Barua kwa Dr. W. Slaa

Barua kwa Dr. W. Slaa

Nimevutiwa sana na jinsi watu walivyo na uchungu na jambo la kutafuta haki. Basi kwa majumuisho tuseme CDM ifanye kile ambacho kitaipa uwezekana wa kulibakiza jimbo la Arusha. Kwa hali ilivyo wananchi wako tayari kwa hilo, ninachomaanisha ni mazingira ya kisheria yatakayofanikisha hilo. Ikiwa rufaa ndiyo itakayoipa Chadema legitimacy ya hata tu kuingia kwenye uchaguzi, basi hilo lifanyike bila kigugumizi. Lakini ikiwa inawezekana kuepuka hilo na kuingia kwenye uchaguzi, acha tu waje tuwabutue. Kulipa milioni 50 kwa ajili ya kuokoa maisha ya watanzania si jambo baya, tena hawa huwa wanaiba zaidi ya hizo bila ridhaa yetu. Tunawapa milioni hamsini kama chambo, wakimeza tu, tunawaburuza nje na kuwabanika kama samaki ng'onda. Hawajui tumewachoka sasa na hatuwataki tena hawa hata wafanyaje.
 
Hujaeleweka mkuu unaweza kudadavua chama kitagawikaje hapa.
Mkuu kuna post nimesema viongozi wa juu wa CDM of course na viongozi wa serikali pamoja na wafanyabiashara wakubwa wa Arusha hawako comfortable na Lema. Pia kada ya kati haiko comfortable naye ila ana mtaji mkubwa sana wa vijana wa Arusha na vitongoji vyake. Viongozi wanamuona ni mtu wa vurugu. Wafanyabiashara wanamuona anawaharibia biashara zao kwa kuwaogofya watu kutembelea Arusha. Hivyo basi kama Lema atakuwa amezuiwa kugombea kwa miaka itakuwa ni nafasi nzuri ya hayo makundi kumweka nje. Hivyo basi CDM haitakata rufaa na itaamua kumsimamisha mtu mwingine na kwa hakika watashinda. Ila sasa nimjuavyo Lema hatakubali kirahisi kuwekwa kando yeye atataka kukata rufaa. Hapo ndipo panapokuja hilo la kukigawa chama. Inaweza ikawa siyo kukigawa mapande bali kukigawa mawazo gongana mengi.
 
Mkuu kuna post nimesema viongozi wa juu wa CDM of course na viongozi wa serikali pamoja na wafanyabiashara wakubwa wa Arusha hawako comfortable na Lema. Pia kada ya kati haiko comfortable naye ila ana mtaji mkubwa sana wa vijana wa Arusha na vitongoji vyake. Viongozi wanamuona ni mtu wa vurugu. Wafanyabiashara wanamuona anawaharibia biashara zao kwa kuwaogofya watu kutembelea Arusha. Hivyo basi kama Lema atakuwa amezuiwa kugombea kwa miaka itakuwa ni nafasi nzuri ya hayo makundi kumweka nje. Hivyo basi CDM haitakata rufaa na itaamua kumsimamisha mtu mwingine na kwa hakika watashinda. Ila sasa nimjuavyo Lema hatakubali kirahisi kuwekwa kando yeye atataka kukata rufaa. Hapo ndipo panapokuja hilo la kukigawa chama. Inaweza ikawa siyo kukigawa mapande bali kukigawa mawazo gongana mengi.
Mbona unasema uongo aisee.... Lema mwenyewe amesema hakati rufaa akaenda mbele zaidi akasema hataki kuwa mbunge wa mahakama sasa wewe unaleta hadithi gani tena.
 
Mbona unasema uongo aisee.... Lema mwenyewe amesema hakati rufaa akaenda mbele zaidi akasema hataki kuwa mbunge wa mahakama sasa wewe unaleta hadithi gani tena.
Mkuu alisema hata kama atakuwa amezuiwa kugombea? Kuna vitu viwili hapa: Kuna kukata rufaa kama Lema atakuwa amezuiwa kugombea kwa miaka mitano ili mahakama imtakase na kuweza kugombea. Kuna kutokata rufaa kwa kuwa Lema hajazuiwa kugombea hivyo ana nafasi ya kurudi kugombea ndani y siku 90 na ku retain kiti chake.
 
Luteni umenena safi, but tukiachie chama kitaamua kina wanasheria wazuri waichakachue vizuri hii issue, na amin watakuja na zuri.... mungu bariki CCM.
 
