BAKWATA iliundwa na nani?
Hebu Rudovic utoo pitia bakwata halafu tuletee taarifa yao ya mapato na matumizi

Ludovic Utoh hawezi kuwasogelea BAKWATA na kuwachunguza matumizi na mapato yao, kumesheheni madudu ambayo yakianikwa ni balaa tupu na kufuatiwa na vitisho.
 
Binafsi suala la BAKWATA hua linanitatiza. Najiuliza kama taasisi hii iliundwa na serikali kwa malengo yake kwa nini basi waislamu wasiunde taasisi nyingine nje ya hii ili iweze kusimamia maendeleo na ustawi wa waislamu. Hilo likifanikiwa tafsiri ya haraka ni BAKWATA kufifia kama sio kufa , lakini tukifungwa na historia hakuna kitakachofanyika.
 
Mi nitakuwa msomaji tuu.....Hivi FaizaFoxy ameanda wapi, sijamuona kitambo hapa jukwaani...Hii mada ina mfaa sana...
 
Last edited by a moderator:
Mi nitakuwa msomaji tuu.....Hivi FaizaFoxy ameanda wapi, sijamuona kitambo hapa jukwaani...Hii mada ina mfaa sana...

Nipo, mada nimeiona lakini kwanza nawasoma wachangiaji. Nijuavyo BAKWATA ilianzishwa na Nyerere alipoiuwa kwa makusudi EAMWS.

Ngoja nisome zaidi, ntarudi.
 
Nipo, mada nimeiona lakini kwanza nawasoma wachangiaji. Nijuavyo BAKWATA ilianzishwa na Nyerere alipoiuwa kwa makusudi EAMWS.

Ngoja nisome zaidi, ntarudi.

Kama iliundwa na Nyerere na mwenyewe alishatoka duniani kwanini iendelee na mambo yake yale yale.
 
Bakwata liundwa na waislam kwa msaada wa serikali.kwa sasa waislam wanataka waunde mahakama ya kadhi kwa masaada wa serikali.
 
tatizo bakwata hawataki uchaguzi ili waislam wapate fursa ya kumchagua kiongozi wanaemtaka,viongozi wote wa bakwata wapatikane kwa kupigwa kura hili ndo suluhisho la matatizo yote
 
nilikuta hii mahali..

[SIZE=+2]Tanga wamshangaa Mufti wa BAKWATA[/SIZE] BAADHI ya wakazi wa Manispaa ya Tanga mji anaotoka Mufti wa BAKWATA Sheikh Hemed bin Jumaa wameeleza kushtushwa kwao na kauli za Mufti huyo alizozitoa huko Shinyanga kwa Masheikh wa BAKWATA Juni 19, mwaka huu.
Katika kikao chake na Masheikh hao, Sheikh Hemed alinukuliwa pamoja na mambo mengine aliwaasa Waislamu kuacha kukatazana kuipigia kura CCM.
Alieleza pia kuwa Waislamu hawana uwezo wa kuongoza nchi na kwamba BAKWATA ni chombo kilichoanzishwa na hayati Mwalimu Nyerere baada ya kuvivunja vyombo vilivyokuwa vimeanzishwa na Waislamu.
Baadhi ya wakazi hao wamesema, walikuwa wakidhani kuwa BAKWATA ni chombo cha Waislamu lakini Mufti Hemed amewazindua kuwa chombo hicho ni cha serikali.
"Hivi Nyerere alianzisha BAKWATA kwa maslahi ya serikali au ya Waislamu na kwanini avivunje vyombo vilivyoanzishwa na Waislamu wenyewe na kuanzisha anachotaka yeye wakati yeye ni Mkristo?" alihoji Bw. Hamza Ali.
Naye Bw. Musa Bakari amsema, haelewi mantiki ya Mufti Hemed kuzunguka nchi nzima kuwaasa Waislamu wasikatazane kuipigia kura CCM wakati BAKWATA si chombo cha siasa.
"Tuna hisia kwamba Mufti anaitumikia serikali kwa vile ameshatuambia kuwa BAKWATA anayoiongoza ilianzishwa na Nyerere", amesema.
Amesema, kitendo cha BAKWATA kujiegemeza mno na serikali kiasi cha kuwakataza watu wasikatazane kuipigia kura CCM kunawafanya wawe na imani kuwa chombo hicho si chao.
Akizungumzia kauli ya Mufti Hemed kwamba Waislamu hawana uwezo wa kuongoza nchi, Bw. Ramadhani Omar kutoka wilaya ya Pangani amesema, amekerwa na kauli hiyo ambayo alidai ni ya kashfa kwa Waislamu.
"Kwani Ali Hassan Mwinyi aliyekuwa Rais wa Awamu ya Pili hakuwa Muislamu?" alihoji Bw. Omar na kumtaka Mufti Hemed aeleze ni kwa mtazamo upi anaona kuwa Waislamu hawawezi kuongoza nchi.
Bw. Omar aliongeza kudai kuwa Mufti Hemed anataka kuleta suala la udini wakati kinachogombwa kwa CCM si kuwa na Rais Mkristo bali ni sera mbovu zinazowakandamiza wananchi.
 
