Barua kwa Dr. W. Slaa

Hakuna kitu hapa. Huyo jamaa katumwa na CCM. Rufaa ni muhimu kuliko mbio za kutaka kushika jimbo. Je, wakitumia polisi kutangaza mshindi mgombea wa CCM mtasemaje? Ni muhimu chama kikakata rufaa ili haki itendeke.

Sijaisoma hukumu kamili, ispokuwa nimeongea na mawakili wa CDM, Kimomogoro, Marando, Lissu na Profesa Safari, wote wanaona kuwa kuna haja ya kukata rufaa. Nami nakubaliana nao na napingana na wote wanaosema CDM wasikate rufaa.

Uwezkeno wa rufaa kushinda unatokana na Jaji kushindwa kueleza kasoro za ushahidi. Kushindwa kwa Bartida kufika mahakamani; kushindwa kwa Lowassa kufika mahakamani kuliathiri vipi kesi ya msingi na ushahidi.
Hoja hapa siyo Lema kuwa mbunge, hoja hapa kwa nini Lema aenguliwe kwa mambo ya kijinga?

Pili, kwa hukumu ile Lema atalazimika kulipa gharama za kesi karibu Sh. 50 milioni. Sasa awalipe wahuini Sh. 50 milioni ili iweje?

Tatu, hata kama CDM hawataka rufaa, CCM watakata rufaa kwa kuwa hawataki kuendelea na uchaguzi mdogo. Watakatia yale mambo mengine mawili ambayo hayakuamuliwa.


CDM msikubali ushauri wowote wa kutokata rufaa. Kwanza, hiyo kesi itakwisha kabla ya mwaka huu kwa kuwa sheria inasema, "Rufaa ya kesi za uchaguzi zinatakiwa kumalizika ndani ya kipindi cha mwaka mmoja" tangu hukumu ilipotolewa.
Je umetumwa au uko serious na unachosema,maana akiniingii akilini. Jimbo linaweza kuwa wazi mpaka 2015 kutokana na mizengwe ya ccm.Unakua kama huwajui ccm au kweli huwajui? Labda nikukumbushe kuwa ndo wenye dola. Luten yuko sahihi.
 
Mkuu Luten wewe kweli ni Luten nakukubali sana kwa barua hii nzuri wewe ni Kamanda,Be blessed raia mwema na mpenda maendeleo
 
Hakuna kitu hapa. Huyo jamaa katumwa na CCM. Rufaa ni muhimu kuliko mbio za kutaka kushika jimbo. Je, wakitumia polisi kutangaza mshindi mgombea wa CCM mtasemaje? Ni muhimu chama kikakata rufaa ili haki itendeke.

Sijaisoma hukumu kamili, ispokuwa nimeongea na mawakili wa CDM, Kimomogoro, Marando, Lissu na Profesa Safari, wote wanaona kuwa kuna haja ya kukata rufaa. Nami nakubaliana nao na napingana na wote wanaosema CDM wasikate rufaa.

Uwezkeno wa rufaa kushinda unatokana na Jaji kushindwa kueleza kasoro za ushahidi. Kushindwa kwa Bartida kufika mahakamani; kushindwa kwa Lowassa kufika mahakamani kuliathiri vipi kesi ya msingi na ushahidi.
Hoja hapa siyo Lema kuwa mbunge, hoja hapa kwa nini Lema aenguliwe kwa mambo ya kijinga?

Pili, kwa hukumu ile Lema atalazimika kulipa gharama za kesi karibu Sh. 50 milioni. Sasa awalipe wahuini Sh. 50 milioni ili iweje?

Tatu, hata kama CDM hawataka rufaa, CCM watakata rufaa kwa kuwa hawataki kuendelea na uchaguzi mdogo. Watakatia yale mambo mengine mawili ambayo hayakuamuliwa.


