Bara la Afrika kuja na Sarafu yake itakayoitwa Afro au Afric (Afro currency au Afric currency)

Arnold Kalikawe

Senior Member
Sep 28, 2016
146
340
Hivi karibuni kumekuwa na uhaba wa sarafu ya Dollar Duniani, kitu ambacho kimepeleka pia sarafu za nchi nyingi barani Afrika kuyumba, na vitu kupanda bei bila mpangilio.

Kwa sababu mimi pia ni Admin wa page moja ya facebook inayoitwa Icon Africa ambapo humo tupo ma-Admin wengi kutoka nchi za Afrika na kila mmoja anapost mambo ya nchi yake ususani utalii. Basi nikaamua kwenda kwenye page kuuliza ni namna gani tuwaweza kuwa na pesa yetu ya bara la Afrika ili kuepuka madhara ya Dollar.

Na kama mnavyojua nchi zetu nyingi za kiafrika bado zinatumia sarafu ya Dollar kufanya manunuzi sehemu mbali ndani na nje ya bara la Afrika. Hivyo ukosefu wa sarafu ya Dollar imepelekea pia nchi nyingi kutikisika kiuchumi. lakini endapo tungekuwa na sarafu yetu ya bara la Afrika kama jinsi ilivyo sarafu ya Ulaya (Euro €), basi tutakuwa imara kiuchumi, hata kama dollar ikitikisika, sisi bado tutakuwa salama. Na pia tutaweza kufanya manunuzi ndani ya bara letu bila kutatizwa na kupanda na kushuka kwa sarafu ya Dollar.

Nimeanza kuona muitikio mkubwa wa watu mbalimbali kwenye comment za hiyo post wakipendekeza Sarafu iitwe Afro au Afric. Na muitikio ni mkubwa na kila mwafrika anatamani tuwe na sarafu yetu. Haya maoni ni namna gani yanawezwa kufikishwa Africa Union na yakafanyiwa kazi kwa haraka. Maana sidhani kama kuna nchi ya kiafrika inataka kuendelea kuikumbatia dollar
 
Au zikiwa nyingi jua hapo hamna kitu.
Ndio tunatakiwa tuchague au kupendekeza jina moja.... Mfano Euro, inatumiwa Ulaya, kila nchi inatumia Euro barani ulaya...

Afrika napo tunataka Sarafu yetu ili kuepuka misukosuko ya Dollar kupanda na kushuka... Wewe unapendekeza jina gani, na namna ipi tufanye hii sarafu kuwa Hai
 
Wazo zuri lakini hii itakuwa pigo kubwa sana kwa wamagharibi na mshirika wao U.S , Swali ni je watakubali lifanikiwe tena kwenye bara lenye viongozi wengi mamluki wao na wanalolimudu?
Hapo ndipo tunapotakiwa kusimama kama waafrika. Afrika ina nguvu sana tukishikamana, Niger, Mali na Burkina Faso wameonesha njia... Hatuwezi kuishi kwa kufikiria mmarekani hatatuonaje tukijitoa kwenye matumizi ya Dollar... Ifike mahali tufanye maamuzi bila kutizama wazungu watatuonaje
 
Rais Muammar Gaddafi alijaribu kulipigia debe hilo akaishia kuuawa na wamarekani, hilo litawezekana kama tu viongozi wote wa africa watakubaliana na kuweka msimamo na siyo kuwaachia viongozi wachache, na ni lazima kuwe na upinzani mkubwa sana toka nchi za magharibi maana hawako tayari kuona hili bara likiungana because unity means strength
 
Hapo ndipo tunapotakiwa kusimama kama waafrika. Afrika ina nguvu sana tukishikamana, Niger, Mali na Burkina Faso wameonesha njia... Hatuwezi kuishi kwa kufikiria mmarekani hatatuonaje tukijitoa kwenye matumizi ya Dollar... Ifike mahali tufanye maamuzi bila kutizama wazungu watatuonaje
Kujaribu ni kuonesha nia nasimama na wewe, wasiwasi wangu tu ni u afiki wa viongozi wa Afrika. Ghadafi alijaribu kuanzisha bank na akawa tayari hadi kutoa capital ili afrika ijinasue na utegemezi wa mikopo gandamizi ya wamagharibi na maswahiba zao sote tunakumbuka mwisho wake ulikuwaje na alikufa kwenye shimo kama panya huku viongozi wa Afrika wakimuangalia tu.
 
