Balozi Lusinde: Lowassa Safi na Anatosha

Balozi Lusinde: Lowassa Safi na Anatosha

OgwaluMapesa

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2008
Posts
10,942
Reaction score
437
Wakati wagombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuwania nafasi ya urais ikifika 32, mwasisi wa chama hicho, Balozi Job Lusinde amesema wimbi hilo ni ishara ya kupanuka kwa demokrasia, huku akisema Lowassa ni mtu safi na anayefaa kwa wakati huu...

Akizungumza jana katika mahojiano maalum na gazeti hili, Balozi Lusinde alisema kada huyo wa CCM ni kiongozi mchapakazi na mwadilifu... Alisema watu wanaopita katika maeneo mbalimbali nchini na kuchafua wagombea wengine wanastahili kuchukuliwa hatua kali sana, kwani tabia hiyo si nzuri...

"Ni Lowassa huyu huyu aliyefutilia mbali mkataba wa City Water baada ya kubaini ni wadanganyifu. Richmond ukiulizwa anahusika vipi huwezi kujibu kwa sababu hausiki. Edward Lowassa ni kiongozi mchapakazi kweli kweli na mwadilifu"..

"Lowassa anaadhibiwa kwa ubunifu wake, kwani alikuwa anahangaika kutafuta suluhu ya tatizo, kama Richmond ilikuwa na tatizo mbona tulinunua Dowans na Obama (Rais wa Marekani) akabariki," alisema Balozi Lusinde....

Huu ni muda wa chama kusimama imara, kuwa na umoja na mshikamao na sio kuwaachia baadhi ya wagombea wanaopita katika maeneo mbali mbali nchini na kuchafua makada wenzao.....

Mpaka sasa makada wa CCM ambao wamechukua fomu kuomba kupeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu hadi kufikia jana ni 32...

Jambo Leo... 14.06.2015...
 
Lowassa ndio chaguo la watanzania kwa sasa...... Bila Lowassa tutaandamwa na umasikini kwa zaidi ya miaka 10 ijayo
 
Balozi Lusinde juzi alikua pamoja na Pinda Dodoma wakati akichukua fomu ya urais. Hivyo tunajua tayari Lusinde yupo na Pinda.

Mleta mada njaa zako za kuongwa pesa za kununulia boxer zitakuahibisha sana pindi jina la huyo ATM wenu litakavyo galagazwa.
 

  • Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), DK. Muzzammili Kalokola jana alichukua fomu ya kuomba kupitishwa kugombea urais, lakini akakiponda chama hicho kuwa kinaiba sera za vyama vya upinzani; mfano wa sera ambayo haikuwa mali ya CCM ni Katiba Mpya. Hii haikuwa mali ya CCM, lakini tumeiiba nakuifanya iwe mali yetu, na tumetumia fedha nyingi kutengeneza katiba mpya' ambayo bado ni mbovu. "Nitaipinga tu mahakamani, kwa kuwa haina sifa, alisema Dk. Kalokola.

    Pia amesema; sababu zinazotolewe za kushuka kwa shilingi ya Tanzania ni za uongo tu, na kwamba ukweli ni kwamba fedha nyingi za kigeni zimehamishiwa nje ya nchi kwa wingi. "sasa tujiulize kuwa ni nani anapeleka fedha nje ya nchi ?" alisema DK. Kalokola.

    Chanzo: Mwananchi, Jumapili, Juni 14, 2015



 
Balozi Lusinde juzi alikua pamoja na Pinda Dodoma wakati akichukua fomu ya urais. Hivyo tunajua tayari Lusinde yupo na Pinda.

Mleta mada njaa zako za kuongwa pesa za kununulia boxer zitakuahibisha sana pindi jina la huyo ATM wenu litakavyo galagazwa.

Hahaha...mtaelewa tu mwaka huu.
 