[TABLE="width: 500"]
[TR]
[TD]
Barua kwa Dr. W. Slaa
Ndugu Slaa,

Kwanza niruhusu nitoe pongezi zangu za dhati kabisa kwako binafsi na kwa chama chako cha CHADEMA kwa mafanikio mliyoyapata kwa kipindi kifupi. Natambua kazi mnayoifanya ni nzito na ya hatari maana wengi wanatamani kuwa kama ninyi lakini wanaogopa kutangulia ila nyie mmesema mnatangulia wengine watawakuta mbele ya safari. Kwa hilo hongera sana.

Bila kupoteza muda kutaja mafanikio mliyoyapata naomba nijikite moja kwa moja kwenye kiini cha barua hii.

Kabla sijasahau naomba chama kisikate rufaa kwa kesi ya Lema.

Naomba nikukumbushe tu kwamba kwenye uchaguzi mkuu wa 2010 CCM hawakutaka si tu nyie mshinde bali msiongeze wabunge wa kuchaguliwa. Utakumbuka matamshi ya aliyekuwa Katibu mkuu wa CCM ndugu Makamba alipowaambia wanachama wa CCM kwenda kutafuta sababu yeyote ile wafungue kesi kupinga ushindi wa wabunge wa Chadema na chama kitagharamia kesi? Yanayotokea sasa ni utekelezaji tumjiandae kwa makubwa.

Utekelezaji wa hukumu ya Lema ni mwanzo tu ya mipango mingi ya CCM kuihujumu Chadema. Mpango ulikuwa trh 1-4 washinde Arumeru Mashariki halafu trh 5-4 ushindi wa Lema utenguliwe na sherehe kubwa yakupongezana ilikuwa ifanyike weekend hii mjini Arusha. Najua hilo limeshindikana.

Hukumu ya kupinga ushindi wa Lema si kwamba Jaji kajichanganya ni mtego wa makusudi ili nyie mjichanganye waendelee na plan B,C. Lengo lao ni kuikamata Arusha kwa hali yeyote kwa vile wanajua fika hawawezi kuikamata kwa kutumia sanduku la kura, kwa hiyo njia iliyobaki ni kutumia mahakama na pingamizi. Narudia tena msikate rufaa.

Lema amehukumiwa kwa kifungu 108 ‘Illegal Campaign’ kinachomruhusu kugombea lakini kwenye majumuisho ya hukumu imeandikwa kahukumiwa kwa kifungu 114 “Illegal Practice” kinachomuzuia kugombea kwa miaka 5. Wanataka mkate rufaa au muombe ku review case na hapo itacheleweshwa mwisho mtaambiwa muda ni mfupi wa kuitisha uchaguzi.

CCM imeanza kuhaha baada ya kuona hamna mpango wa kukata rufaa, wanachosubiri ni Lema ateuliwe kugombea wamuwekee pingamizi, believe me or not lazima ataondolewa hata kama mtakuwa na hukumu mkononi.

Ndugu Slaa, CCM wameshafanya kosa wanajishauri endapo waingie kwenye uchaguzi ama la. Ushauri wangu ni kuwa, whatever the case, nendeni kwenye uchaguzi hata kama Lema hatogombea najua mtapata mgombea mwingine makini. Kama chama kitaona Lema asigombee, apewe kazi makao makuu ya kukiimarisha chama, akusaidie kuzunguka nchi nzima hasa katika kuimarisha matawi tayari kwa uchaguzi wa ndani na wa serikali za mitaa.

Nawatakia mafanikio mema katika ukombozi, najua kadritaabu zinavyozidi ndivyo ukombozi unavyokaribia.


Luteni.






[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

Wellsaid mkuu
 
Mkuu alisema hata kama atakuwa amezuiwa kugombea? Kuna vitu viwili hapa: Kuna kukata rufaa kama Lema atakuwa amezuiwa kugombea kwa miaka mitano ili mahakama imtakase na kuweza kugombea. Kuna kutokata rufaa kwa kuwa Lema hajazuiwa kugombea hivyo ana nafasi ya kurudi kugombea ndani y siku 90 na ku retain kiti chake.
Ninavyojua mimi kama ni kuzuiwa kwa miaka mitano anaweza kukata rufaa muda wowote hata baada ya uchaguzi kufanyika ili asafishwe kwa ajili ya 2015, kuliko kuzuia uchaguzi na watu kubaki bila mwakilishi (amelisema hili). Kumbuka aliyezuiwa ni Lema si chama na yeye amesema anasubiri maamuzi ya chama ninavyomjua Lema alivyo loyal kwa chama chake sidhani kama anaweza kwenda against na chama chake.
 
Tulianza na Mungu na tutamaliza na Mungu.VIVA CHADEMA.
 
