata rufaa. Nami nakubaliana nao na napingana na wote wanaosema CDM wasikate rufaa.

Uwezkeno wa rufaa kushinda unatokana na Jaji kushindwa kueleza kasoro za ushahidi. Kushindwa kwa Bartida kufika mahakamani; kushindwa kwa Lowassa kufika mahakamani kuliathiri vipi kesi ya msingi na ushahidi.
Hoja hapa siyo Lema kuwa mbunge, hoja hapa kwa nini Lema aenguliwe kwa mambo ya kijinga?

Pili, kwa hukumu ile Lema atalazimika kulipa gharama za kesi karibu Sh. 50 milioni. Sasa awalipe wahuini Sh. 50 milioni ili iweje?

Tatu, hata kama CDM hawataka rufaa, CCM watakata rufaa kwa kuwa hawataki kuendelea na uchaguzi mdogo. Watakatia yale mambo mengine mawili ambayo hayakuamuliwa.


CDM msikubali ushauri wowote wa kutokata rufaa. Kwanza, hiyo kesi itakwisha kabla ya mwaka huu kwa kuwa sheria inasema, "Rufaa ya kesi za uchaguzi zinatakiwa kumalizika ndani ya kipindi cha mwaka mmoja" tangu hukumu ilipotolewa.
Spanner unachosema kina msingi endapo haki itapatikana mahakamani....lakini hoja ya msingi hapa ni kuwa inaonekana haki imepindishwa mahakamani kwa hukumu hii na hivyo msingi wa kuirudisha kesi hii mahakamani unakosekana....tayari mahakama kuu imeshaonesha kuwanyima haki raia waliomchagua Lema sasa kwanini utegemee haki ipatikane huko huko mahakamani????msingi wa hoja hapa ni kurudia uchaguzi ili hukumu itolewe na wananchi wenyewe......Ieleweke wanaonyimwa haki hapa si Lema bali wananchi waliomchagua Lema....ni hawahawa wananchi watakaotoa hukumu ya kesi hii kwa njia ya kura....Hoja ya polisi kutangaza matokeo ni sawa tu na hoja ya rufaa kukataliwa....hivyo hapa ni kupima probability....kwamba wapi haki inaonekana itatendeka??????????BADO NASISISTIZA CDM WASIKATE RUFAA BALI WARUDIE UCHAGUZI KWA KUMSIMAMISHA MTU MAKINI AMBAYE NI DR.SLAA......HII ITAKATA MZIZI WA HILA ZA CCM ARUSHA....BELIEVE ME..........
 
una uhakika gani kuwa wakikata rufaa watashinda????mahakama zenyewe si ndio hizi hizi????
 
Wara hii naona vita sasa kuliko mambo yanavoenda"bora vita ya haki" LEMA.wasitutishe ndugu zangu kama ni vita na ianze wanadhalilisha sana utu wetu..
 
Jamani,CDM ina wanasheria na kama kupata habari toka jikoni CDM ndo champions,hebu tuwaachieni wafanye maamuzi yaliyo sahihi.Lengo la hukumu na mipango yote Dr. aliijua mapema ndo maana alimpigia Kamanda Lema juu ya hukumu hata kabla ya kwenda mahakamani!Ushauri ni mzuri na yote yanafaa na kukubarika lakin tuwaachie makamanda ambao hawalali sababu ya "Movement for change......"
 
Asante Luteni kwa barua yako nafikiri Dr. Slaa atakuwa ameipata.

Kama ulivyoshauri katika barua yako CDM wasikate rufaa na mimi niko na wewe kwa 100%. Jambo la msingi ni kuwa politically jimbo la Arusha mjini ni muhimu kwa sana kwa CDM, kulipoteza litakuwa pigo kubwa kwa chama. Najua kuna watu watasema Lema atapoteza haki yake ya msingi au hukumu yake itatumika kama reference kwa hukumu zingine, ni kweli na si kweli kwa upande mwingine. Hakimu atakayetumia hukumu kama hii yenye utata atazidi kuidhalilisha mahakama na taaluma yake.

Wanaotaka Lema akatafute haki mahakama za juu hawajui kuwa hii kesi ni planned, sote tunajua mahakama zetu zilivyo siyo independent yaliyotokea yanaweza kutokea tena yakawa na impact mbaya zaidi kwake Lema, kwa chama na kwa wananchi wa Arusha mjini wanaweza wasiwe na mwakilishi kwa kipindi kirefu. Waliomvua ubunge Lema hawakufanya kwa bahati mbaya wanajua wanafanya nini kwa hiyo wamejiandaa watafanya nini endapo CDM watakata rufaa. Mwisho nikupongeze tu kwa draft nzuri ya barua yako nafikiri imekuja kwa muda mwafaka.
 
Hello Wanajamii Forum, ni mara ya kwanza kujiunga, nawatakia kazi njema na ninaunga mkono hoja ya Luteni....Tupo pamoja...
 
Nazidi kukazia ushauri wangu kuwa CDM ikate rufaa kwa grounds zifuatazo:

1.Jaji haja fuata utaratibu wa kisheria wa kutoa adhabu. Adhabu ya kusimamishwa kugombea tena hakuitaja, ingawa alitumia s.114, bila yeye kuwa specific ktk kutoa adhabu.(It is fatal per se).

2.Katika hukumu yake alitumia ushahidi wa upande mmoja wa walalamikaji tu.Hakuzingatia wala kuuchambua ushahidi wa wakili wa mlalamikiwa. Kwa tendo hili jaji amekiuka the Golden principal of Natura Justice: The right to be heard (Audi alteram partem).
3.Katika kesi hii ambayo msingi wake(cause of action) ni udhalilishaji, Mtu mwenye na Locus Standi ni Dr. Burian against the whole world. Wa pili ni Lowassa. Hao waliofungua kesi ni wageni(they are strangers).katika kesi za defamation hakuna wa kuirithi.

Tujikumbushe kwenye Law of Torts:
An actionable defamatory statement has three ingredients for it to stand:
i)It must be published.
ii)it must refer to the complainant(plaintiff).
iii)It must be false.


4.Pia jaji ilibidi ajiulize juu ya ukweli au uwongo wa kauli alizosema kwenye mikutano hiyo.Kupima ukweli au uwongo wa hili mahakama ilitakiwa kumuita Dr.Burian na E.Lowassa waje wahojiwe na mahakama na mawakili wa pande zote ili kujua ukweli uko wapi. Pia ulihitajika ushahidi wa kitaalam(expert opinion) i.e DNA test ya mtoto wa Dr.Burian, ili kujiridhisha juu ya baba halali wa mtoto huyo. Ingethibitika kuwa alichosema Lema ni ukweli, basi Lema hangetiwa hatiani kwa sababu ya defense ya JUSTIFICATION(amesema ukweli).

Kwakweli hukumu hii ni kichekesho mtupu. Dawa ni kukata rufaa, si vinginevyo. CDM wakikata rufaa Lema atarudi Bungeni. Labda mahakama ya rufaa ifisadi tena.
 
Back
Top Bottom