BAKWATA tokeni hadharani kukomea dhuluma za watawala

BAKWATA tokeni hadharani kukomea dhuluma za watawala

ngara23

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2019
Posts
15,774
Reaction score
35,994
BAKWATA ni Moja kati ya taasisi kubwa ya kidini hapa nchini

Sijui jukumu lake ni kuangalia mwandam wa mwezi na kutangaza sikukuu ya Eid tu au kuchinja ngamia pale uwanja wa Biafra Kinondoni

Kuna dhulumu za watawala wanatenda Kwa wapinzani ikiwemo kubambikizia kesi watu za uhaini, kunyima katiba mpya, kutokuwepo Kwa tume huru ya uchaguzi n.k

Hizi ni dhuruma za haki za watu

Taasisi kama BAKWATA tulitegemea itoke ikemee machafu haya

Leo kanisa katoliki Tanzania wametoa ujumbe wa Pasaka na kukemea hayo machafu na dhuruma za haki za watu

Nashauri BAKWATA muige na msimamie haki na amani ya Taifa letu
 
Kua na Sheria zenye usawa, na Dora itumike ipasavyo, kwa wote na wananchi wachague Viongozi wanaowataka, pia kue Haki sawa kwa wote, Yaani Chama Tawala na Vyama vingine ktk Box la kupigia kura.
Pia pasiwepo na udanganyifu wa kwa Chama chochote.
Kwa Mimi Binafsi yangu sina Mpango wa kupiga kura hayo, ni maamuzi yangu.
Kupiga kula au kutokupiga kura sio Kosa kisheria.
 
Hakuna serikali inayoweza kuona chokochoko za kuhatarisha usalama wa nchi ikakaa kimya,Wakati cuf ilipokuwa na nguvu na kupelekea kina Lipumba kupigwa na kukamatwa mbona hukuhamasisha maaskofu wakemee? Tuiache jamhuri ifanye kazi yake.Hakuna mtu aliye juu ya Sheria,Viongozi wa dini waendelee kukemea tuache Zina, pombe na mambo mengine.
 
Hakuna serikali inayoweza kuona chokochoko za kuhatarisha usalama wa nchi ikakaa kimya,Wakati cuf ilipokuwa na nguvu na kupelekea kina Lipumba kupigwa na kukamatwa mbona hukuhamasisha maaskofu wakemee? Tuiache jamhuri ifanye kazi yake.Hakuna mtu aliye juu ya Sheria,Viongozi wa dini waendelee kukemea tuache Zina, pombe na mambo mengine.
Kwanini hutaki tume huru ya uchaguzi?
Kubambikizia kesi ndo amani
Kuiba Imani ya wananchi ndo amani?
 
BAKWATA ipi, hii ya kina mruma na kova? labda ile jumuiya ya kina ponda
 
Kuna jumuiya zingine za kidini zimekaa kichawachawa tu wala hazibweki kukemea uvunjifu wa haki. Zenyewe ni kuombeaombea dua tu, mara maombezi, hazioni uvunjifu wa haki za wananchi
 
Kwanini hutaki tume huru ya uchaguzi?
Kubambikizia kesi ndo amani
Kuiba Imani ya wananchi ndo amani?
Kila kitu kina taratibu,Huwezi ghafra unalazimisha jambo ambalo linahitaji muda, Hayo madai kwanini ushupaze shingo sasa? Na kwanini ni wewe tu wakati vyama vipo vingi? Mlikatazwa hata kufanya mikutano leo hii mnaranda Kila mahala hata hili huoni ni mabadiliko?
 
BAKWATA ni Moja kati ya taasisi kubwa ya kidini hapa nchini

Sijui jukumu lake ni kuangalia mwandam wa mwezi na kutangaza sikukuu ya Eid tu au kuchinja ngamia pale uwanja wa Biafra Kinondoni

Kuna dhulumu za watawala wanatenda Kwa wapinzani ikiwemo kubambikizia kesi watu za uhaini, kunyima katiba mpya, kutokuwepo Kwa tume huru ya uchaguzi n.k

Hizi ni dhuruma za haki za watu

Taasisi kama BAKWATA tulitegemea itoke ikemee machafu haya

Leo kanisa katoliki Tanzania wametoa ujumbe wa Pasaka na kukemea hayo machafu na dhuruma za haki za watu

Nashauri BAKWATA muige na msimamie haki na amani ya Taifa letu
Bakwata ni tawi la CCM, sasa kibaya zaidi Rais ni wa dini yao, hata akaua watanzania woote akabakiza waislamu, kwao Bakwata ni sawa tu!
 
Back
Top Bottom