Ninavyojua mimi kama ni kuzuiwa kwa miaka mitano anaweza kukata rufaa muda wowote hata baada ya uchaguzi kufanyika ili asafishwe kwa ajili ya 2015, kuliko kuzuia uchaguzi na watu kubaki bila mwakilishi (amelisema hili). Kumbuka aliyezuiwa ni Lema si chama na yeye amesema anasubiri maamuzi ya chama ninavyomjua Lema alivyo loyal kwa chama chake sidhani kama anaweza kwenda against na chama chake.
Anaweza akawa loyal ila nyuma yake kuna kundi la vijana ambalo wanaona bila Lema hakuna Arusha!
 
Chadema Mungu awatangulie mfanye maamuzi sahihi kwa umakini mkubwa kwa faida chama na taifa kwa ujumla.
 
Ndugu Slaa,

Kwanza niruhusu nitoe pongezi zangu za dhati kabisa kwako binafsi na kwa chama chako cha CHADEMA kwa mafanikio mliyoyapata kwa kipindi kifupi. Natambua kazi mnayoifanya ni nzito na ya hatari maana wengi wanatamani kuwa kama ninyi lakini wanaogopa kutangulia ila nyie mmesema mnatangulia wengine watawakuta mbele ya safari. Kwa hilo hongera sana.

Bila kupoteza muda kutaja mafanikio mliyoyapata naomba nijikite moja kwa moja kwenye kiini cha barua hii.

Kabla sijasahau naomba chama kisikate rufaa kwa kesi ya Lema.

Naomba nikukumbushe tu kwamba kwenye uchaguzi mkuu wa 2010 CCM hawakutaka si tu nyie mshinde bali msiongeze wabunge wa kuchaguliwa. Utakumbuka matamshi ya aliyekuwa Katibu mkuu wa CCM ndugu Makamba alipowaambia wanachama wa CCM kwenda kutafuta sababu yeyote ile wafungue kesi kupinga ushindi wa wabunge wa Chadema na chama kitagharamia kesi? Yanayotokea sasa ni utekelezaji tumjiandae kwa makubwa.

Utekelezaji wa hukumu ya Lema ni mwanzo tu ya mipango mingi ya CCM kuihujumu Chadema. Mpango ulikuwa trh 1-4 washinde Arumeru Mashariki halafu trh 5-4 ushindi wa Lema utenguliwe na sherehe kubwa yakupongezana ilikuwa ifanyike weekend hii mjini Arusha. Najua hilo limeshindikana.

Hukumu ya kupinga ushindi wa Lema si kwamba Jaji kajichanganya ni mtego wa makusudi ili nyie mjichanganye waendelee na plan B,C. Lengo lao ni kuikamata Arusha kwa hali yeyote kwa vile wanajua fika hawawezi kuikamata kwa kutumia sanduku la kura, kwa hiyo njia iliyobaki ni kutumia mahakama na pingamizi. Narudia tena msikate rufaa.

Lema amehukumiwa kwa kifungu 108 ‘Illegal Campaign’ kinachomruhusu kugombea lakini kwenye majumuisho ya hukumu imeandikwa kahukumiwa kwa kifungu 114 “Illegal Practice” kinachomuzuia kugombea kwa miaka 5. Wanataka mkate rufaa au muombe ku review case na hapo itacheleweshwa mwisho mtaambiwa muda ni mfupi wa kuitisha uchaguzi.

CCM imeanza kuhaha baada ya kuona hamna mpango wa kukata rufaa, wanachosubiri ni Lema ateuliwe kugombea wamuwekee pingamizi, believe me or not lazima ataondolewa hata kama mtakuwa na hukumu mkononi.

Ndugu Slaa, CCM wameshafanya kosa wanajishauri endapo waingie kwenye uchaguzi ama la. Ushauri wangu ni kuwa, whatever the case, nendeni kwenye uchaguzi hata kama Lema hatogombea najua mtapata mgombea mwingine makini. Kama chama kitaona Lema asigombee, apewe kazi makao makuu ya kukiimarisha chama, akusaidie kuzunguka nchi nzima hasa katika kuimarisha matawi tayari kwa uchaguzi wa ndani na wa serikali za mitaa.

Nawatakia mafanikio mema katika ukombozi, najua kadritaabu zinavyozidi ndivyo ukombozi unavyokaribia.


Luteni.

Nakuaminia mkuu, ushauri mzuri.
Chondechonde CDM pamoja na kuw na wansheria wengi waliobobea, kuweni makini sana, mtego uliowekwa ni mkali.
 
Kitu kinachotakiwa ni kukata rufaa kwa mahakama ya wananchi ambayo kuhongeka si rahisi, hizi mahakama zingine zote hamuwezi kuni convince.
 