Rais Muammar Gaddafi alijaribu kulipigia debe hilo akaishia kuuawa na wamarekani, hilo litawezekana kama tu viongozi wote wa africa watakubaliana na kuweka msimamo na siyo kuwaachia viongozi wachache, na ni lazima kuwe na upinzani mkubwa sana toka nchi za magharibi maana hawako tayari kuona hili bara likiungana because unity means strength
Mabadiliko uanza na mimi... Kama kila mwafrika mmoja akiweka nia ya kuwa na sarafu mmoja, hili jambo linawezekana... Muammar Gaddafi aliibuka wakati mbaya, Siasa za kibeberu usijitoe wewe kama wewe kupingana nao, wewe sema wananchi ndio wamesema... Huoni Burkina Faso na Mali walivyomuweza Mfaransa, sio mtu mmoja ambaye alitoka kupigania nchi, bali raia wote... Lakini kule Libya kilichomua Gaddafi ni baadhi ya wananchi wake kuanza kumuita Dictator, wananchi wengine hawakumuunga mkono, na Marekani akishaona tu wengine hawakuungi mkono, ndio anawatimua hao hao kukuangamiza... Sasa sisi kama Afrika na mwafrika mmoja mmoja sote kwa pamoja tukisimama hawawezi kufanya kitu... Niger, Mali na Burkina Faso wananchi wote hawakutengana, waliungana na kua taifa kama taifa
 
Labda kama Magu angekuwa hai, laasivyo ni ndoto za mchana tu
Yes... Lakini bado haimaanishi fulani hasipokuwepo ndio pia sisi tulale na tusifanye mabadiliko... Kumbuka Dollar ikitikisa Dunia sio Magu tena anayeteseka, bali ni wewe uliye hai
 
Mkishaanzisha hiyo sarafu bado mnatakiwa kulipa madeni yenu ambayo ni trilioni za dola kwa US$ na wala sio kwa hiyo sarafu mtakayoanzisha.

Na bado kuna kukopa na misaada mingine ambazo nazo bado zitatolewa kwa dola ya Marekani, hivyo hayo ni mambo ya kwenye vijiwe vya tangawizi tu.
 
Ndio tunatakiwa tuchague au kupendekeza jina moja.... Mfano Euro, inatumiwa Ulaya, kila nchi inatumia Euro barani ulaya...

Afrika napo tunataka Sarafu yetu ili kuepuka misukosuko ya Dollar kupanda na kushuka... Wewe unapendekeza jina gani, na namna ipi tufanye hii sarafu kuwa Hai

Hata Uingereza inatumia Euro?
 
Kweli tutamkumbuka sana mwamba Gadaffi na wengine waliokuwa na mawazo haya
Hongera zako mkuu ila kwa Africa ni waoga sana mpaka mito yao ya maji hawana uhuru nao
Kila kitu tunaogopa kufanya

Leo kama tuna akili tungekuwa na matajiri wakubwa duniani kwa kuwa na maduka ya almasi na dhahabu kuanzia London, Paris na NY hata Dubai
Ila hizi ni ndoto zangu tu
 
Mpango wa kuipatia dola jina lingine ila thamani yake itabakia pale pale....jamani Waafrika tufanye kazi.
 
Mkishaanzisha hiyo sarafu bado mnatakiwa kulipa madeni yenu ambayo ni trilioni za dola kwa US$ na wala sio kwa hiyo sarafu mtakayoanzisha.

Na bado kuna kukopa na misaada mingine ambazo nazo bado zitatolewa kwa dola ya Marekani, hivyo hayo ni mambo ya kwenye vijiwe vya tangawizi tu.
Kweli aisee! Hili lipo tricky sana
 
Mabadiliko uanza na mimi... Kama kila mwafrika mmoja akiweka nia ya kuwa na sarafu mmoja, hili jambo linawezekana... Muammar Gaddafi aliibuka wakati mbaya, Siasa za kibeberu usijitoe wewe kama wewe kupingana nao, wewe sema wananchi ndio wamesema... Huoni Burkina Faso na Mali walivyomuweza Mfaransa, sio mtu mmoja ambaye alitoka kupigania nchi, bali raia wote... Lakini kule Libya kilichomua Gaddafi ni baadhi ya wananchi wake kuanza kumuita Dictator, wananchi wengine hawakumuunga mkono, na Marekani akishaona tu wengine hawakuungi mkono, ndio anawatimua hao hao kukuangamiza... Sasa sisi kama Afrika na mwafrika mmoja mmoja sote kwa pamoja tukisimama hawawezi kufanya kitu... Niger, Mali na Burkina Faso wananchi wote hawakutengana, waliungana na kua taifa kama taifa
Ndicho nilichosema mkuu viongozi wote wa africa waungane na waweke misimamo sisi wananchi tukiona hivyo nasi tutaunga mkono tu wala hatuwezi kuwa na shida, ila kama viongozi wao wenyewe tu wanageukana na wengine ni mamluki sisi wananchi wa kawaida hatuwezi kuwa na nguvu yoyote ya kupitisha hilo hata hizo nchi za magharibi kuungana ni kwa sababu viongozi waliamua hilo, maana wananchi walianza kupiga kelele muda mrefu ila viongozi walipoamua tu kwamba kweli sasa ni muda wa kumkataa mfaransa ndio habari ikaishia hapo
 
Back
Top Bottom