Ndugu Slaa,
Kwanza niruhusu nitoe pongezi zangu za dhati kabisa kwako binafsi na kwa chama chako cha CHADEMA kwa mafanikio mliyoyapata kwa kipindi kifupi. Natambua kazi mnayoifanya ni nzito na ya hatari maana wengi wanatamani kuwa kama ninyi lakini wanaogopa kutangulia ila nyie mmesema mnatangulia wengine watawakuta mbele ya safari. Kwa hilo hongera sana.
Bila kupoteza muda kutaja mafanikio mliyoyapata naomba nijikite moja kwa moja kwenye kiini cha barua hii.
Kabla sijasahau naomba chama kisikate rufaa kwa kesi ya Lema.
Naomba nikukumbushe tu kwamba kwenye uchaguzi mkuu wa 2010 CCM hawakutaka si tu nyie mshinde bali msiongeze wabunge wa kuchaguliwa. Utakumbuka matamshi ya aliyekuwa Katibu mkuu wa CCM ndugu Makamba alipowaambia wanachama wa CCM kwenda kutafuta sababu yeyote ile wafungue kesi kupinga ushindi wa wabunge wa Chadema na chama kitagharamia kesi? Yanayotokea sasa ni utekelezaji tumjiandae kwa makubwa.
Utekelezaji wa hukumu ya Lema ni mwanzo tu ya mipango mingi ya CCM kuihujumu Chadema. Mpango ulikuwa trh 1-4 washinde Arumeru Mashariki halafu trh 5-4 ushindi wa Lema utenguliwe na sherehe kubwa yakupongezana ilikuwa ifanyike weekend hii mjini Arusha. Najua hilo limeshindikana.
Hukumu ya kupinga ushindi wa Lema si kwamba Jaji kajichanganya ni mtego wa makusudi ili nyie mjichanganye waendelee na plan B,C. Lengo lao ni kuikamata Arusha kwa hali yeyote kwa vile wanajua fika hawawezi kuikamata kwa kutumia sanduku la kura, kwa hiyo njia iliyobaki ni kutumia mahakama na pingamizi. Narudia tena msikate rufaa.
Lema amehukumiwa kwa kifungu 108 Illegal Campaign kinachomruhusu kugombea lakini kwenye majumuisho ya hukumu imeandikwa kahukumiwa kwa kifungu 114 Illegal Practice kinachomuzuia kugombea kwa miaka 5. Wanataka mkate rufaa au muombe ku review case na hapo itacheleweshwa mwisho mtaambiwa muda ni mfupi wa kuitisha uchaguzi.
CCM imeanza kuhaha baada ya kuona hamna mpango wa kukata rufaa, wanachosubiri ni Lema ateuliwe kugombea wamuwekee pingamizi, believe me or not lazima ataondolewa hata kama mtakuwa na hukumu mkononi.
Ndugu Slaa, CCM wameshafanya kosa wanajishauri endapo waingie kwenye uchaguzi ama la. Ushauri wangu ni kuwa, whatever the case, nendeni kwenye uchaguzi hata kama Lema hatogombea najua mtapata mgombea mwingine makini. Kama chama kitaona Lema asigombee, apewe kazi makao makuu ya kukiimarisha chama, akusaidie kuzunguka nchi nzima hasa katika kuimarisha matawi tayari kwa uchaguzi wa ndani na wa serikali za mitaa.
Nawatakia mafanikio mema katika ukombozi, najua kadritaabu zinavyozidi ndivyo ukombozi unavyokaribia.
Luteni.
Mkuu moma2k, unasema mimi nimetumwa umesahau na wewe umeishauri CDM kwenye post hii hapa chini kama mimi nilivyoishauri. Kwani wewe umetumwa na nani?Huyu Luteni katumwa na CCM. ushauri wake niwakuiangamiza CDM na kuinufaisha CCM.