CDM msikubali ushauri wowote wa kutokata rufaa. Kwanza, hiyo kesi itakwisha kabla ya mwaka huu kwa kuwa sheria inasema, "Rufaa ya kesi za uchaguzi zinatakiwa kumalizika ndani ya kipindi cha mwaka mmoja" tangu hukumu ilipotolewa.

du kama kuna kulipa mil 50 kuwapa magamba hata mimi naunga mkono lufaa pia mahakama itakua inajiweka pahala pabaya kubaki la judgement ya hovyo(precedent)
nahisi pia kweli CCM inaweza kukata rufaa kujifanya na wao hawakulidhika na maamuzi bila hivyo itakula kwao na ni aibu
 
Huu sasa ni mchezo wa paka na panya,chadema lazime watulize kichwa kwenye hili jambo.
 
Ndugu Slaa,

Kwanza niruhusu nitoe pongezi zangu za dhati kabisa kwako binafsi na kwa chama chako cha CHADEMA kwa mafanikio mliyoyapata kwa kipindi kifupi. Natambua kazi mnayoifanya ni nzito na ya hatari maana wengi wanatamani kuwa kama ninyi lakini wanaogopa kutangulia ila nyie mmesema mnatangulia wengine watawakuta mbele ya safari. Kwa hilo hongera sana.

Bila kupoteza muda kutaja mafanikio mliyoyapata naomba nijikite moja kwa moja kwenye kiini cha barua hii.

Kabla sijasahau naomba chama kisikate rufaa kwa kesi ya Lema.

Naomba nikukumbushe tu kwamba kwenye uchaguzi mkuu wa 2010 CCM hawakutaka si tu nyie mshinde bali msiongeze wabunge wa kuchaguliwa. Utakumbuka matamshi ya aliyekuwa Katibu mkuu wa CCM ndugu Makamba alipowaambia wanachama wa CCM kwenda kutafuta sababu yeyote ile wafungue kesi kupinga ushindi wa wabunge wa Chadema na chama kitagharamia kesi? Yanayotokea sasa ni utekelezaji tumjiandae kwa makubwa.

Utekelezaji wa hukumu ya Lema ni mwanzo tu ya mipango mingi ya CCM kuihujumu Chadema. Mpango ulikuwa trh 1-4 washinde Arumeru Mashariki halafu trh 5-4 ushindi wa Lema utenguliwe na sherehe kubwa yakupongezana ilikuwa ifanyike weekend hii mjini Arusha. Najua hilo limeshindikana.

Hukumu ya kupinga ushindi wa Lema si kwamba Jaji kajichanganya ni mtego wa makusudi ili nyie mjichanganye waendelee na plan B,C. Lengo lao ni kuikamata Arusha kwa hali yeyote kwa vile wanajua fika hawawezi kuikamata kwa kutumia sanduku la kura, kwa hiyo njia iliyobaki ni kutumia mahakama na pingamizi. Narudia tena msikate rufaa.

Lema amehukumiwa kwa kifungu 108 ‘Illegal Campaign' kinachomruhusu kugombea lakini kwenye majumuisho ya hukumu imeandikwa kahukumiwa kwa kifungu 114 "Illegal Practice" kinachomuzuia kugombea kwa miaka 5. Wanataka mkate rufaa au muombe ku review case na hapo itacheleweshwa mwisho mtaambiwa muda ni mfupi wa kuitisha uchaguzi.

CCM imeanza kuhaha baada ya kuona hamna mpango wa kukata rufaa, wanachosubiri ni Lema ateuliwe kugombea wamuwekee pingamizi, believe me or not lazima ataondolewa hata kama mtakuwa na hukumu mkononi.

Ndugu Slaa, CCM wameshafanya kosa wanajishauri endapo waingie kwenye uchaguzi ama la. Ushauri wangu ni kuwa, whatever the case, nendeni kwenye uchaguzi hata kama Lema hatogombea najua mtapata mgombea mwingine makini. Kama chama kitaona Lema asigombee, apewe kazi makao makuu ya kukiimarisha chama, akusaidie kuzunguka nchi nzima hasa katika kuimarisha matawi tayari kwa uchaguzi wa ndani na wa serikali za mitaa.

Nawatakia mafanikio mema katika ukombozi, najua kadritaabu zinavyozidi ndivyo ukombozi unavyokaribia.


Luteni.

