britanicca
JF-Expert Member
- May 20, 2015
- 15,634
- 30,000
Obama alisema hayo mapema jana Jumapili wakati akiendelea kuwashawishi wamarekani wamchague Bi Clinton awe rais.
Obama alisema kuwa kwa miaka na miaka hawajawahi kuwa na rais mwanamke na hii inatokana na tatizo la kihistoria na la muda mrefu katika jamii ya taifa hilo kuhusu mtazamo kwa wanawake wenye nguvu. Obama alionya kuwa tatizo hilo bado lipo na litaathiri kampeni za Clinton mwaka huu.
Obama anaendelea kuimarisha kampeni za Clinton katika wapiga kura na maeneo ambayo yanaonekana kusita kumuunga mkono Clinton.
Juzi aliwataka watu weusi wajitokeze kwa wingi kumpigia kura Clinton kama kweli wanataka kumuaga vizuri wakati atakapoachia madaraka ya urais na aliwaambia itakuwa ni udhalilishaji katika misingi aliyoiweka yeye ikiwa watu weusi hawatamuunga mkono Bi Clinton.
Michelle Obama nae anatumia ushawishi wake mkubwa na kupendwa kwake na Wamarekani kuendelea kumpigia kampeni Hillary Clinton na anaendelea kuwahamasisha watu weusi wajiandikishe kwa wingi zaidi.
Obama alisema kuwa kwa miaka na miaka hawajawahi kuwa na rais mwanamke na hii inatokana na tatizo la kihistoria na la muda mrefu katika jamii ya taifa hilo kuhusu mtazamo kwa wanawake wenye nguvu. Obama alionya kuwa tatizo hilo bado lipo na litaathiri kampeni za Clinton mwaka huu.
Obama anaendelea kuimarisha kampeni za Clinton katika wapiga kura na maeneo ambayo yanaonekana kusita kumuunga mkono Clinton.
Juzi aliwataka watu weusi wajitokeze kwa wingi kumpigia kura Clinton kama kweli wanataka kumuaga vizuri wakati atakapoachia madaraka ya urais na aliwaambia itakuwa ni udhalilishaji katika misingi aliyoiweka yeye ikiwa watu weusi hawatamuunga mkono Bi Clinton.
Michelle Obama nae anatumia ushawishi wake mkubwa na kupendwa kwake na Wamarekani kuendelea kumpigia kampeni Hillary Clinton na anaendelea kuwahamasisha watu weusi wajiandikishe kwa wingi zaidi.