Barara ya Mbezi - Msumi kila mwaka kujengwa Km 1 - Meneja TANROAD

Muite

JF-Expert Member
Sep 10, 2013
2,342
4,801
Nimeangalia maelezo ya Meneja wa TANROAD mkoa -DSM ndugu Haruon Senkuku alipohojiwa na muandishi wa habari kuhusu malalamiko ya wakazi wa maeneo ya Mbezi-Msumi wanaolalamia TANROAD kutokuijenga barabara na wakihoji kuhusu mkandarasi anayejenga kakipande kasikofika hata km 1 ambapo anaifanya kazi hiyo karibia mwaka wa pili sasa ikiwa ni pamoja na kujenga kwa kiwango duni cha lami na wembamba wa barabara.

Kilichonishangaza ni pale huyo Meneja wa TANROAD kwenye kujibu hoja amesema hiyo barabara itakuwa inajengwa kwa km 1 kila mwaka. Nikajiuliza hivi kumbe kujenga barabara ya ukubwa wa km 1 inachukuwa miezi 12+, au labda anamaana itakuwa inatengewa fedha za kujenga urefu huo. Kwa maana hiyo basi kukamilika kwa barabara kutoka mbezi kwenda Msumi wakazi wa maeneo hayo wategemee miaka 8 kwa maana ya km 1 kwa mwaka x km 8(Msumi-mbezi).

Kuna haja mambo mengine Mama yetu mhe Rais ni vema akayajua maana hawa watendaji katika taasisi na wizara SIO KABISA
 
Nimeangalia maelezo ya Meneja wa TANROAD mkoa -DSM ndugu Haruon Senkuku alipohojiwa na muandishi wa habari kuhusu malalamiko ya wakazi wa maeneo hayo wanayolalamia TANROAD kutokuijenga barabara na wakihoji kuhusu mkandarasi anayejenga kakipande kasikofika hata km 1 lakini ambapo anaifanya kazi hiyo karibia mwaka wa pili sasa ikiwa ni pamoja na kujenga kwa kiwango duni cha lami na wembamba wa barabara.

Kilichonishangaza ni pale huyo Meneja wa TANROAD kwenye kujibu hoja amesema hiyo barabara itakuwa inajengwa kwa km 1 kila mwaka. Nikajiuliza hivi kumbe kujenga barabara ya ukubwa wa km 1 inachukuwa miezi 12+, au labda anamaana itakuwa inatengewa fedha za kujenga useful huo. Kwa maana hiyo basi kukamilika kwa barabara kutoka mbezi kwenda Msumi wakazi wa maeneo hayo wategemee miaka 8 kwa maana ya km 1 kwa mwaka x km 8(Msumi-mbezi).

Kuna haja mambo mengine Mama yetu mhe Rais ni vema akayajua maana hawa watendaji katika taasisi na wizara SIO KABISA
Shushia na hii mkuu...
 

Attachments

  • IMG_7387.jpg
    IMG_7387.jpg
    54.2 KB · Views: 24
Nimeangalia maelezo ya Meneja wa TANROAD mkoa -DSM ndugu Haruon Senkuku alipohojiwa na muandishi wa habari kuhusu malalamiko ya wakazi wa maeneo hayo wanayolalamia TANROAD kutokuijenga barabara na wakihoji kuhusu mkandarasi anayejenga kakipande kasikofika hata km 1 lakini ambapo anaifanya kazi hiyo karibia mwaka wa pili sasa ikiwa ni pamoja na kujenga kwa kiwango duni cha lami na wembamba wa barabara.

Kilichonishangaza ni pale huyo Meneja wa TANROAD kwenye kujibu hoja amesema hiyo barabara itakuwa inajengwa kwa km 1 kila mwaka. Nikajiuliza hivi kumbe kujenga barabara ya ukubwa wa km 1 inachukuwa miezi 12+, au labda anamaana itakuwa inatengewa fedha za kujenga useful huo. Kwa maana hiyo basi kukamilika kwa barabara kutoka mbezi kwenda Msumi wakazi wa maeneo hayo wategemee miaka 8 kwa maana ya km 1 kwa mwaka x km 8(Msumi-mbezi).