HAPA KINACHOTAKIWA NI KUKATA RUFAA! kwa utaratibu ufuatao:
1.Notice of appeal
2.Stay of decree of execution pending appeal(application hii iki succeed Lema ataendelea kuwa Mbunge na kupata haki zote za kibunge, mpaka appeal yake itakaposikilizwa na kuamriwa vinginevyo).
3.Filing of memorandum of appeal
OMBI: Shauri hili linatakiwa kuangaliwa kisheria zaidi kuliko kihisia. Lazima rufaa ikatwe kwani ni haki ya kikatiba.Mimi binafsi nauhakika rufaa ikikatwa Lema atashinda, kwasababu ile hukumu ina mashimo mengi sana.Ameandikwa kisiasa zaidi kuliko kisheria.
Nawaombeni sana rufaa ikatwe, ili tuone utawala wa sheria unaoongelewa siku zote una sura gani katika nchi yetu. Je ni porojo au kweli kuna utawala wa sheria?
Kisheria rufaa ikikatwa na kama itasikilizwa kwa haki kwa mujibu wa sheria za nchi hii, lema atashinda tuu!!!!
Tafadhari sana: Tusiukimbile uchaguzi ambapo kuna uwezekano wa kumweka mbunge wao kwa kutumia mtutu wa bunduki!
hapa lazima kufikiri sana!
Hilo liko wazi, kwa arusha nakuhakikishia wala usiwe na wasi wasi... Labda huo uchaguzi uhairishwe!Ili serikali ijifunze CDM inatakiwa ishinde uchaguzi wa marudio kwa kishindo, itatoa funzo kuwa mbunge ni chaguo la wananchi si la mahakama.
Ndio kauli inayoongelewa na watu wa arusha kwa sasa. Na ni kweli wanamaanisha manake kiukweli CCM kwa arusha ni kama inajisumbua bure, haitakiwi hata kwa dawa! Tunasubiri kwa hamu huo uchaguzi, tutawatia aibu kuliko waliyoipata 2010.Nimeipenda hii kauli hapa kwenye haya maandishi mekundu hata CCM ingemsimamisha JK mwenyewe na Chadema wakasimamisha jiwe, jiwe litashinda!.
HAPA KINACHOTAKIWA NI KUKATA RUFAA! kwa utaratibu ufuatao:
1.Notice of appeal
2.Stay of decree of execution pending appeal(application hii iki succeed Lema ataendelea kuwa Mbunge na kupata haki zote za kibunge, mpaka appeal yake itakaposikilizwa na kuamriwa vinginevyo).
3.Filing of memorandum of appeal
OMBI: Shauri hili linatakiwa kuangaliwa kisheria zaidi kuliko kihisia. Lazima rufaa ikatwe kwani ni haki ya kikatiba.Mimi binafsi nauhakika rufaa ikikatwa Lema atashinda, kwasababu ile hukumu ina mashimo mengi sana.Ameandikwa kisiasa zaidi kuliko kisheria.
Nawaombeni sana rufaa ikatwe, ili tuone utawala wa sheria unaoongelewa siku zote una sura gani katika nchi yetu. Je ni porojo au kweli kuna utawala wa sheria?
Kisheria rufaa ikikatwa na kama itasikilizwa kwa haki kwa mujibu wa sheria za nchi hii, lema atashinda tuu!!!!
Tafadhari sana: Tusiukimbile uchaguzi ambapo kuna uwezekano wa kumweka mbunge wao kwa kutumia mtutu wa bunduki!
hapa lazima kufikiri sana!
G natamani uchaguzi ungekuwa hata kesho.... Wataelewa maana ya nguvu ya uma ni nini.1.Hakuna muda wa kuanza kuona kama kuna utawala wa shria ,It is obvious haupo.Mahakama ni hiyo hiyo ya CCM
2.Twende kwenye Uchaguzi,Kuiba hawataweza,Wakijaribu ndo kutachimbika vizuri.Ukombozi wa damu utaanzia huko
Naunga mkono hoja! Lakini kwa nini Lema ameandamwa sana tangu awe mbunge? Nakumbuka tangu awe mbunge amesakamwa sana why?