Bakuli la CCM Mtwara!!

Bakuli la CCM Mtwara!!

kweli dunia ina mambo,,,, ungeweka jina la huyo aliyeandikiwa hiyo barua ingekuwa poa sana

Hii barua ni Template, hivyo wahusika wanatembea na lundo la nakala. Wakikuona tu wanaandika jina lako au kampuni yako kwa mkono na kukukabidhi.

Iwayo yote makampuni na mashirika yote ya umma wamepewa barua hii!
 
Hii barua ni Template, hivyo wahusika wanatembea na lundo la nakala. Wakikuona tu wanaandika jina lako au kampuni yako kwa mkono na kukukabidhi.

Iwayo yote makampuni na mashirika yote ya umma wamepewa barua hii!

sio template mkuu,ililetwa ofisini kwetu na washapewa pesa,wamezigawa sana tu.
 
Khaa, milioni ishirini kumkaribisha katibu mkuu? Kwani yeye hana bajeti yake ya hiyo safari? Sasa anayeombwa huo mchango hapo ni nani? No wonder CCM imeshindwa kudeal na mafisadi, maana hao ndiyo wanaochangia safari za akina Nape na viongozi wengine kwenda mikoani. Lakini CHADEMA wakichangisha kwenye mikutano inakuwa nongwa.

Nape tuombe radhi kwa kuuponda utaratibu wetu wa kuomba michango kwenye mikutano ilihali ninyi mnawaomba mafisadi kwa njia ya barua.

wanaombwa wafanya biashara,makampuni na taasisi za umma na binafsi,almost ofisi zote za mji huu zimepokea hizo barua.
 
Hela zote za nini. Kwanini wasichangie kununua hata ya madawati ya watoto wanaokaa chini kuliko matumizi yasiyo na tija?

nini madawati,korosho zimedoda tu wakulima wana maisha magumu hadi wanauza akiba ya chakula ili waweze kumudu mahitaji mengine.soon mtasikia njaa kali mtwara hasa vijijini.
 
Kweli mazoea ni kilema!! Hivi mpaka sasa CCM bado tu hawajajua kuwa michango ni kati ya kero zinazowafanya watu waichukie CCM? Duu!

Mbona CDM na uchanga wake hawaombi michango kihivo?
 
inasikitisha wananchi hawana huduma za msingi kama shule, hospitali
afu chama klichoshiba chenye rasilimali tele bado wanataka kuwakamua hata kidogo walichonacho
imenikumbusha mfano wa tajiri aliepata mgeni akaaamua kuchukua ngombe wa maskini kumchinjia
wakati katika zizi lake kumejaa wanyama tele.(Ilimhusu Daud alieamua kumchukua mke wa askari wake)
CCM wanafanya the same thing
 
fikiria chama kilichokuja kukuomba kura kwa kauli mbiu ya maisha bora kwa kila mtanzania na ukakipa kura lakini baada ya maisha kukubana na kuwauliza wakakuambia maisha bora yatakuja kwa kufanya kazi ukakubali.
leo unalima korosho kwa jasho na kuuziwa pembejeo feki ambazo hazifiki kwa wakati na baada ya madhila yote hayo bei serikali hiyohiyo yachama hichohicho inapanga bei ambayo haikidhi mahitaji ya uzalishaji kinakuja kwako kwa safari ya ghafla na kukutaka kukichangia ili kuja kutoa matamko ambayo hayana tija.

maswali kwa kinana.
je angetolea hayon matamko dar ingekuwaje?
aliyepanga bei ya 1200 ni chadema?
je anahisi kuna kura ambazo chama chake hatujawapa na yuko kwenye kampeni ili tuwape?
 
limetembezwa kuanzia juzi.