Kuna haja mambo mengine Mama yetu mhe Rais ni vema akayajua maana hawa watendaji katika taasisi na wizara SIO KABISA
Mkuu usiishie kulalamika.
Lipa kodi yako kikamilifu.
Hela ya kutosha itapatikana kujenga hiyo barabara.
 
Bara bara muhimu zinazohitaji lami kwa jiji la Dar hazizidi hata km 100! Namshauri Samia kufumba macho na kukopa Tsh Bilioni 160 ili tumalizane na maneno ya hizi bara bara za Dar kisha tutumie hiyo miaka kumi kulipa deni. Benki za ndani zina uwezo wa kufanya loan syndication na kuikopesha serikali hiyo pesa chap-kwa haraka!
Kinachotakiwa ni Tanroads kugawa tenda kwenye lots zisizozidi km 10 ili wakandarasi wamalize hizi bara bara ndani ya miezi 14!
 
Duh! Waliobahatika barabara zao kujengwa kipindi cha JPM washukuru Mungu. Nchi huwa hazipati viongozi kama wale mara kwa mara.
 
Shida ni watu kujenga unplanned areas, hata serikali inaona hakuna umuhimu wa kupeleka barabara.

Kingine ukiona mkandarasi anatumia muda mrefu sababu ni pesa
 
Sasa we jamaa unamkosoa mwenzio huku nawewe kilaza tu.
BARARA Ndio nini?
Toa boriti kwanza kwenye jicho lako
Hiyo typing error ina shida gani, je imesababisha watu wasielewe maudhui!? Nina wasiwasi wewe ndio wale wabunge wanaoomba taarifa kwa spika kwaajili ya kurekebisha neno kwa mbunge mwenzake hata kama halina madhara kwenye maudhui ya hoja, yaani YEYE HOJA KWAKE SIO ISSUE.

Taarifa Mheshimiwa Spika, Taarifa Mheshimiwa Spika, Taarifa Mheshimiwa Spika.

Taarifa Mheshimiwa...

Mhe...... katika hoja yake kuhusu kero ya kukosekana hospitali wilayani kwake naona huyu mhe anatoa kijiti kwa mwenzake badala ya boriti jichoni kwake, amesema Darisalama badala ya Dar es salaam
 
Mama anadili na mambo makubwa hizo inshu ndogo za mabarabara ya mitaa kuna wasaidizi wengi Sana DC, ded, madiwani wa kata husika na meneja tarura wataweka mambo Sawa, halafu pia kwenye fungu la fedha za barabara za mitaa huenda Baraza la madiwani ktk halmashauri husika waligawana Kwa uwiano huo so rais si busara kutengua maamuz ya madiwani.
 
Nimeangalia maelezo ya Meneja wa TANROAD mkoa -DSM ndugu Haruon Senkuku alipohojiwa na muandishi wa habari kuhusu malalamiko ya wakazi wa maeneo ya Mbezi-Msumi wanaolalamia TANROAD kutokuijenga barabara na wakihoji kuhusu mkandarasi anayejenga kakipande kasikofika hata km 1 ambapo anaifanya kazi hiyo karibia mwaka wa pili sasa ikiwa ni pamoja na kujenga kwa kiwango duni cha lami na wembamba wa barabara.

Kilichonishangaza ni pale huyo Meneja wa TANROAD kwenye kujibu hoja amesema hiyo barabara itakuwa inajengwa kwa km 1 kila mwaka. Nikajiuliza hivi kumbe kujenga barabara ya ukubwa wa km 1 inachukuwa miezi 12+, au labda anamaana itakuwa inatengewa fedha za kujenga urefu huo. Kwa maana hiyo basi kukamilika kwa barabara kutoka mbezi kwenda Msumi wakazi wa maeneo hayo wategemee miaka 8 kwa maana ya km 1 kwa mwaka x km 8(Msumi-mbezi).

Kuna haja mambo mengine Mama yetu mhe Rais ni vema akayajua maana hawa watendaji katika taasisi na wizara SIO KABISA
Afadhali hao wanajengewa kilometa Moja kwa mwaka. Sisi kwetu huku wanajenga mita 400 kwa mwaka kwa barabara ya kilometa 1.7 tena kwa kutumia lami nyepesi! Ahahahahaha!!!
 
Back
Top Bottom