GE2025 Balozi Ali karume amvaa Humphrey Polepole

GE2025 Balozi Ali karume amvaa Humphrey Polepole

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025
sidhan kama takwa hilo la kuwa planepontery maana weng wameteuliwa hata hapa kenya wala hawakua maafsa.hata huko tz weng tu. pili naskianga aliwah kushambulia pres mwiny kipind flan? was that diplomatic ethicals
 
Balozi Ali Karume ameelezea mahusiano ya kipekee kati ya Cuba na Afrika ikiwemo Tanzania .


TOKA MAKTABA :

Havana, Cuba

Cumbre de Jefes de Estado y de Gobierno del Grupo de los 77 y China

tarehe 14 September 2023
Mwandishi
Na Pedro Rioseco


View: https://m.youtube.com/watch?v=Lhxm7jatf5U

Mh. Rais Dr. Hussein Mwinyi akiwa na balozi wa Tanzania nchini Cuba Mh. Humphrey Hesron Polepole uwanja wa ndege wa Aeropuerto Internacional José Martí de La Habana nchini Cuba.


Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Hussein Mwinyi amewasili nchi Cuba kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Hassan katika mkutano wa nchi za kundi la G77

Rais wa Cuba Miguel Díaz Canel Bermúdez ataongoza Ijumaa hii tarehe 15 hadi Jumamosi tarehe 16 September 2023 Mkutano muhimu wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kundi la 77 na China kujadili mada "Changamoto za sasa za maendeleo: Jukumu la Sayansi, Teknolojia na Ubunifu" .

Likiwa limeitishwa na Cuba, katika nafasi yake kama mwenyekiti wa muda nchi za G77 tangu Januari iliyopita, Kundi hili G77 ndilo kambi kubwa zaidi ya nchi zinazoendelea ndani ya Mfumo wa Umoja wa Mataifa na kundi la mashauriano tofauti zaidi katika nyanja ya kimataifa.

Inajumuisha nchi wanachama 134 ambazo zinawakilisha theluthi mbili ya wanachama wa Shirika la Umoja wa Mataifa na asilimia 80 ya idadi ya watu duniani, ambayo inaonyesha jukumu lake muhimu.


G77 Ilianzishwa mnamo Juni 15, 1964 kama kikundi cha nchi zinazoendelea na ambazo hazijaendelea kwa madhumuni ya kusaidiana, kudumisha na kusaidiana katika mijadala ya Umoja wa Mataifa, jukumu lake katika nyanja ya kimataifa lilikua na ujumuishaji uliofuata wa nchi za Ulimwengu wa Tatu.
Source : https://www.contraloria.gob.cu/noti...te-reunion-cumbre-del-grupo-de-los-77-y-china


15 September 2023
Havana, Cuba

RAIS DR. HUSSEIN MWINYI AKIHUTUBIA MKUTANO WA G77+CHINA MJINI HAVANA CUBA
1757689004899.png

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amehutubia Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kundi la G77+ China akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.



Akihutubia katika Mkutano huo, Dkt. Mwinyi amesema Sayansi, Teknolojia na Ubunifu ni nguzo muhimu kwa nchi zinazoendelea kujiletea maendeleo ya kiuchumi na kuongeza kuwa nchi hizo zinaweza kuendelea kiuchumi kupitia maendeleo katika sekta muhimu za kilimo, nishati, elimu, afya, madini, maendeleo ya muindombinu, maji na mazingira.

Mhe. Rais Dkt. Mwinyi amekumbusha namna nchi zinazoendelea zilivyoathirika na janga la maradhi ya UVIKO-19, bidhaa kupanda bei, mizozo ya kisiasa na athari za mabadiliko ya tabia nchi na kuongeza kuwa baadhi ya changamoto zilisababisha kupanda kwa gharama za maisha na kudhoofisha jitahada za kujikwamua kiuchumi.



Mhe. Dkt. Mwinyi alikumbushia namna nchi zilizoendelea zilivyobanwa na teknolojia ya kutengeneza chanjo na kunyimwa msaada wa kiteknolojia ili zitengeneze chanjo zao na kusababisha kampuni za kutengeneza dawa za mataifa tajiri kupata faida kubwa kwa kuziuzia nchi zinazoendelea chanjo ya UVIKO-19.å

Mhe.Dkt. Mwinyi amezitanabaisha nchi za kundi la G77+China kuchukua changamoto hizo kama somo na zisibweteke kusubiri msaada kutoka mataifa yaliyoendelea.



Mkutano huo unaofanyika jijini Havana nchini Cuba tarehe 15-16 Septemba 2023 unayakutanisha mataifa yanayoendelea unajadili changamoto zinazoikabili dunia baada ya kuathirika na janga la UVIKO-19 na migogoro inayoendelea duniani na vikwazo mbalimbali vya kiuchumi.



Mkutano huo umejikita kutafuta namna bora ya kujenga ustahimilivu kupitia maendeleo ya sayansi na teknolojia na ubunifu ili kundi la G77+China liweze kufikia malengo yake kwa pamoja.