Mimi kama Mzalendo wa Tz naunga hoja ya Luteni 100%. Na hapo pekundu ni muhimu sana pafanyiwe kazi na uongozi wa Chadema. Chadema wasihangaike na kwenda mahakamani, kwani kesi itapigwa danadana mpaka 2015 na mpaka hapo hasira za wana-Arusha zitakuwa zimetulia, hivyo hata CCM wanaweza kushinda Ubunge. Mimi nauomba uongozi wa CHADEMA waachane na habari za kukata rufaa na badala yake waendelee na ujenzi wa Chama. Na uchaguzi wa Arusha itatangaza zaidi Chadema ki yume na matarajio ya wana-ccm walivyotarajia.

CCM wanaweza kukata rufaa katk mamabo mawili;
1. Kama Lema akiruhusiwa kugombea, then CCM watamwekea pingamizi na utendaji wa Tume ya Uchaguzi na Mahakama zetu mnaujua. Nani kakuambia kwamba kuna haki kwa vyama vya upinzani TZ wakt ni mkakati maalumu kati ya Serikali-CCM-Usalama wa Taifa-Mahakama na Polisi ili kudhoofisha CHADEMA? Njia pekee ya CHADEMA kuweza kuwashinda wote hawa ni kwenye Sanduku la kura.

2. Kama Lema akikata rufaa yoyote ile; I can assure you kwamba hakuna Uchaguzi Arusha mpaka mwaka 2015 na hukumu haitabadilika kabisa na hivyo itaigharimu sana CHADEMA kuliko mnavyofikiria.

NB: Chadema mjue mimi siyo mwanachama wenu lkn napenda nione mnachukua nchi kwani chama changu hakika hakina mwelekeo mzuri, kwani imejaa kujuana na ufisadi kwa sana. Mimi nina mtu Usalama wa Taifa, hivyo ni bora mchukue ushauri wa Luteni kuliko mengine. Msione kuna watu wanakuja hapa na kuwashauri kwamba mkatafute haki mahakamani, mkae mkijua kwamba hawa ni watu wa system na wanatumiwa makusudi ili mpotee njia na CCM ibaki inachekelea.

Narudia tena, CHADEMA mkijichanganya tu na kutafuta haki Mahakamani, basi jimbo litakuwa wazi mpaka 2015, na hapo ndipo mtakapoona ugumu wa kulipata sasa. Arusha ni rahisi sana kwa CHADEMA kwasasa kuliko mwaka 2015 kama jimbo litakuwa wazi sasa.
 
Poleni sana, naona. Chadema mna mawazo. Mkate rufaa msikate yote tisa. Kumi ni kuwashawishi wananchi aw Arusha, mmechangia ni ni katika maendeleo ya Arusha tangu Lema achaguliwe Zanzibar ya fujo na mauajiq. Hata madiwani went hawafanyi kazi yeyote, mchaguliwe tena kwa shughuli gani fujo! Msifikri CCM inafanana makos a kila siku kisha ni nyi mfaidi,Kama mlivyofaidi Arumeru kutokana na makosa ya uteuzii. Ole wenu na kujeadili jiwe. People's itageuka ,kuwa popos.
 
Mkuu moma2k, unasema mimi nimetumwa umesahau na wewe umeishauri CDM kwenye post hii hapa chini kama mimi nilivyoishauri. Kwani wewe umetumwa na nani?

Tuacheni malumbano kuwa huyu katumwa au la, Kinachotakiwa ni kila mtu kuchangia tusilaumiane tena. Hapa tuko kwenye wakati mgumu sana. Ivyo kila mwenye lake achangie tujadiliane kwa amani tusiwe kama magamba wenye dola la kuonea raia wake wenyewe, wanachojali ni vyeo na kula yao. Chadema wana wanasheria waliobobea kuliko hao wa serikali ivyo kila kitu kitachotolewa kesho ujue wameona mbali. Ndio mana jana Mbowe hakuropoka kama magamba alisema tusubiri wakae na wanasheria wa chama na matokeo ni kesho ivyo tuvumilie tu bado masaa. Kwa mawazo yangu kukata rufaa ni muhimu kwani haki na demokrasia ndio liko kwake ivyo itakuwa si haki kukimbilia kugombea ubunge pasipo kuwaelimisha wananchi ni jinsi gani chama cha magamba wanavyotumia mahakama kufanya chochote kile wanachotaka. Mfano wanaua watu, makada wao, wanaonyesha silaha hadharani wala hawachukuliwi hatua, watoto wao wanatishia watu kwa bastola wala hawafunguliwi mashtaka.Hapa tunataka haki wana ARUSHA vumilieni kwa muda haki yenu mtaipata tu bora muwe na msimamo msirubuniwe kwa pesa,sabuni, nguo mkageuka. Tuikomboe tanganyika yetu
 
