Ballali aibuka na kujibu

Status
Not open for further replies.
. Bila shaka ndiyo mwanzo mkubwa wa kusambaratika kwa CCM. Wapinzani kwa ujumla kwanini kusifanyike kwa maandamano nchi nzima ya kumuunga mkono aliyefichua bomu hili na kulaani vikali wizi na uzembe wa CCM?..

Unamjua aliyefichua hilo bomu kabla hujaiitisha maandamano! Au unakurupuka tu? Angalia quote hii kutoka page 2 ya thread hii!!!

 
watu walidhani tunawatania.. chess.. juu ya chess.. watu waende kusoma raiamwema.co.tz pale juu kuna kaujumbe...

http://www.raiamwema.co.tz/08/01/16/3.php



Pia:http:Mawaziri wahojiwa:
//www.raiamwema.co.tz/08/01/16/1.php
 
Mkuu Halisi,

Bwana wee! makubwa haya!

Ila hii ya kwamba alitumiwa ni ujinga mtupu. Muhimu kama ameanza kuropka kama wale wasaidizi wa Saddam. Atatusaidia kumkamata the big fish.

Hapo mchezo utakuwa mtamu sana, kama JK anataka kuondoa corruption basi awe tayari ku bargain na Ballali ili kuhakikisha wengine wote wananaswa. Anaweza kumhakikishia japo msosi wa maana na matibabu akiwa Keko.
 
Hivi na Balali ameanza kuwa kama OSAMA? Kutoka Ugavana sasa anaanza kuibuka ibuka tu.

Halafu nani ana uhakika kama zile barua zilizotumwa na mama Meghiji ziliandikwa kipindi kile?
 
Breaking News toka Iringa ni kwamba mganga wa kienyeji wa Balali anayejulikana kwa jina GM (nafupisha kutomharibia soko) amethibitisha kuwa ndugu Balali ni mzima wa afya na atarudi Tanzania kusafinya jina lake baada ya yeye Mganga kukamilisha shughuli za maandalizi ya ujio wake!
NB: This is not a Joke
BTW
Wana JF Tanzania naomba mnirekodie Ze-Comedy ya leo kuhusu BOT please!
 

Kwa mtindo huu watanzania tutakuwa tunazunguka katika mduara tu bila kufika popote.
Sasa tunataka Ballali 'a-bargain' kwa manufaa yake? Tunajuaje kuwa ufisadi haupo kwenye hiyo ofisi kubwa!

Tumwache Ballali ajitetee kivyake, bila ya kumning'inizia peremende zenye sumu ya panya.
 
Unamjua aliyefichua hilo bomu kabla hujaiitisha maandamano! Au unakurupuka tu? Angalia quote hii kutoka page 2 ya thread hii!!!


Nadhani aliyeibua sakata hili ni Slaa, maana kama kawaida serikali huwa inafanya vitu vyake ndani kwa ndani na hata matokeo ya uchunguzi yakitoka huwa hatusikii chochote, wanaamua wanavyotaka wao bila kujali public opinion au wakuadhibiwa aadhibiwe.

Kitu alichofanya Slaa was History, he made History, yaani kwa mara ya kwanza tumeona kiongozi akiwachukulia wananchi kama waajiri na kweli wenye nchi akaenda kushitaki kwao! the resonance which came out was big BIG, hata Mahakama kuu ya Tanzania isingeweza kuleta muamko na matokeo tuyaonayo sasa.

Jamaa made it so big mpaka Mataifa wahisani wakaingilia kati, mpaka wananchi wa vijijini wakawazomea mawaziri waliotaka kutetea ujinga.

So, Yes wakupongezwa hapa ni Slaa, mafisadi wanamuogopa kuliko hata Raisi.

Nakumbuka wakati alipokuwa anachimba mkwara kwamba atashitaki kwa wananchi kuna watu humu ndani walidiriki kusema kwani wananchi wana uwezo wa kufanya nini? yaani Slaa gave wananchi so much power they never thought they had.
 

Kalamu,

Polisi yeyote wa maana hapa duniani atakuambia ukimkamata jambazi, kitu cha kwanza unamwambia yuko kwenye hot water, sasa aamue atapunguzaje maumivu yake.

Kwa habari alizo nazo Ballali, ningelikuwa JK, na kama kweli nataka kunasa kila mtu kwenye huo mtandao, ningekubali ku bargain naye.

