Baraza Jipya: Huu Uundwaji wa Baraza Dogo, Je Rais Magufuli Hajakiuka Sheria, Taratibu na Kanuni?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,494
113,590
Wanabodi,

Kwanza naomba nianze kwa pongezi za uteuzi wa baraza dogo, sina uhakika sana na umakini, lakini Katika kulitafakari baraza hili jipya la mawaziri, nimenote kuna sheria, taratibu na kanuni zinaweza kuwa zimekiukwa katika uteuzi huu!. JMT ni nchi ya Muungano kati ya Tanzania Bara na Tanzania Visiwani, au Tanzania Zanzibar, hivyo baraza la Mawaziri linapaswa kuwa na mawaziri kutoka Zanzibar wakiongozwa na Rais wa Zanzibar ambaye anapaswa kuwa waziri asiye na wizara maalum akiwakilisha maslahi ya Zanzibar ndani ya Baraza, sikusikia kama rais halali wa Zanzibar, akiteuliwa uwaziri!. Hivi katiba inasema juu ya hili?!.

La pili katika wizara zote za muungano, kwa mujibu wa sheria na kanuni, lazima ziongozwe na mawaziri kutoka pande zote za muungano!, yaani waziri akitoka upande mmoja, naibu waziri lazima atoke upande wa pili wa muungano, hili sikufanikiwa kuliona katika wizara zote za muungano, hili limekaaje?!.
Wiza hizo ni
WIZARA

Ofisi ya makamu wa Rais, muungano na mazingira: Waziri ni January Yusuf Makamba, naibu Luhaga Mpina-Hii ni wizara ya Muungano, waziri na naibu wake wote ni kutoka upande mmoja!.

Ujenzi, uchukuzi na mawasiliano: Waziri bado sijamtafuta, naendelea kumfikiria, Naibu waziri mhandisi Edwin Ngonyani. Ujenzi ni ya bara tuu, Uchukuzi na Mawasiliano zina mwelekeo wa ki muungano kupitia TCRA, TAA na POSTA hivyo hapa amnasubiriwa Mzenj?!.

Fedha na mipango: Waziri bado tunamtafuta, naibu waziri ni Ashantu Kizachi, kama huyu sii Mzanzibari, then Waziri anapaswa awe Mzanzibari.

Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa: Waziri ni Augustine Philip Mahiga ambae nimemteua kuwa mbunge na kisha waziri, Naibu ni Dr Suzan Kolimba.- Hii ni wizara ya muungano, waziri na naibu wote ni kutoka bara!.

Ulinzi na kujenga taifa: Waziri ni Dr. Hussein Ali Mwinyi-Hii ni wizaa ya muungano, kushikwa na Mzanzibari ni haki yake!.

Mambo ya ndani: Charles Muhangwa Kitwanga-Hii ni wizara ya muungano, iliyakiwa ikishikwa na Mbara, lazima iwe na naibu kutoka up

Elimu,Sayansi Teknolojia na Ufundi: Waziri bado hajapatikana, Naibu ni Stella Manyanya-Hapa pia Waziri anatakiwa kutoka Zanzibar kwa ajili ya Elimu ya Juu ambayo ni ya muungano!.

Japo Magufuli ana lengo zuri la kubana matumizi, jee ubanaji huo, ni lazima uzingatie sheria,taratibu na kanuni?!, au kwa vile lengo ni kubana tuu, tumwache abane namna yoyote ile atakayoona vile inafaa?!. Swali ni Baraza Jipya la Mawaziri: Huu Uundwaji wa Baraza Dogo, Jee Rais Magufuli Hajakiuka Sheria, Taratibu na Kanuni?!, au kwa vile jamaa ni mbabe fulani, hakuna yoyote wa kumwambia kitu?!, hata sisi jf pia tumuogope?!, au tumuheshimu ila ukweli tumuambie?!.

NB. Mtanote sijaitaja kifungu chochote cha sheria yoyote, taratibu yoyote au kanuni yoyote, kwa sababu sio kila sheria lazima iandikwe, zipo taratibu nyingine ni kama sheria, ukikiuka unakuwa kama umevunja sheria na sio mpaka ziandikwe!. Uingereza ina katiba yake lakini haijaandikwa popote!.

Tangu tumepata uhuru wetu, marais wa Tanzania wamekuwa wakipokezana kati ya Mkristu na Muislamu, Alianza Julius, akafuatia Ali, akafuatia Benyamini, akafuatia Mrisho na sasa ni Yohana!, haijaandikwa popote lakini huu ndio utaratibu wetu, tena akiwa Mkiristu, ni lazima awe kutoka...mkubali mkatae huo ndio uhalisia wa mambo bila kuandikwa popote, bali hupangwa iwe hivyo by a premeditated moves japo wengine huona kama just a coincidence!, hivyo sitarajii kama bado kuna watu wataniuliza sheria gani, taatibu gani na kanuni gani?!.

Pasco


 
Viwanda na biashara kuna waziri hakuna naibu
michezo sanaa kuna waziri na naibu...

Tanzania ya viwanda?
Yeah...Tanzania ya viwanda...

Kuwa na Tanzania ya viwanda haihitaji kuwa na Naibu Waziri Chifu....Katibu Mkuu atamaliza kila kitu...