Ndugu Slaa,

Kwanza niruhusu nitoe pongezi zangu za dhati kabisa kwako binafsi na kwa chama chako cha CHADEMA kwa mafanikio mliyoyapata kwa kipindi kifupi. Natambua kazi mnayoifanya ni nzito na ya hatari maana wengi wanatamani kuwa kama ninyi lakini wanaogopa kutangulia ila nyie mmesema mnatangulia wengine watawakuta mbele ya safari. Kwa hilo hongera sana.

Bila kupoteza muda kutaja mafanikio mliyoyapata naomba nijikite moja kwa moja kwenye kiini cha barua hii.

Kabla sijasahau naomba chama kisikate rufaa kwa kesi ya Lema.

Naomba nikukumbushe tu kwamba kwenye uchaguzi mkuu wa 2010 CCM hawakutaka si tu nyie mshinde bali msiongeze wabunge wa kuchaguliwa. Utakumbuka matamshi ya aliyekuwa Katibu mkuu wa CCM ndugu Makamba alipowaambia wanachama wa CCM kwenda kutafuta sababu yeyote ile wafungue kesi kupinga ushindi wa wabunge wa Chadema na chama kitagharamia kesi? Yanayotokea sasa ni utekelezaji tumjiandae kwa makubwa.

Utekelezaji wa hukumu ya Lema ni mwanzo tu ya mipango mingi ya CCM kuihujumu Chadema. Mpango ulikuwa trh 1-4 washinde Arumeru Mashariki halafu trh 5-4 ushindi wa Lema utenguliwe na sherehe kubwa yakupongezana ilikuwa ifanyike weekend hii mjini Arusha. Najua hilo limeshindikana.

Hukumu ya kupinga ushindi wa Lema si kwamba Jaji kajichanganya ni mtego wa makusudi ili nyie mjichanganye waendelee na plan B,C. Lengo lao ni kuikamata Arusha kwa hali yeyote kwa vile wanajua fika hawawezi kuikamata kwa kutumia sanduku la kura, kwa hiyo njia iliyobaki ni kutumia mahakama na pingamizi. Narudia tena msikate rufaa.

Lema amehukumiwa kwa kifungu 108 ‘Illegal Campaign’ kinachomruhusu kugombea lakini kwenye majumuisho ya hukumu imeandikwa kahukumiwa kwa kifungu 114 “Illegal Practice” kinachomuzuia kugombea kwa miaka 5. Wanataka mkate rufaa au muombe ku review case na hapo itacheleweshwa mwisho mtaambiwa muda ni mfupi wa kuitisha uchaguzi.

CCM imeanza kuhaha baada ya kuona hamna mpango wa kukata rufaa, wanachosubiri ni Lema ateuliwe kugombea wamuwekee pingamizi, believe me or not lazima ataondolewa hata kama mtakuwa na hukumu mkononi.

Ndugu Slaa, CCM wameshafanya kosa wanajishauri endapo waingie kwenye uchaguzi ama la. Ushauri wangu ni kuwa, whatever the case, nendeni kwenye uchaguzi hata kama Lema hatogombea najua mtapata mgombea mwingine makini. Kama chama kitaona Lema asigombee, apewe kazi makao makuu ya kukiimarisha chama, akusaidie kuzunguka nchi nzima hasa katika kuimarisha matawi tayari kwa uchaguzi wa ndani na wa serikali za mitaa.

Nawatakia mafanikio mema katika ukombozi, najua kadritaabu zinavyozidi ndivyo ukombozi unavyokaribia.


Luteni.