na hii ni nukuu kutoka mwandishi Mohamed Said....

[SIZE=+2]Kuvunjwa kwa jumuia ya EAMWS[/SIZE] HII ni sehemu ya nane ya mfululizo wa makala ambazo ni sehemu ya muswada wa kitabu "Mwalimu Julius K. Nyerere, Kanisa Katoliki na Uislamu: Dola na tatizo la Udini Tanzania" kitakachotoka hivi karibuni. Kitabu hicho kimeandikwa na mwandishi maarufu wa masuala ya historia hasa ya Tanganyika BWANA MOHAMMED SAID.
MKUTANO wa Iringa ulipitisha katiba ya jumuiya mpya ya Waislam, katiba ambayo ilikuwa sawasawa na katiba ya TANU. Hivi ndivyo BAKWATA ilivyoundwa.
BAKWATA ikamchagua Saleh Masasi, Muislam tajiri na ambae alikuwa kama mwenyekiti wa mkutano ule kuwa Mwenyekiti wa Taifa na Adam Nasibu akawa Katibu Msaidizi. Nafasi zote za juu katika BAKWATA kama ilivyotegemewa zilichukuliwa na kundi la Adam Nasibu, kundi ambalo toka mwanzo lilikuwa likidai kuvunjwa kwa EAMWS.
Uongozi wa BAKWATA uliomba serikali itambue jumuiya hiyo mara moja na ipige marufuku EAMWS kama jumuiya isiyo halali na mali zake zizuiwe. BAKWATA ilitoa maazimio kadha lakini azimio namba nne ndilo hasa linafaa kuelezwa. Azimio hilo liliomba serikali, TANU na ASP kuwatazama na kufanya uchunguzi wa kina kwa viongozi wote wa EAMWS, hasa Rais, Makamo wa Rais, Katibu wao na baadhi ya viongozi wa mikoa na wilaya ambao wana chuki na hii jumuiya mpya.[SUP]70[/SUP] Uongozi wa BAKWATA katika ushindi wao hawakutaka salama na mawaelewano na Waislam wenzao katika EAMWS wala kuwaonea huruma kama Uislam unavyofundisha, bali ulitaka chama na serikali uwaandame, hasa wale waliokuwa viongozi.
Baada ya kuundwa BAKWATA, ili kuondoa wasiwasi na kuwarudishia imani Waislam, Katibu wa Tume ya Waislam, Mussa Kwikima alitoa taarifa iliyosema:
Hakuna anaeweza kutishia kuwepo kwa EAMWS isipokuwa wanachama wake, sheria na serikali, lakini si watu binafsihata ikiwa mikoa yote kumi na saba ikijitoa haitamaananisha kuwa jumiya imekufa kwa kuwa kuwepo kwake hakutokani na kuwepo kwa mikoa hiyo kama wanachama isipokuwa kuwepo kwa wanachama wake, Waislam.[SUP]71[/SUP]
Wakati ilipotoka taarifa hii BAKWATA ilikuwa bado haijaandikishwa rasmi na Msajili wa Vyama. Kisheria ilikuwa haiwezekani kwa kundi la Adam Nasibu kuunda jumiya mpya iliyokuwa na malengo sawa na jumuiya ambayo tayari ishaandikishwa. Kwa muda wa siku tatu BAKWATA na EAMWS zikawepo kwa wakati mmoja. Ilionekana kama kwamba EAMWS itashinda vitimbi vya serikali na vya kundi la Adam Nasibu.
Tarehe 19 Desemba, 1968 serikali kama vile imegutushwa na taarifa ya Kwikima, iliipa BAKWATA Cerificate of Exemption na kuifungia EAMWS.[SUP]72[/SUP] Waziri wa Mambo ya Ndani Said Ali Maswanya kwa niaba ya serikali alitoa taarifa fupi:
Waziri wa Mambo ya Ndani kwa kuamriwa na Rais anatangaza kuwa tawi la Tanzania la East African Muslim Welfare Society na Baraza la Tanzania la la East African Muslim Welfare Society ni jumuiya zisizotambulika kisheria chini ya kifungu 6 (i) cha Sheria ya Vyama.[SUP]73[/SUP]
Kwa tangazo hilo la Rais wa Tanzania, Julus Nyerere, Waislam walinyimwa nafasi ya kukutana na kuzungumza kuhusu tatizo ambalo kwa kweli liliwahisu Waislam peke yao. Kwa ajili hii basi Waislam walinyimwa nafasi ya kujadili na kulitolea uamuzi tatizo hilo.