Habari, Michezo, Utamaduni na Wasanii kuwa na Naibu Waziri ni sawa...Kwa haraka haraka inaonekana ni Wizara isiyo na umuhimu ila ni ya muhimu sana hii Wizara na ni kubwa...Inahusisha mambo mengi...Hivyo si vibaya akawepo Naibu Waziri.
 
Ulinzi kashika mzenji pekeyake, ni sawa, na nyingine wakishika watanganyika peke yao siyo sawa:angry:
sisi sote ni watanzania, tukitoka ubara na uzenji, tutakuja kaskazini hawajapata waziri siyo sawa, kanda ya ziwa wametoka mawaziri 10 siyo sawa (kila mkoa utoe waziri, ndo alichokuwa anafanya mtangulizi); halafu tutasema wanaume ni wengi kuliko wanawake siyo sawa (tunataka 50 - 50).
with due respect, tusubiri tuone utendaji wa hili jeshi jipya, mengine tunajipa ugumu tu, SHERIA ILIYO KUU/KUBWA KULIKO YOTE NI UPENDO
 
Leo nimeshangazwa sana na hatua ya rais John Magufuli kuunganisha wizara za uchukuzi na ujenzi kuwa wizara moja! Big No!

Nimeshangazwa sana na namna wizara ya elimu ilivyoundwa! Hapa sijui Magufuli amewaza nini!

Nashindwa kuelewa kauli ya Magufuli ya "sijampata mtu sahihi bado" huku akiweza kumpata naibu waziri!

Kwanini walemavu wawekwe wizara inayohusu sera za CCM wakati kuna wizara ya jamii?

Uteuzi wa baadhi ya mawaziri kwa kweli sijakubaliana nao hasa January Makamba mtu aliyezoea kuishi kijanjajanja, Sospeter Muhongo ambaye ana tuhuma za kufanya udalali ndani ya ofisi ya umma na kurudishwa kwenye ofisi ileile! Harison Mwakyembe mtu mwenye tuhuma pale bandarini!

Nimeweka alama za kuuliza sana kwenye teuzi za Magufuli kuwa zimezingatia vigezo gani? Yapo mapungufu mengi sana ya kiufundi na nina uhakika kuwa baraza hili halitadumu hata miezi sita!
 
siwakubali akina mwigulu na nape kuwa mawaziri, hawana uhalisia ama udhati kwenye hulka zao
 
Pasco be serious bro. Haya in mazoea. Hakuna sheria au kanuni inayosema wanaoteuliwa watoke wapi. Hiyo ilikuwa ni tabla ya JK kuwatengenezea ulaji wapambe wake. Hata tungekuwa na mawaziri wote from Bara au zenji....I care less. As long as they can deliver.

In any case, not everybody can be satisfied with what Magufuli is doing. So let the guy do his work.
 
Ulinzi kashika mzenji pekeyake, ni sawa, na nyingine wakishika watanganyika peke yao siyo sawa:angry:
sisi sote ni watanzania, tukitoka ubara na uzenji, tutakuja kaskazini hawajapata waziri siyo sawa, kanda ya ziwa wametoka mawaziri 10 siyo sawa (kila mkoa utoe waziri, ndo alichokuwa anafanya mtangulizi); halafu tutasema wanaume ni wengi kuliko wanawake siyo sawa (tunataka 50 - 50).
with due respect, tusubiri tuone utendaji wa hili jeshi jipya, mengine tunajipa ugumu tu, SHERIA ILIYO KUU/KUBWA KULIKO YOTE NI UPENDO

Kaskazini sidhani kama wamepata Mawaziri, Arusha, Kilimanjaro na Manyara nadhani Rais katekeleza agizo la Rizmoko
 
Midomo mali yenu. Fanya kazi yako mh.rais.sisi tunataka maendeleo ya kweli tu. Kwa watanzanis wote.!!
 
Umesahau na Tanzania Meteoroligical Agency(TMA).Hii ni Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini ikiwa ni moja ya Taasisi ya kimuungano.
 
Magu why whyyyyy Magu nape why mwigulu whyyyyy muhongo whyyyyy??? Please I demand to know right now whyyyyy??

Hv decided to go far far north to the pole or further south to Antarctic to spend the rest of my life alon instead of mingling with ccm people.

Okay you kengez bring those malimaoz and ndimuz I eat damn you.

Kamon!!
 
acha kukalili.....shein kuwa rais wa zenj automaticanaingia kwenye baraza la mawaziri.....siyo mpaka atangazwe.....hala hamnakitu kama hixho ki sheria....eti waziri mbara naibu mzenj.....wewe umekariri wewe.......hebu mwachen Prof apige kazi......"hapa ni Kaaaaaaazi Tu!!"
 
Yani ccm watu waajab sana. Muhongo kateuliwa maususi tu kumdhibit mengi baas. Mwigulu na nape nikutukomoa na kututambia Ukawa. Basi mpe Ritz wizara ya fedha mzidi kitukomoa nafsi zenu zifurahi
 
Kwani wote si Watanzania? Shida ya nini? By the Way Wazanzibari wanayo Serikali yao
 
Back
Top Bottom