Naomba niongeze tu katika barua yako yenye hekima kuwa plan nyingine ni kipindi hiki cha kupitisha bajeti basi jimbo liwe wazi. Tafadhali watahadharisheni madiwani wa CDM mjini Arusha wasisusie vikao waingie na wachakalike hata kama watapitisha kwa kura, bado CDM ina plan B kuibana serikali kama ilivyokuwa kule Mwembe Yanga. Tusipuuze mkakati katili huu (si wa CCM) bali wa milafi ya nchi hii ya TZ ambayo mingine imo ndani ya CCM na mingine imejichomeka katika vyama vya upinzani ikiwemo na CDM. Kuweni makini na matamshi na mienendo ya watu wote wakiwemo na wanachama wenu.
 
HAPA KINACHOTAKIWA NI KUKATA RUFAA! kwa utaratibu ufuatao:

1.Notice of appeal
2.Stay of decree of execution pending appeal(application hii iki succeed Lema ataendelea kuwa Mbunge na kupata haki zote za kibunge, mpaka appeal yake itakaposikilizwa na kuamriwa vinginevyo).
3.Filing of memorandum of appeal

OMBI: Shauri hili linatakiwa kuangaliwa kisheria zaidi kuliko kihisia. Lazima rufaa ikatwe kwani ni haki ya kikatiba.Mimi binafsi nauhakika rufaa ikikatwa Lema atashinda, kwasababu ile hukumu ina mashimo mengi sana.Ameandikwa kisiasa zaidi kuliko kisheria.
Nawaombeni sana rufaa ikatwe, ili tuone utawala wa sheria unaoongelewa siku zote una sura gani katika nchi yetu. Je ni porojo au kweli kuna utawala wa sheria?
Kisheria rufaa ikikatwa na kama itasikilizwa kwa haki kwa mujibu wa sheria za nchi hii, lema atashinda tuu!!!!
Tafadhari sana: Tusiukimbile uchaguzi ambapo kuna uwezekano wa kumweka mbunge wao kwa kutumia mtutu wa bunduki!
hapa lazima kufikiri sana!

That is an issue ..sidhani kama kuna mtu ana shaka zaidi ya hili
 
Hakuna kitu hapa. Huyo jamaa katumwa na CCM. Rufaa ni muhimu kuliko mbio za kutaka kushika jimbo. Je, wakitumia polisi kutangaza mshindi mgombea wa CCM mtasemaje? Ni muhimu chama kikakata rufaa ili haki itendeke.

Sijaisoma hukumu kamili, ispokuwa nimeongea na mawakili wa CDM, Kimomogoro, Marando, Lissu na Profesa Safari, wote wanaona kuwa kuna haja ya kukata rufaa. Nami nakubaliana nao na napingana na wote wanaosema CDM wasikate rufaa.

Uwezkeno wa rufaa kushinda unatokana na Jaji kushindwa kueleza kasoro za ushahidi. Kushindwa kwa Bartida kufika mahakamani; kushindwa kwa Lowassa kufika mahakamani kuliathiri vipi kesi ya msingi na ushahidi.
Hoja hapa siyo Lema kuwa mbunge, hoja hapa kwa nini Lema aenguliwe kwa mambo ya kijinga?

Pili, kwa hukumu ile Lema atalazimika kulipa gharama za kesi karibu Sh. 50 milioni. Sasa awalipe wahuini Sh. 50 milioni ili iweje?

Tatu, hata kama CDM hawataka rufaa, CCM watakata rufaa kwa kuwa hawataki kuendelea na uchaguzi mdogo. Watakatia yale mambo mengine mawili ambayo hayakuamuliwa.


CDM msikubali ushauri wowote wa kutokata rufaa. Kwanza, hiyo kesi itakwisha kabla ya mwaka huu kwa kuwa sheria inasema, "Rufaa ya kesi za uchaguzi zinatakiwa kumalizika ndani ya kipindi cha mwaka mmoja" tangu hukumu ilipotolewa.

Wewe ndio Jembe...
 
Hili swala ni nyeti sana kutokukata rufaa kutmuathili Lema na pia kutawapa mwanya ccm kuthibitisha kuwa hoja zilizotumika kufuta ubunge wa Lema ni za kweli, lakini pia hapa issue siyo jimbo wala Lema kuwa mbunge issue ni HAKI itendeke, lakini pia wananchi wana haki ya kuwa na mbunge ambaye ni chaguo lao kwanini walazimishiwe kubadili mbunge kwa nguvu na mashinikizo ya kisiasa.