Wenzetu ndivyo wanavyomaliza mitandao ya madawa na hata Italy ndivyo walivyoweza kuwapunguza sana Mafia.

Vinginevyo tutapata nusu ukweli na nusu uwongo.

Kama serikali ina kila kitu then hakuna haja ya ku bargain naye. Nina wasiwasi kwa serikali ya Kizembe kama yetu kama wanajua kila kitu.
 
Mtanzania, tatizo wao hawataki kukamata wote wanaohusika.. wanataka kupata mtu mmoja, ili yaishe..!
 
I smell KADA MPINZANI in making. Yule aliyekuwa katika kundi la watu wa ajabu. Endelea FISADIST- I mean FISI DUST

Asha
JENGA HOJA ACHA MAJUNGU YA KUTAFUTA NANI KASEMA.aka KUWA NA TABIA ZA KIUME.Ni kichekesho mtu kukubali kufanya wizi wote huo kama alikuwa katumwa na kigogo flani,ina maana yeye hakuwa na maamuzi binafsi!!!!!!!!!!!!aliona nini kuresigne kama kweli analipenda taifa lake.mbona Mwakyembe alipoona kuwa NBC mambo hayaendi sawa alijivua ujumbe wa board?Na KWA NINI TUMWAMINI KUWA NI MKWELI WAKATI ALIDILIKI HATA KUMDANGANYA MAMA ZAKIA KUWA MALIPO NI HALALI WAKATI SIO KWELI?AKINGOJA MPAKA AFUKUZWE NDIO ASEME?ANAEKUFA HAACHI KUTAPATAPA.BALALI KUFA MWENYEWE HUSITAKE MKUCHAFUA BABA ZETU WAADILIFU
 

We fisadi mchanga acha utaahira.
 
....Halafu pamoja na yote haya-Richmond, Loliondo, Benki Kuu, Mkapa kufanya biashara ikulu, maisha duni, rada, Buzwagi na mengine mengi tu ambayo nikiamua kuyataja sitamaliza-lakini bado CCM inachaguliwa kwa vishindo na watu wanaimba nyimbo za kuisifu na kuipigia vigelele. Ujinga kama huu unapatikana Afrika peke yake na mifano iko wazi kabisa. Hakuna maelezo zaidi ya kwa nini ufisadi umekithiri na kushamiri zaidi ya watu kuwa wajinga.
 
Nasema kumekucha...Balali anataka kuwa Kamikaze wa Japan lazima afe na wake......
 
Sasa akishataja hayo majina ndo itakuwaje? Halafu kuna chochote atakachotaja ambacho hatukijui tayari? Mi naona wanazinguana tu
 
eti nilikuwa natumiwa? mpuuzi sana huyu na bora aje aseme ukweli tujue who/where is the money? akiwa mkweli wananchi tunaweza kumpa immunity maana atakuwa ametusaidia kuondoa mafisadi wengi sana
MNATUNGA SANA HABARI ZA MAFISADI LAKINA HAMKO CRITICAL NA WALA HAMNA DATA.NGOJA LEO NIWASAIDIE KUWAONYESHA NAMNA YA KUGUNDUA MAMBO.chukua gazeti la raia mwema la jana,angalia barua za zakhia kwa delloite,umeona barua ya kuwithdraw inafanana ref no na hio nyingine?maanake ni kuwa hio ya pili ni ya kuforge si kweli alikanusha anajisafisha.barua mbili tofauti hazifanani ref no ata siku moja
 

Mtanzania:
Hapana. Jambazi mwenye kujua mambo anaponaswa na polisi habwabwaji hovyo kwa vitisho; kwani anazijua haki zake, na huyo polisi kama ni polisi kweli atamsomea haki zake kuwa "Lolote utakalolisema litatumika katika mahakama kukupa kbano." Huyo jambazi anayo haki ya kutosema kitu bila kuwepo kwa mwanasheria wake.

Kwanza mafia wenyewe hata huko Napoli? wameshindikana, kwa kung'ang'ania biashara za taka kiasi kwamba mji mzima umekuwa mlima wa taka!

Kama ni kweli Ballali anataka kujisafisha, ama kuzama na walaji wenzie, njia iliyo bora kwake ni kushirikiana na watu kama akina Dr. Slaa, wenye uchungu na mali za walalahoi. Ballali anatakiwa atoe kila habari na kitu alichonacho kama ushahidi utakaowezesha kuwanasa mafisadi wote waliomo.
 
bt msiseme nawageuka wazee wangu
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…