Kaulimbiu ya Mkutano inasema, “Changamoto za Maendeleo: Nafasi ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu”.
 
TOKA MAKTABA :

Mazito aliyosimamia mheshimiwa Polepole alipokuwa balozi nchini Cuba,

14 September 2023
Havana, Cuba

RAIS HUSSEIN MWINYI AZINDUA JENGO LA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI CUBA
1757687636797.png

Rais Dr. Hussein Mwinyi na makamu wa rais wa Cuba Mh. Salvador Valdés Mesa wakikata utepe kuashiria ufunguzi wa jengo la ubalozi wa Tanzania Havana Cuba. Pia mikataba kadhaa ya makubaliano imesainiwa baina ya Cuba na Tanzania .

Mahusiano ya Tanzania na Cuba yalianza enzi za Julius Nyerere miaka ya 1960 huku Che Ernesto Guevara akifika Tanzania ..

View: https://m.youtube.com/watch?v=q6629qSntRk

El vicepresidente de Cuba, Salvador Valdés, asistió hoy a la apertura de la embajada de la República Unida de Tanzania en el contexto del inminente inicio mañana aquí de la Cumbre del G77 y China.
1757687748426.jpeg

Vicepresidente de Cuba asiste apertura de embajada de Tanzania (+Fotos) - Prensa Latina

Source : Prensa Latina TV
 
TOKA MAKTABA :
MAHUSIANO YA CUBA NA TANZANIA

2024 26 January

JAKAYA KIKWETE NA MAKAMU WA RAIS WA CUBA SALVADOR MESSA,
mstaafu rais Jakaya Kikwete ambapo rais mstaafu alishukuru misaada ya Cuba toka enzi za mapambano ya kutafuta uhuru wa Afrika yaliyochagizwa kupitia Ernesto Che Guevera,


View: https://m.youtube.com/watch?v=ajTrgFceFYE
Antes de su partida a Zimbabwe , el miembro del Buró Político y vicepresidente de la República de Cuba Salvador Valdés Mesa, sostuvo intercambios con personalidades y altos funcionarios del gobierno de la República Unida de Tanzania como parte de la visita oficial que realizó a esa nación de África.
 
TOKA MAKTABA :

Utumishi wa mheshimiwa Polepole akiwa balozi

2023 15 March
Humphrey Herson Polepole : First international Joint Cardiovascular medical camp by Tanzania and Malawi


View: https://m.youtube.com/watch?v=82RUFnhzdzk
An international Joint Cardiovascular medical camp was held by Tanzania and Malawi fromMarch 20 -26 2023 . It was not the "first" such camp, as there have been previous collaborations. The camp was hosted in Blantyre, Malawi, and featured specialists from Tanzania's Jakaya Kikwete Cardiac Institute (JKCI) and Malawi's Queen Elizabeth Central Hospital (QECH).
 
Balozi Ali Karume amkosoa vikali Humphrey Polepole

View: https://m.youtube.com/watch?v=sN6hZvI5faY
Mheshimiwa Polepole ni mwanasiasa shughuli ya ubalozi hakuwa anaufahamu kuielewa wala hakutaka kujifunza ndo maana tunaona haya yaliyotokea, balozi Karume anapigilia msumari harakati za Polepole


Ali Karume aliyewahi kutumikia wadhifa wa kidiplomasia kama balozi kwa miaka 27 amesema Humphrey Polepole mazungumzo yake amekiuka imani aliyopewa na mteuliwa wake balozi namba moja aliye rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Balozi Ali Karume anafafanua balozi kamili wa ukweli ni wale walioanza kazi katika wizara ya mambo ya nje na kufikia ngazi ya minister plenipotentiary grade one katika mafaili yao ya utumishi ndani ya wizara kabla ya kupewa ubalozi, tofauti na kina Polepole wanaopachikwa juu kwa juu kuwa mabalozi wasio na uzoefu wizarani

Balozi Ali Karume anaongeza kuwa tuchukulie mfaño mahusiano mema na ya aina ya kipekee katika ya Cuba na Tanzania, hivi kweli balozi wa Cuba nchini Tanzania angeweza kujiuzulu na kuanza kuishambulia nchi yake ya Cuba ?

Balozi Ali Karume amesema yu tayari kuanzisha mazungumzo na Humphrey Polepole katika jukwaa lolote liwe katika televisheni, ZOOM, YouTube ili kuongelea masuala mbalimbali wabadilishane mawazo

Balozi Ali Karume anasema hali hii ya Polepole kuanza mazungumzo yake ipo haya mamlaka za uteuzi za nani anakuwa balozi wetu nje kuwa na njia bora zaidi za kuchuja nani anafaa kuwa balozi ili taifa liepukane na aina ya mheshimiwa Humphrey Polepole kupenya na kuwa balozi isitokee.

Wanazidi kutoka mapangoni 🤣🤣🤣🤣
 
Mnufaika wa mfumo haoni chochote nchi inapitia
 
Back
Top Bottom