Na hizo 50 million zilipwe bila sababu za msingi!!!
 
Ndugu Slaa,

Kwanza niruhusu nitoe pongezi zangu za dhati kabisa kwako binafsi na kwa chama chako cha CHADEMA kwa mafanikio mliyoyapata kwa kipindi kifupi. Natambua kazi mnayoifanya ni nzito na ya hatari maana wengi wanatamani kuwa kama ninyi lakini wanaogopa kutangulia ila nyie mmesema mnatangulia wengine watawakuta mbele ya safari. Kwa hilo hongera sana.

Bila kupoteza muda kutaja mafanikio mliyoyapata naomba nijikite moja kwa moja kwenye kiini cha barua hii.

Kabla sijasahau naomba chama kisikate rufaa kwa kesi ya Lema.

Naomba nikukumbushe tu kwamba kwenye uchaguzi mkuu wa 2010 CCM hawakutaka si tu nyie mshinde bali msiongeze wabunge wa kuchaguliwa. Utakumbuka matamshi ya aliyekuwa Katibu mkuu wa CCM ndugu Makamba alipowaambia wanachama wa CCM kwenda kutafuta sababu yeyote ile wafungue kesi kupinga ushindi wa wabunge wa Chadema na chama kitagharamia kesi? Yanayotokea sasa ni utekelezaji tumjiandae kwa makubwa.

Utekelezaji wa hukumu ya Lema ni mwanzo tu ya mipango mingi ya CCM kuihujumu Chadema. Mpango ulikuwa trh 1-4 washinde Arumeru Mashariki halafu trh 5-4 ushindi wa Lema utenguliwe na sherehe kubwa yakupongezana ilikuwa ifanyike weekend hii mjini Arusha. Najua hilo limeshindikana.

Hukumu ya kupinga ushindi wa Lema si kwamba Jaji kajichanganya ni mtego wa makusudi ili nyie mjichanganye waendelee na plan B,C. Lengo lao ni kuikamata Arusha kwa hali yeyote kwa vile wanajua fika hawawezi kuikamata kwa kutumia sanduku la kura, kwa hiyo njia iliyobaki ni kutumia mahakama na pingamizi. Narudia tena msikate rufaa.

Lema amehukumiwa kwa kifungu 108 ‘Illegal Campaign' kinachomruhusu kugombea lakini kwenye majumuisho ya hukumu imeandikwa kahukumiwa kwa kifungu 114 "Illegal Practice" kinachomuzuia kugombea kwa miaka 5. Wanataka mkate rufaa au muombe ku review case na hapo itacheleweshwa mwisho mtaambiwa muda ni mfupi wa kuitisha uchaguzi.

CCM imeanza kuhaha baada ya kuona hamna mpango wa kukata rufaa, wanachosubiri ni Lema ateuliwe kugombea wamuwekee pingamizi, believe me or not lazima ataondolewa hata kama mtakuwa na hukumu mkononi.

Ndugu Slaa, CCM wameshafanya kosa wanajishauri endapo waingie kwenye uchaguzi ama la. Ushauri wangu ni kuwa, whatever the case, nendeni kwenye uchaguzi hata kama Lema hatogombea najua mtapata mgombea mwingine makini. Kama chama kitaona Lema asigombee, apewe kazi makao makuu ya kukiimarisha chama, akusaidie kuzunguka nchi nzima hasa katika kuimarisha matawi tayari kwa uchaguzi wa ndani na wa serikali za mitaa.

Nawatakia mafanikio mema katika ukombozi, najua kadritaabu zinavyozidi ndivyo ukombozi unavyokaribia.


Luteni.


Nadhani mkuu hatujapishana kwenye thread ya LEMA AVULIWA UBUNGE page ya 47 niliandika hii comment


Wakuu tetesi ni kwamba hilo jimbo litakuwa open kwa mda usiojulikana,na wanataka wa make sure wamemuweka Lema nje ya siasi kwa mda mrefu zaidi hata akirudi tena asiwe na nguvu tena ya siasi kama sasa hivi,na wanajisifia wamefanya hivyo kwa makusudi kumpa chance ya yeye kugombea tena ila wakishaona chadema wamempa tena agombee kuna vipingamizi watatoa,so wakuu wa Chadema chezeni part yenu vizuri sana hawa CCM wanaleta ujinga hapa......