Tumuamini nani kati ya Lusinde na Nyerere?

kwani Nyerere alisemaje ndugu???tuache kumlisha nyerere maneno
lowassa hafai urais kwa mujibu wangu na sii nyerere au lusinde, natumia akili zangu
hapa anayefaa ni MAKO na au MAGUFULI
 

  • Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), DK. Muzzammili Kalokola jana alichukua fomu ya kuomba kupitishwa kugombea urais, lakini akakiponda chama hicho kuwa kinaiba sera za vyama vya upinzani; mfano wa sera ambayo haikuwa mali ya CCM ni Katiba Mpya. Hii haikuwa mali ya CCM, lakini tumeiiba nakuifanya iwe mali yetu, na tumetumia fedha nyingi kutengeneza katiba mpya' ambayo bado ni mbovu. "Nitaipinga tu mahakamani, kwa kuwa haina sifa, alisema Dk. Kalokola.

    Pia amesema; sababu zinazotolewe za kushuka kwa shilingi ya Tanzania ni za uongo tu, na kwamba ukweli ni kwamba fedha nyingi za kigeni zimehamishiwa nje ya nchi kwa wingi. "sasa tujiulize kuwa ni nani anapeleka fedha nje ya nchi ?" alisema DK. Kalokola.

    Chanzo: Mwananchi, Jumapili, Juni 14, 2015




TUNATAKA wana ccm wa aina hii na sio wafagilia ujinga kuinda shibe/lishe ya matumbo yao.
 
Balozi Lusinde amekua msemaji wa Lowassa? Lowassa yeye mwenyewe hawezi kemea rushwa hata dakika moja,uadilifu wa Lowassa ni upi kama sio Kumpamba Fisadi sifa asizo nazo
 
Hii ni dalili tosha kwamba hakuna kiongozi imara na anayekubalika zaidi kwa wananchi licha ya wagombea wenzake kukosa sera na kuanzia kutumia jina la lowasa kama sera zao katika kutangaza nia kumbe hawajui wanajikaanga wenyewe kwa mafuta
 
Balozi Lusinde juzi alikua pamoja na Pinda Dodoma wakati akichukua fomu ya urais. Hivyo tunajua tayari Lusinde yupo na Pinda.

Mleta mada njaa zako za kuongwa pesa za kununulia boxer zitakuahibisha sana pindi jina la huyo ATM wenu litakavyo galagazwa.

We mwanamke kweli mwehu..... Lusinde alikuwa Arusha uwanja wa Amri Abeid... Soma gazeti la leo hata mimi pia nimelisona.... Kawasifia Lowassa na Muhongo..... Usiwe unakurupuka wewe mamaaaa
 
kwani Nyerere alisemaje ndugu???tuache kumlisha nyerere maneno
lowassa hafai urais kwa mujibu wangu na sii nyerere au lusinde, natumia akili zangu
hapa anayefaa ni MAKO na au MAGUFULI

Hahahaha Makongoro kweli kuna vichaa hapa duniani......

Magufuli ukimuliza hata Mkt wa Ccm mkoa wa Mara hamjui, mtu kama huyo hatuwezi kumpa chama Mkuu
 
Je ile dhana kuwa ni zamu ya Zanzibar ipo?

Je kwenye mawazo ya Wakristo.... Ni zamu ya Mkristo.... Ina madhara yeyote katika uteuzi kwa CCM na UKAWA?

Tunaomba wachambuzi wa mambo waseme hapa.... Uchambuzi tafadhali wa kitaalamu..

Comment mstari mmoja ama 2 haisaidii kupanua mjadala..
 
ocampo four

Huyu Mzee ana retire Imprest ya alichokula. Hana jipya zaidi ya kutaka kuhalalisha maovu aliyotufanyia akiwa waziri.
 
Last edited by a moderator:
Balozi Lusinde amekua msemaji wa Lowassa? Lowassa yeye mwenyewe hawezi kemea rushwa hata dakika moja,uadilifu wa Lowassa ni upi kama sio Kumpamba Fisadi sifa asizo nazo

Wataanzania wanazidi kuelewa ukweli kuhusu Richmond
 
1. Wazee wamechoka. . . . .. Wakati anajiengua mbona hakusema??!!!
2. Hayo ya Dowans angeyasema lini kama Lowassa asingegombea? ?!!
3. Amemueleza mwenyekiti wake kuwa alipokubali huyu candidate kujiengua uwaziri mkuu alifanya kosa??!!

Kama kweli ni mzalendo mbona hasemi kwa uwazi akaeleweka juu ya hiyo Richmond??!!!
 
Back
Top Bottom