Bara la Africa limelaaniwa na Mungu

Bara la Africa limelaaniwa na Mungu

Duniani kote angalia sehemu wanazoishi watu weusi...ni za kusikitisha mpaka unajiuliza watu weusi ni wapi tulikosea
 
Yani wale ambao kwao wenye kulawitiana wana haki zao,na bila aibu wanatulazimisha hadi na sie waafrika. Lakini bado wasilaaniwe ila tulaaniwe sie tu?
Ndio tatizo letu kusukumia lawama mahala pengine kuna watu kama ulivyoainisha hapo yote hayo hawajalaaniwa ila sisi.Nadhani mentor of slave kama alivyoimba Nesta marley inatuhusu na inajumuisha kujikomba na kutosimamia mambo yetu wenyewe ukija jumlisha ulafi na unafiq wa viongozi wetu bila kutizama kwa makini utakimbilia conclusion ya laana.
 
Nchi za kaskazini mwa afrika zimepiga hatua kubwa sana ya maendeleo, kuna baadhi ya nchi huwezi kujua kama ziko afrika,siamini kama kuna laana ila kuna tatizo la uongozi tu
 
Kwa sababu wayahudi walichaguliwa na Mungu by then na hata vitabu vya dini(kwa tunaoamini)vinaliongelea ilo,na vina simulia neema mbali mbali ambazo mayahudi walipewa na Mungu ikiwemo kuwa na Elimu kubwa sana na hata kula msosi toka mbinguni...wewe hata ndotoni hujawahi kuula huo msosi wa peponi.
Na ww unamini hvyo kabsa? Vitabu vyote vya dini vnasema wayahudi wamekuwa wakimkosea mungu lakin mungu asiwaalan awalaani wafrika? Bac mungu atakuwa hana Upendo
 
Hv nyie mbona mnamzalilisha huyu mungu wenu? Alafu mnasema yy n mwenye upendo... Kweli mungu mwenye upendo ndo anayafanya haya ??
 
Hapana kuhusu qadar coz ukiisoma historia ya Africa uzuri utaona wale wapigania uhuru wa kwanza nyerere,kwame,sekou toure,lumumba,kaunda walikuwa wanakiamini walichokuwa wakikihubiri na ndo maana watakumbukwa kwa muda mrefu baada yao ndio wakaja hawa muflis wa nafsi ambao sio tu walafi isipokuwa wafujaji wa mali zetu.
Swali litakuja kwnn yote haya yalijitokeza Africa na sio mabara mengine?na mbona kuna mabara pia yalitawaliwa lkn hayapo kama ilivo africa?
 
huwezi kusema afrika inarudi nyuma kwa sababu ya viongozi bali afrika inarudi nyuma kwa ujinga wa waafrika wote.

kila mwanadamu ana uwezo alio nao kulingana na mazingira yalimuumba vipi kufikia hapo alipo yaani mifumo ya elimu rasmi na zisizo rasmi inawafanya wanadamu ukubwani wawe na uwezo tofauti ingawa wakati wa kuzaliwa wanakuwa sawa wote.

kama unavyoona wanyama wanavyotoa products tofauti mfano kuku anatoa mayai, ngombe anatoa maziwa, mbwa yeye ulinzi kwake ni namba moja na wengine ndivyo wanadamu wanavyokua ukubwani kila mmoja na product yake.

sasa ili jamii iweze kusonga mbele inahitaji kutumia wanadamu hawa jinsi mazingira yalivyowaumba.

huwezi kuwa unahitaji maziwa ukafuga kuku au mbwa akakupa product ambayo hukulenga ukabaki kumlaumu huyu kuku au mbwa eti hakukupa maziwa.

viongozi ni kama wanyama hawa, huwezi kumlaumu kiongozi aliyeshindwa kukuletea maendeleo maana amefanya kwa kadiri ya uwezo wake bali ajilaumu yule alifanya makosa katika kuchagua.

ikifika uchaguzi waafrika tunabeba ajenda ambazo haziwezi hata siku moja kutupatia viongozi bora na matokeo yake ni kupata viongozi kulingana na ajenda tunazozitumia alafu tunaanza kumlaumu hawa tuliowachagua kwa vigezo visivyo sahihi.



Mkuu waliokalaaniwa si Waisrael?


Vipi tuangalie level ya maendeleo na kwetu nadhani tutapata jibu nini kinatusumbua Afrika ila kiukweli ni uzembe wa viongozi wetu, uongozi mbovu n.k
 
Mimi Naungana na wewe juu ya Laana ilalolitafuna Bara la Africa, ni wachachetu watakaopinga nani kwa sababu ya kutokumjua Mungu na Maneno yake.