Viongozi wa EAMWS waliitwa mbele ya Kabidhi Wasii ambae ndiye alikuwa amekabidhiwa na serikali jukumu la kusimamia shughuli za kufunga rasmi shughuli za EAMWS. Viongozi walifahamishwa kuwa chini ya sheria ya vyama mali zote za EAMWS zitauzwa na madeni yatalipwa kutokana na fedha hizo na fedha zitakazobaki watapewa wanachama. Serikali ilikuwa haiwezi kufanya kama sheria ilivyokuwa imeelekeza. Ilikuwa jambo zito sana kwa serikali ya Nyerere kuonekana anasimamia kuuzwa kwa mali za Waislam. Viongozi wa EAMWS walipoitwa kwa Kabidhi Wasii mara ya pili walifahamishwa kuwa serikali imebadilisha mawazo yake kutekeleza amri kama sheria inavyosema kwa ajili hiyo basi imefanya mabadiliko ya sheria ya vyama ambayo yanaiwezesha sasa kutoa mali ya EAMWS na kukabidhi BAKWATA. Hivi ndivyo mali za EAMWS zilivyochukuliwa na kupewa BAKWATA bila ya ridhaa ya Waislam wenyewe. Hivi ndivyo shule zote zilizojengwa na EAMWS pamoja na mradi wa Chuo Kikuu cha Kiislam kilipoanguka katika mikono ya kundi la Adam Nasibu. BAKWATA haikuwa na uwezo wa kuendesha mipango yoyote na taratibu shule na miradi yote ya elimu ikafifia na mwishowe kufa kabisa. Hivi ndivyo halikadhalika moto wa Waislam uliowashwa kwa kupatikana kwa uhuru waliopigania hadi ukapatikana ulivyokufa. Moto huu ulikuja ukawaka tena, lakini hiki ni kisa kingine. Insha Allah Mwenyezi Mungu akipenda tutakuja kukieleza.
Huu ndiyo ukawa mwisho wa kile kilichokuwa kikijulikana kama mgogoro wa Waislam ulivyomalizika. Mgogoro ambao ulianza pale mwalimu wa shule ya msingi asiyefahamika na yeyote alipofanya maandamano katika mitaa ya Bukoba akimuunga mkono Julius Nyerere na Azimio lake la Arusha na ukaishia kwa mwalimu huyu akiwa na nafasi juu katika jumuiya ya Kiislam ambayo ilikuwa ikichukiza machoni mwa Waislam. Mwalimu huyu ambae sasa amekuwa Makamu Katibu Mkuu wa BAKWATA alianza kazi yake kwa kuwashutua Waislam. Katika mkutano wa waandishi wa habari Adam Nasibu aliiomba TANU na ASP kujikinga na watu wanaohujumu umoja wa nchi kupitia dini. Akaendelea na kusema kuwa BAKWATA ni sawa na Baraza la Kikristo la Tanzania. [SUP]74[/SUP] Kwa kuwa Waislam walinyimwa fursa ya kujadili "mgogoro' hivi sasa kilichobaki na dhana tu, kuwa nini kingelitokea endapo wangeliruhusiwa kufanya mkutano ule ulioitishwa na EAMWS. Waislam wa Bukoba ambao ilitaarifiwa kuwa walifanya maandamano kuunga mkono Azimio la Arusha hawakutayarisha maandamano ya kuunga mkono BAKWATA. Dar es Salaam na katika miji mingi ya Tanzania, neno BAKWATA halina tofauti na tusi. Kumuita Muislam kuwa yeye ni mwanachama wa BAKWATA ni sawa na kumuita Mkristo mfuasi wa Yuda Iscariot, aliyemsaliti Yesu kwa vipande thelathini vya fedha.
Mjumbe mmoja wa Tume ya Waislam inastahili kuelezwa habari zake - Mussa Kwikima. Mussa Kwikima mwaka 1968 alikuwa ameteuliwa kuwa jaji na Rais Nyerere. Yeye ndiye hasa alikuwa nguvu kuu katika tume ya Waislam. Wakati alipojitolea kuisaidia tume katika kupambana na kundi la Adam Nasibu, Waikela alimuonya kuhusu hatari ambayo itamkabili yeye mwenyewe binafsi na kazi yake. Kwikima alijibu kuwa umoja wa Waislam ni muhimu kuliko maslahi yake binafsi. Ilipoundwa BAKWATA na hapo kuwa ndiyo mwisho wa 'mgogoro', Kwikima alihamishwa kutoka Dar es Salaam na kupelekwa Mwanza kama Hakimu Mkazi na Rais Nyerere akamvua madaraka ya ujaji wake. [SUP]75[/SUP]
