kiukweli huko kishumundu sidhani kama kunatatizo ila mentality tu kuwa wahuko ni washamba.kuhusu komu yy anatokea uru mawella(kitandu)kwa wanaojua geo. ya uru ukifika rau madukan kuna njia panda moja inaenda shimbwe+kishmundu nyingine inaenda uru sokon+mawella huko ndo mb mtarajiwa mr komu anakotoka.
Ni ahadi ya Kikwete! Ahadi nyingine inabidi watu watumie akili zao pia kabla hawajaziamini. Au JK kaona hao jamaa ndio rahisi kuwadanganya. Wachaga wenyewe wanabeza huko Kishumundu, JK anasema atapeleka barabara ya lami!
Mwenzio mmoja humu ndani kasema kumbe Kishumundu kuna barabara ya lami tangu enzi za Mwalimu Nyerere. Pengine basi JK alipaswa kuwaahidi jambo tofauti wakati huu, lakini nashangaa ahadi ndiyo hiyo na wameshangilia sana, na kura watampa. Anthony Komu aligombea ubunge huko Moshi uchaguzi uliopita, namfahamu tulikuwa naye Mlimani late 1980's, yeye alikuwa akituambia ni mtu wa Uru lakini siku zote alisisitiza kuwa si mkishumundu, sijui kuna shida gani huko? Labda nikuulize ndugu Mtu B, unaziamini ahadi za JK kuwa ataunganisha shule zote na internet? Shule hazina umeme wala computer, hiyo internet itafungwa wapi? Na ni kwa gharama za nani, maana hata hizi shule za kata tunazoambiwa ada ni sh 20,000 kwa mwaka kuna michango lukuki hadi ya kumlipa mgambo anayelinda kifusi cha kokoto kilichomwagwa uwanja wa shule!
I am grateful kuishi to see this day, ahadi ya Kikwete ya lami hadi nyumbani Kishumundu imekamilika kwa 50% lami ya Uru West tayari imetandikwa, na misingi ya maji taka mizuuuuuuuuri kabisa, rehabilitation ya lami ya Uru East on way. SITAMBEZA RAIS WANGU KAMWE.
Let time tell the tale.
Naomba nikusaidie ndugu yangu. Tatizo la Uru Kishumundu limeletwa na wachaga wenyewe, yaani wachaga ni watu wabaguzi sana, na ubaguzi wao wanauanzia kwao kwa kubaguana wao kwa wao. Wachaga wanadharauliana wao kwa wao, lakini cha ajabu wote wanadharau wa Kishumundu. Na huo ubunge wa Moshi vijijini nakuhakikishia Komu hatashinda kamwe, na kosa lake ni moja tu, kunasibishwa na Uru (haidhuru ni Kishumundu au la!). Wakibosho na wengine huko KAMWE hawatachagua mtu wa Uru, hilo wanalisema wazi. Muda wa Anthony Komu na wauru wenzie kupata ubunge ni pale litakapoanzishwa jimbo la Uru, kama inawezekana. Sijawahi kuona ubaguzi mbaya kama huu!
Sitashangaa kusikia kuwa ni hao wachaga wengine wamemwambia JK kuwa wakishumundu kwanza washamba wale, atoe ahadi hewa za barabara ya lami na internet, tayari keshashinda!
Nijuavyo kutoka kijiji cha mbali kabisa cha Uru Kishumundu hadi mjini Moshi kati ni maili kumi
-wajasiria mali wadogo 45% wanatoka Kishumundu unaowaona Moshi mjini
-Kishumundu kwa mwendo wa Mguu ni saa moja na nusu tu jambo hlli haliwezekani sehemu nyingine ya moshi
-kila mtu wa Uru anaweza kwenda kutafuta huduma mjini saa yoyote na siku yoyote sehemu nyingine mtu aweza zaliwa hadi umri utu uzima bila kufika mjini
Kishumundi ni sehemu pekee wanakoishi koo zote za Wachaga kama,MUSHI,MASAWE,NGOWI,MOSHA,CHUWA,AKARO,MATERU,KESI,MTALO,OFOO,MMBANDO,ORIO,KISAMO,OWENYA,MREMA,MARIALE Na kadhalika
Uru ina wasomi wengi mno
-uru ina watumishi wengi wa ngazi ya kati serikalini
-uru ina wafanya biashara wengi mno wa ngazi ya kati
-kwa taarifa maji yote,mbogamboga ,ndizi,asilimia kubwa zinatoka Uru
-Wanawake wazuri,wapole,wachapa kazi,waumini,wasio na tamaa hata nanihiii alitoka Uru
pima mwenyewe huo ushamba uko wapi,mwacheni docta waukweliatekeleze ahadi.
Yalitimia! Na tusipokuwa macho yatadumu