Again wakuu wa chadema kama ni possible msimamisheni mtu mwingine hapo Arusha na uchaguzi ufanyike tena.....achaneni na mambo ya rufaaa watawapotezea muda mwingine, hawa CCM now hamna haja ya kuweka majibishano nao nyinyi fanyeni vitendo tu basi, maana hapo sasa hivi wanawatafuta kwa kila namna so kaeni pembeni alafu waonekane wajinga na nyinyi muweke mtu mwingine hapo.....wanahaha sasa hivi hawana cha kufanya wamechanganyikiwa....
 
CDM mnahitaji kuwaachia wanasheria watoe ushauri juu ya jambo hili. Neno HAKI ni jambo la muhimu sana katika nchi hii.
Mbunge wa chama chochote cha siasa asipotendewa haki sisi tukaendelea tu na mambo mengine kwa kuwa tunajua tutashinda, itakuwa tumeikandamiza haki.
Rufaa ni ya muhimu mno na wanasheria wa CDM wakijipanga vizuri rufaa hii CDM watashinda.
Huwezi kumuacha Mbunge anyimwe kugombea kwa kosa la rushwa ambalo halikuwa mahakamani. Hata kama pingamizi litatolewa Lema akisimama kuna rufaa pia na iko wazi kuwa kesi hii imekaa vibaya.
Sijajua kwa nini wahakumkataa Jaji toka Sumbawanga tangu mwanzo.
 
Hii nchi wenye busara kama wewe wangekuwa kumi tu, tungekuwa tumepiga hatua ndefu katika maendeleo.

Cheers mkuu!
 
Hapa hakuna dawa nyingine, zaidi ya kukata rufaa. Lazima tuone HAKI inatendeka. Afadhari jimbo libaliki wazi kwa mwaka moja(wote tukose kuwa na Mbunge) kuliko kukimbilia uchaguzi huki tukikigawa chama. Kura 56,000 alizopata Lema ni nyingi sana. Hatua ya kwanza iwe ni kulinda HAKI ya wapiga kura hao wengi.

Tafadhari sana ndugu zanguni, hapa kitu cha kwanza kabisa ni kukata RUFAA.

Time Limitation ya rufaa: Rufaa ya uchaguzi inatakiwa isikilizwe ndani ya mwaka moja. Mwaka huo mmoja utaisha kabla ya 2015. Lazima tuwe principled ktk kulinda na kutetea HAKI, kuliko kukimbilia uchaguzi.
Note well: Tukumbuke kuwa hii HUKUMU isipotenguliwa na mahakama ya juu, basi itakuwa PRECEDENT ambayo itatumikaa kung'oa wabunge wengi wa upinzani hapo baadaye.
 
G natamani uchaguzi ungekuwa hata kesho.... Wataelewa maana ya nguvu ya uma ni nini.


Kuhusu swala la kuiba kura sahau manake za Batilda waliiba bado hazikutosha, safari hii hawataiba kura hata moja!

'Mwana-Arusha piga kura yako linda kura yako'na mara hii tutazilinda hata kwa vifaru ili kama ni vita na ianze ....hapa hatutaki rufaa wala cha dada yake na rufaa.
 
Siasa tamu kweli. Mimi ninachojua ni kwamba viongozi wakuu wa CDM pamoja na baadhi ya wafanyabiashara wakubwa wa Arusha hawamkubali Lema wakisema ana vurugu. Pia kuna kada ya kati ma wao hawamkubali Lema ila vijana wengi sana wanamuunga mkono Lema. Hivyo basi sioni CDM wakikata rufaa badala yake watatumia hii nafasi kumuengue Lema technically bila kusababisha mayowe toka kwa watu wengine. Ila pia Lema hatakubali kama kweli amepigwa marufuku kugombea kwa miaka mitano atataka atakaswe na mahakama. Kuna mchezo hapa ngoja tusubiri tuone.
 
Back
Top Bottom