Kasekenya: Barabara Mianzini hadi Ngaramtoni Juu inafunguliwa upya kwani kuna maeneo ya km 8 hayakuwa na barabara kabisa

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,987
Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mheshimiwa Mhandisi Geoffrey Kasekenya amesema barabara Mianzini hadi Ngaramtoni Juu inafunguliwa upya kwani kuna maeneo ya km 8 hayakuwa na barabara kabisa lengo ni kuhakikisha Wananchi wa maeneo hayo ambao ni wafanyakazi wakubwa wa shughuli za kilimo, wanapata unafuu wa kuyafikia masoko Arusha Mjini kwa Urahisi, kwa haraka na kwa bei rahisi na itatumika pia kama Njia ya Mchepuo [Arusha By Pass] kwa ajili ya kupunguza msongamano kwenye barabara kubwa inayotoka Moshi - Arusha kwenda Namanga.

"Ukiacha hii barabara tulioweka jiwe la Msingi, tutajenga barabara nyingine ya njia nne kutoka Kisongo hadi Soko la Kilombero, tutajenga Km 10 tena njia nne hadi Usa River, Junction kwenda Arusha National Park, Serikali Itajenga KM 10 barabarani ya Kikavu mji wa Moshi na tunaendelea kufanya usanifu kuanzia Tengetu, Mbuguni hadi Merirani barabara hiyo ijengwe kwa kiwango cha lami, tunakamilisha Usanifu wa barabara ya kuanzia Longido kwenda Sia ili watu wanatoka Kilimanjaro kwenda Nairobi sio lazima wapite Arusha mjini" ameongeza Naibu Waziri Kasekenya.

1684515908753.jpg
1684515908691.jpg
1684515909005.jpg
 
Wahusika Tarura na Tanroads tunaomba ujenzi wa barabara uendane na quality msisimamie kwenye bei rahisi tuu. Kuna barabara inatoka Bunju mianzini kwenda Furaha hospital inajengwa chini ya kiwango.

Mkandarasi akiulizwa na wananchi anasema hiyo inatokana na thamani ya hela aliyolipwa ile rami haitakaa miaka 5, inafanana na ile ya baracuda segerea kila siku viraka.

Barabara ingine ni ya kutoka mbweni ubungo mpaka njia panda ya shamsiye school haina viwango kabisa.

Huyu anayenga mwendokasi kutoka magomeni mpaka mbagala kazi yake haina viwango kabisa si bora mkampatia strabag, Delmonte, Mac hawa wamejenga mwenge moroco chini ya consultant wa JiCa. Hii mwendokasi ya mbagala haitakuwa na maana sana kama itajengwa kijinga kijinga angalia daraja la changombe veta lilivyopinda. Pesa si ya mkopo nyinyi waswahili inawauma nini mnaibana ujenzi unakuwa chini ya kiwango. Mh chalamila tunaomba usimamie haya mkoani kwako.

Njia ya kawe tunahitaji ibomolewe ili hifadhi ya barabara ionekane maana ni hatari sana kwa watumiaji. Ikiwezekana kawe litengwe eneo maalum packers ijengwe stend ya kisasa kama mawasiliano
 
Back
Top Bottom