oba
JF-Expert Member
- Oct 31, 2010
- 310
- 65
Wana jamvii,
Nimetafakari sana mstakabali wa taifa letu katika mfumo huu wa vyama vingi nikaona kuwa mbele kuna giza totoro. Hivi ni nani anapanga vipaumbele vya taifa letu? tunaliendesha taifa letu kwa dira ya nani?mi ninaona kwa sasa chama kilichoko madarakani ndicho kinachopanga vipaumbele hivyo mfano, MKUKUTA, MKURABITA , MEM, MES n.k na mara nyingi vipaumbele hivyo vimekuwa ni matokeo ya vipaumbele vya UN, mfano millenium Dev goals na nyingine.
Kwangu hii naiona ni hatari sana kwasababu nchi yetu na raslimali zetu na hatima yetu inategemea UN na wanasiasa walioko madarakani ambao siku za hivi karibuni wameonekana kuwa wabinafsi na wa kujilimbikizia mali.
Kwa nini kwenye katiba mpya tusiwe na baraza la seneti? baraza hili liundwe na watu maalumu, professional and politicians pia.. mfano maraisi wastafu na majaji, ( kama tu wana sifa zinazotakiwa na wako tayari kupoteza uvyama wao baada ya kustafu), watu wenye sifa zilizotukuka katika jamii, watu wa type ye desmond Tutu,nk, bila kujali dini zao au kabila ila uwezo wao kama hazina ya taifa.
Wajumbe hao hawatakuwa wanavyama wa vyama vya siasa , watakuwa watanzania, wazalendo, watu wanaoangalia maslahi na mstakabali wa taifa letu.
Baraza hilo litakuwa na kazi ya kupanga vipaumbele vyetu kama taifa , mipango ya muda mrefu na mfupi, litajadili na kuweka malengo kwa ajili ya kulifikisha taifa katika ustawi halisi wa kijamii, kiuchumi na kisiasa.
Kazi ya vyama vya siasa itakuwa siyo kupanga sera bali kueleza namana gani wanasiasa wao watafanya ili kutufikisha kule ambako baraza letu la taifa, baraza la seneti limepanga kwenda.
Wanasiasa hawatakuwa na muda wa kutuchezea sarakasi (mfano, mara huyu aje na sera ya kuunganisha masomo ya fizikia na kemia kuwa somo moja kabla ya mwenzie kurudisha kuwa mawili tofauti) na kutuuingiza kwenye nikataba feki tena ya muda mrefu kama miaka 100
Wanasiasa watapimwa kila baada ya miaka mitano kwa swali hili; kwa miaka mitano tuliyokupa ni hatua gani tumepiga kuelekea kwenye malengo yetu kama yalivyopangwa na baraza letu la seneti? kama amefanya kwa kiwango cha kuridhisha atapata nafasi ya kuendelea, la hajaweza atapigwa chini.
Nchi hii inahitaji waonaji, wazalendo na watu wenye moyo wa taifa hii ndio wapewe nafasi ya kutupa dira ya tuendako na siyo wanasiasa ambao sera zao mara nyingi ni za kuwahadaa wananchi ili waendelee kutawala, no wonder wanaweza kutoa ahadi ( mfano barabara za angani au kusomesha watoto wetu bure nk) huku wakijua fika kuwa ahadi hizo hazitekelezeki, ilmradii tu wapewe dhamana ya kuongoza.
Nawasilisha
Nimetafakari sana mstakabali wa taifa letu katika mfumo huu wa vyama vingi nikaona kuwa mbele kuna giza totoro. Hivi ni nani anapanga vipaumbele vya taifa letu? tunaliendesha taifa letu kwa dira ya nani?mi ninaona kwa sasa chama kilichoko madarakani ndicho kinachopanga vipaumbele hivyo mfano, MKUKUTA, MKURABITA , MEM, MES n.k na mara nyingi vipaumbele hivyo vimekuwa ni matokeo ya vipaumbele vya UN, mfano millenium Dev goals na nyingine.
Kwangu hii naiona ni hatari sana kwasababu nchi yetu na raslimali zetu na hatima yetu inategemea UN na wanasiasa walioko madarakani ambao siku za hivi karibuni wameonekana kuwa wabinafsi na wa kujilimbikizia mali.
Kwa nini kwenye katiba mpya tusiwe na baraza la seneti? baraza hili liundwe na watu maalumu, professional and politicians pia.. mfano maraisi wastafu na majaji, ( kama tu wana sifa zinazotakiwa na wako tayari kupoteza uvyama wao baada ya kustafu), watu wenye sifa zilizotukuka katika jamii, watu wa type ye desmond Tutu,nk, bila kujali dini zao au kabila ila uwezo wao kama hazina ya taifa.
Wajumbe hao hawatakuwa wanavyama wa vyama vya siasa , watakuwa watanzania, wazalendo, watu wanaoangalia maslahi na mstakabali wa taifa letu.
Baraza hilo litakuwa na kazi ya kupanga vipaumbele vyetu kama taifa , mipango ya muda mrefu na mfupi, litajadili na kuweka malengo kwa ajili ya kulifikisha taifa katika ustawi halisi wa kijamii, kiuchumi na kisiasa.
Kazi ya vyama vya siasa itakuwa siyo kupanga sera bali kueleza namana gani wanasiasa wao watafanya ili kutufikisha kule ambako baraza letu la taifa, baraza la seneti limepanga kwenda.
Wanasiasa hawatakuwa na muda wa kutuchezea sarakasi (mfano, mara huyu aje na sera ya kuunganisha masomo ya fizikia na kemia kuwa somo moja kabla ya mwenzie kurudisha kuwa mawili tofauti) na kutuuingiza kwenye nikataba feki tena ya muda mrefu kama miaka 100
Wanasiasa watapimwa kila baada ya miaka mitano kwa swali hili; kwa miaka mitano tuliyokupa ni hatua gani tumepiga kuelekea kwenye malengo yetu kama yalivyopangwa na baraza letu la seneti? kama amefanya kwa kiwango cha kuridhisha atapata nafasi ya kuendelea, la hajaweza atapigwa chini.
Nchi hii inahitaji waonaji, wazalendo na watu wenye moyo wa taifa hii ndio wapewe nafasi ya kutupa dira ya tuendako na siyo wanasiasa ambao sera zao mara nyingi ni za kuwahadaa wananchi ili waendelee kutawala, no wonder wanaweza kutoa ahadi ( mfano barabara za angani au kusomesha watoto wetu bure nk) huku wakijua fika kuwa ahadi hizo hazitekelezeki, ilmradii tu wapewe dhamana ya kuongoza.
Nawasilisha