Katika Biblia kuna kiongozi aliyekuwa anaitwa Ahabu, huyu bwana alipo tawala Nchi Alikuwa Amelaaniwa, na alipelekea nchi kuugua kutokana na Laana zilizokuwa juu ya kichwa chake, kupelekea ugumu wa maisha kwa wananchi wake.

"Asomaye na Afahamu"
Isaya 1:4-9
Ole wake taifa lenye dhambi, watu wanaochukua mzigo wa uovu, wazao wa watenda mabaya, watoto wanaoharibu; wamemwacha BWANA wamemdharau yeye aliye Mtakatifu wa Israel, wamefarakana naye na kurudi nyuma.

Nchi yenu ni Ukiwa; miji yenu imeteketezwa kwa moto, nchi yenu, wageni wameila mbele ya macho yenu, nayo ni ukiwa kana kwamba imeangamizwa na wageni.

"ASOMYE NA HAFAHAMU"
 
Sio kweli viongozi wetu ndio waliolaaniwa! wabinafsi, waongo, wezi, wanafiki, kila aina ya ushetani! ila sio wote!
 
Heri taifa Ambalo BWANA ni Mungu wao. (Zaburi 33:12)

Tujiulize Tanzania Mungu wake ni Nani?
 
Nchi za kaskazini mwa afrika zimepiga hatua kubwa sana ya maendeleo, kuna baadhi ya nchi huwezi kujua kama ziko afrika,siamini kama kuna laana ila kuna tatizo la uongozi tu
Unakumbuka lkn walichomfanyia Gadafi ktk moja ya izo nchi za north of africa?yale matendo yao utasema yanasababishwa na nini?
 
Na ww unamini hvyo kabsa? Vitabu vyote vya dini vnasema wayahudi wamekuwa wakimkosea mungu lakin mungu asiwaalan awalaani wafrika? Bac mungu atakuwa hana Upendo
Mungu anasema Mayahudi wamekasirikiwa...rejea qur an 1:6-7
 
We fikiria ccm hakushinda ikalazimisha kuchukua madaraka! Pale Uganda kila MTU aliona jinsi museven alivyo ibakura kimabavu na bado wenzie was eac wakainuka Kumpongeza kwa ushindi wa kishindo!!haya mashetani yakiondoka hili bara litakuwa nchi ya Maziwa na asali Kama Mungu alivyo ahidi
 
Ni ukweli usio na ubishi wowote kuwa bara la africa lililaaniwa na Mungu.
Huu ndo ukweli halisi ambao ni wapumbavu tu wanaweza kuukataa.
Haiwezekani nchi zote 55 za africa zenye raslimali za kila aina na ambazo hakuna bara lolote duniani linazo.

Taifa lina dhahabu, gesi, ardhi nzuri Kwa kilimo, almasi, bahari, maziwa, misitu, lakini eti bado ni maskini na ombaomba. Ghadaffi alipojitahidi Kwa akili zake zote kuinua uchumi wa libya hadi Libya ikawa haidaiwi na taifa lolote,wananchi wake wakamuua kikatili Kwa point feki ya kukaa madarakani muda mrefu, zote hizo ni laana.

Kama mwenyezi Mungu ametupatia raslimali zote hizi na bado hazitusaidii, hiyo ndo laana zenyewe sasa. Baraka Zipo Kwa mtu mmoja mmoja Kwa kadri anavyoamua kumtegemea Mungu Kwa akili zake zote. Hakuna baraka za taifa ila kuna laana ya taifa.Viongozi wa afrika ni walafi, wabinafsi, Wachoyo, wezi na makatili, hawaijui kesho ya raia wao.

Nilibahatika kuishi Finland miaka mitatu, Kwa utaratibu wa maisha ya hawa watu, hata iweje hatuwezi kuwafikia.Raia wa Finland wasio na ajira hupokea posho ya kupunguza ukali wa maisha kila mwezi.

Wanyonge hutibiwa bure, na kusomeshwa bure kuanzia kindergarten hadi chuo kikuu. 60% ya ardhi ya Finland ni maji na 40% ndo nchi kavu, hawana raslimali, wanategemea viwanda waliyovipta Kwa shida, Finland husaidia nchi kibao za africa.Viongozi wa africa wapo tayari kuuwa watu ili watawale, ni mlolongo Wa laana.

Huyu ni mtoto anayeviziwa kuliwa na tai akifa, Sudan, mwandishi Kevin Carter aliyefanikiwa kupiga hii picha alijiua baadae Kwa stress, mtoto huyo alikuwa akijongea kwenye kambi ya chakula.
Umenikumbusha kule Zanzibar mkuu...
 
Back
Top Bottom