Kilichobakia baada ya kuvunjika kwa EAMWS ilikuwa ni kujaribu kuiweka BAKWATA katika mikoa kama jumuiya inayowakilisha Waislam wote wa Tanzania Bara. Mwaka mzima wa 1969 Adam Nasibu na kamati ya watu wanne walitembea katika mikoa wakiahidi msaada wa fedha kwa katibu yeyote wa zamani wa EAMWS ambae atashirikiana na BAKWATA makao makuu kuisaidia kufungua ofisi katika mkoa wake. Waislam waliipuuza BAKWATA.
Tabora ambayo haikujitoa katika EAMWS, serikali iliwaruhusu Adam Nasibu na kikundi chake kufanya mkutano wa hadhara. Kabla Adam Nasibu hajahutubia Waislam, Maulid Kivuruga mmoja wa wakongwe wa African Association na muasisi wa TANU Tabora, alipanda jukwaani kwa niaba ya Waislam wa Tabora na kuweka sharti kuwa Waislam watakuwa tayari kumsikiliza Adam Nasibu endapo Waikela mjumbe wa Tume ya Waislam iliyokuwa ikitafuta sulhu na yeye ataruhusiwa na serikali kuwahutubia Waislam ili aeleze upande wa pili wa kisa kile. Kivuruga alisema kuwa Waislam wanaomba sharti hili likubaliwe kwa sababu katika Uislam panapotokea mgogoro basi mpatanishi ni lazima asikilize pande zote mbili. Sharti hili lilikataliwa na BAKWATA na serikali. Palepale mbele ya waheshimiwa wa serikali na viongozi wa BAKWATA, Waislam wakaanza kuzomea huku wakitawanyika wakipiga takbir na wengine wakiitikia Allahu Akbar.
Siku chache baada ya tukio hili Waikela aliitwa na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Jinai kusailiwa kwa nini anaipinga BAKWATA. Wakiwa ndani ya chumba cha Tabora Hotel, Geoffrey Sawaya, Mkrugenzi wa C.I.D, alimpiga maswali Waikela na kutaka kujua kwa nini yeye hayuko tayari kushirikiana na serikali kuipa nguvu na kuieneza BAKWATA. Sawaya akatoa hongo ya shilingi elfu arobaini kwa Waikela ili asaidie kuimarisha BAKWATA. Waikela kama istizai alimuuliza Sawaya kama fedha zile zilikuwa zimetoka bait mal. Waikela alikataa kupokea hongo ile. Sawaya akamtisha lakini Waikela hakutishika. Waikela aliwekwa ndani ya chumba kile akiulizwa maswali kwa kiasi cha saa nne na kisha akaamrishwa kuweka sahihi yake katika makaratasi fulani. Hili alilifanya. Waikela hakufuatwa tena na serikali. Ingawa kulikuwepo na juhudi za chinichini za kuipinga BAKWATA, juhudi hizi hazikushinda kwa kuwa BAKWATA iliweza kufungua matawi yake nchi nzima pamoja na Tabora. Wapo baadhi ya viongozi ambao hawakuweza kuhimili vishawishi vya kupokea ile hongo ya serikali na kwa ajili hii walishirikiana na serikali hivyo kuwezesha ofisi za BAKWATA kufunguliwa, hata kama zipo pale kwa jina tu. Kuangushwa kwa EAMWS kulisababishwa na watu watatu ambao wao ndiyo walikuwa mstari wa mbele kabisa - Adam Nasibu, Sheikh Kassim Juma na Abdallah Chaurembo[SUP]76[/SUP] - na njama hii ikaungwa mkono na Rashid Kawawa na Abeid Amani Karume. Mkono wa Julius Nyerere na Kanisa Katoliki katika njama hii haukuonekana kabisa kama ilivyo kawaida katika njama zote za kupiga vita Uislam na Waislam Tanzania
 
