Bango Hili La Mchina Hatare!!

Bango Hili La Mchina Hatare!!

PakaJimmy

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2009
Posts
16,202
Reaction score
8,783
Mchina ni noma jamani!
Kuanzia Balozi wao hadi Makampuni yao ya ujenzi ni majanga!
Hapa ni kibao cha Ujenzi kilichowekwa eneo la Majengo Chini Arusha, ambapo kuna ujenzi wa barabara inayounganisha barabara ya Dodoma na ile ya Nairobi. Kampuni inayohusika inaitwa CRSG (China Railway Seventh Group)

2013-09-21+15.35.18.jpg
 
Hiki KIZUNGU ni mgogoro kwa wengi kumbe!! Nilidhani ni kwetu tuu akina Kayumba....🙂
 
Kingereza majanga na makelele, mradi wajenge kwa kiwangi stahiki. Wasije kufanya kama ile ya Kilwa.
 
Hahahahaha dah. Ila kwa wachina sishangai sana maana wao wameweka lugha yao mbele kuliko za mataifa mengine makubwa kama kiingereza, kijerumani na kifaransa. Mara nyingi wanapopata kazi kwenye nchi flani huwa wanajifunza kwa muda lugha kubwa inayotumika katika hiyo nchi. Sasa kwa Tanzania wengi wetu wanakithamini kiingereza na hadi kuwa ''an official language'' na kukiweka pembeni kiswahili.
Bora hivyo kitaeleweka kinachofanyika kuliko wangeandika Kichina chao. Mataifa mengi miaka hii ya karibuni wanajifunza kiswahili lakini sisi waswahili wenyewe hatuweki juhudi katika kuikuza lugha yetu ya kiswahili.
 
Sehemu nyingine watasema "the road is not snake one by one" barabara haijanyoka moja kwa moja.
 
cc pmwasyoke.
Ina maana mradi kama huo hauna Resident Engineer na Consultants?...na hata kama hiyo si sehemu ya kazi yao, je bango hilo haliwaletei ukakasi kwenye Bongo zao?
 
Last edited by a moderator:
Mchina ni noma jamani!
Kuanzia Balozi wao hadi Makampuni yao ya ujenzi ni majanga!
Hapa ni kibao cha Ujenzi kilichowekwa eneo la Majengo Chini Arusha, ambapo kuna ujenzi wa barabara inayounganisha barabara ya Dodoma na ile ya Nairobi. Kampuni inayohusika inaitwa CRSG (China Railway Seventh Group)

2013-09-21+15.35.18.jpg
Ni kweli PakaJimmy. Kampuni hii ya kichina ama ina madharau au haijui kanuni za mabango ya ujenzi kwa mujibu wa CRBM au mamlaka ya ujenzi hapa Tanzania. Bango hili hapa limekaa kichizi sana!
 
Last edited by a moderator:
Baba yangu mdogo yupo kwenye hii kampuni. Sijui ndiye kaandika? Hahaha......
 
"The Front is working" Ha ha ha hahaaa...!!! nimeteguka mbavu..
 
  • Thanks
Reactions: awp
Ni kweli PakaJimmy. Kampuni hii ya kichina ama ina madharau au haijui kanuni za mabango ya ujenzi kwa mujibu wa CRBM au mamlaka ya ujenzi hapa Tanzania. Bango hili hapa limekaa kichizi sana!

TANROADS NI USELESS. Kama wanafumbia macho upuuzi kama huu, bila kufikiri mnawatupia lawama wachina, mtanishangaza.
 
Back
Top Bottom