Ndugu Slaa, CCM wameshafanya kosa wanajishauri endapo
waingie kwenye uchaguzi ama la. Ushauri wangu ni kuwa,
whatever the case, nendeni kwenye uchaguzi hata kama Lema
hatogombea najua mtapata mgombea mwingine makini. Kama
chama kitaona Lema asigombee, apewe kazi makao makuu ya
kukiimarisha chama, akusaidie kuzunguka nchi nzima hasa katika
kuimarisha matawi tayari kwa uchaguzi wa ndani na wa serikali za
mitaa.
IMENIKUNA SANA HII!
 
Mkuu alisema hata kama atakuwa amezuiwa kugombea? Kuna vitu viwili hapa: Kuna kukata rufaa kama Lema atakuwa amezuiwa kugombea kwa miaka mitano ili mahakama imtakase na kuweza kugombea. Kuna kutokata rufaa kwa kuwa Lema hajazuiwa kugombea hivyo ana nafasi ya kurudi kugombea ndani y siku 90 na ku retain kiti chake.

Mkuu jaribu kuelewa jinsi Jaji alivyolikoroga kwa makusudi kabisa na si bahati mbaya, mtego wao CCM na huyo Jaji wao ni huu hapa,

"Lema amehukumiwa kwa kifungu 108 ‘Illegal Campaign' kinachomruhusu kugombea lakini kwenye majumuisho ya hukumu imeandikwa kahukumiwa kwa kifungu 114 "Illegal Practice" kinachomuzuia kugombea kwa miaka 5. Wanataka mkate rufaa au muombe ku review case na hapo itacheleweshwa mwisho mtaambiwa muda ni mfupi wa kuitisha uchaguzi."
 
Nazidi kukazia ushauri wangu kuwa CDM ikate rufaa kwa grounds zifuatazo:

1.Jaji haja fuata utaratibu wa kisheria wa kutoa adhabu. Adhabu ya kusimamishwa kugombea tena hakuitaja, ingawa alitumia s.114, bila yeye kuwa specific ktk kutoa adhabu.(It is fatal per se).

2.Katika hukumu yake alitumia ushahidi wa upande mmoja wa walalamikaji tu.Hakuzingatia wala kuuchambua ushahidi wa wakili wa mlalamikiwa. Kwa tendo hili jaji amekiuka the Golden principal of Natura Justice: The right to be heard (Audi alteram partem).
3.Katika kesi hii ambayo msingi wake(cause of action) ni udhalilishaji, Mtu mwenye na Locus Standi ni Dr. Burian against the whole world. Wa pili ni Lowassa. Hao waliofungua kesi ni wageni(they are strangers).katika kesi za defamation hakuna wa kuirithi.

Tujikumbushe kwenye Law of Torts:
An actionable defamatory statement has three ingredients for it to stand:
i)It must be published.
ii)it must refer to the complainant(plaintiff).
iii)It must be false.


4.Pia jaji ilibidi ajiulize juu ya ukweli au uwongo wa kauli alizosema kwenye mikutano hiyo.Kupima ukweli au uwongo wa hili mahakama ilitakiwa kumuita Dr.Burian na E.Lowassa waje wahojiwe na mahakama na mawakili wa pande zote ili kujua ukweli uko wapi. Pia ulihitajika ushahidi wa kitaalam(expert opinion) i.e DNA test ya mtoto wa Dr.Burian, ili kujiridhisha juu ya baba halali wa mtoto huyo. Ingethibitika kuwa alichosema Lema ni ukweli, basi Lema hangetiwa hatiani kwa sababu ya defense ya JUSTIFICATION(amesema ukweli).

Kwakweli hukumu hii ni kichekesho mtupu. Dawa ni kukata rufaa, si vinginevyo. CDM wakikata rufaa Lema atarudi Bungeni. Labda mahakama ya rufaa ifisadi tena.
jaji hajafuata sheria......kapindisha vingele na hata kutengua ubunge...usitegemee haki itendeke mahakamani kwa hii issue kabisa......bora warudie uchaguzi na wananchi watoe hukumu wenyewe....Pia kama wale makada wa ccm walioshinda kesi wakiamua kukata rufaa kwa ajili ya vile vipengele vilivyotupwa nje..then hapa CDM wanaweza ku counter appeal all together......
 
Nimependezwa sana na ushauri wako luteni. Kwa mtazamo wangu ninaomba Dr W Slaa agombee ili arudi bungeni kupambana ili pia watanzania wengine wamfahamu vizuri.
 
Back
Top Bottom