ni ugomvi wa sadaka na vitega uchumi, nani aliwaambia waislamu wakitaka kumuabudu huyo allah lazima wawe na baraza
 
ni ugomvi wa sadaka na vitega uchumi, nani aliwaambia waislamu wakitaka kumuabudu huyo allah lazima wawe na baraza

kama jina lako....mada imeanzishwa kwa lengo zuri la kutaka kujua na kupata ukweli kuhusu BAKWATA ambayo imekua ndio chanzo kikubwa cha kuvunjika amani na kutoelewana waislam na serikali
wewe unakuja kutoa maneno ya kijinga..kama huna cha kuchangia funga domo lako chafu
 
kama jina lako....mada imeanzishwa kwa lengo zuri la kutaka kujua na kupata ukweli kuhusu BAKWATA ambayo imekua ndio chanzo kikubwa cha kuvunjika amani na kutoelewana waislam na serikali
wewe unakuja kutoa maneno ya kijinga..kama huna cha kuchangia funga domo lako chafu

ukweli ndio huo ni ubwabwa mbele wala sio ibada, kikubwa ni commercialization of islam kama unafikiri duniani kuna siku utaiona amani basi we ni chizi, ni kaburini tu ndiko kuliko na amani, zoea vurugu kama uko hai usiwe mwanamke mkubwa.
 
Mkuu Crabat,.

shukran kwa kulileta tena bandiko hilo,
nadhan tulishawahi lidiscuss humu ndani,
Pamoja sana
 
Back
Top Bottom