KUMB. NA. MTR/CCM/V.10/VOL.
CHAMA CHA IVIAPINDUZI
SIMU NA. 2333076:0FISI KUU YA CCM MKOA - MTWARA: S.L.P. 180:
Barua zote zipelekwe kwa Katibu wa Mkoa:

YAH: YAH: MAOMBI YA MCHANGO ICUSAIDIA, KATIBU MICUU WA CCM TAREHE 21.11.2012

Tafadhali husika na somo hilo hapo juu.
Kutokana na ziara ya ghafla ya Katibu Mkuu na Msafara wake wa zaidi ya watu 17 tunaomba mchango wako wa fedha kusaidia gharama za mapokezi ya Viongozi hao zinazofikia Milioni Ishirini (Tshs.20,000,000/=).
Ni matumaini yetu wewe kama mdau mwenzetu wa maendeleo utatusaidia mchango wako huo.

" KIDUMU CHAMA CHA 1VIAPINDUZI "
( R. KNY: KAT M MKOA MKOA WA MTWARA.
19/11/2C'
 
Niliwahi kufanya kazi kampuni moja ya kigeni kule Mtwara, hawa wajinga wanakuja na mibarua yao yaani tena wanalazimisha kupewa hiyo michango, na sio mara moja yaani kila tukio likitokea wao na barua za kulazimisha michango. Wanaudhi sana makenge hawa.

Ndio maana nikakwambia hawa jamaa ndio zao. Hapa kwetu walipitisha mchango wa laki 7. Na tuwatengenezee shati aisee!!!
 
Kwani hao akina kinana hawakupewa per diem makao makuu?
 
" KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI "
19/11/2C \,
-------------~-~.~.~
.
CHAMA CHA MAPINDUZI

SIMU NA. 2333076:0FISI KUU YA CCM MKOA - MTWARA: S.L.P. 180:

Barna zote zipelekwe kwa Katibu wa Mkoa:

KUMB. NA. MTR/CCMIV.I0NOL:c
-
.

Tafadhali husika na somo hilo hapo juu.
Kutokana na ziara ya ghafla ya Katibu Mkuu na Msafara wake wa zaidi ya
watu 17 tunaombamchango 'wako wa fedha kusaidia gharama za mapokezi
ya Viongozi hao zinazofikia Milioni Ishirini (Tshs.20,OOO,OOOl-).
Ni matumaini yetu wewe kama mdau mwenzetu wa maendeleo utatusaidia
mchango wako huo.



( R.
KNY: KAT M MKOA
MKOA WAMTWARA.
 
KUMB. NA. MTR/CCM/V.10/VOL.
CHAMA CHA IVIAPINDUZI
SIMU NA. 2333076:0FISI KUU YA CCM MKOA - MTWARA: S.L.P. 180:
Barua zote zipelekwe kwa Katibu wa Mkoa:

YAH: YAH: MAOMBI YA MCHANGO ICUSAIDIA, KATIBU MICUU WA CCM TAREHE 21.11.2012

Tafadhali husika na somo hilo hapo juu.
Kutokana na ziara ya ghafla ya Katibu Mkuu na Msafara wake wa zaidi ya watu 17 tunaomba mchango wako wa fedha kusaidia gharama za mapokezi ya Viongozi hao zinazofikia Milioni Ishirini (Tshs.20,000,000/=).
Ni matumaini yetu wewe kama mdau mwenzetu wa maendeleo utatusaidia mchango wako huo.

" KIDUMU CHAMA CHA 1VIAPINDUZI "
( R. KNY: KAT M MKOA MKOA WA MTWARA.
19/11/2C'


Inawezekana na Polisi huwa wanalipwa
 
Barua hii ilikuwa inakwenda kwa nani au ni mtu yo yote yule anaweze kupewa? Na kwa mtindo huu ni rahisi pesa zikiishia mikono mwa wale walitumwa kupeleka barua hizo. Ndiyo namna ya wana CCM Mkoa na Wilaya kula alafu wanasema CCM ina wenyewe!
 
Ccm ni wahuni kweli hawa,jamani kila mtu aendelee kuhimiza hawa vijana ili mara mchakato wa Daftari la Kudumu la Wapiga kura likianza wajiandikishe kwa wingi huku mwishowa siku tulinde kura zetu mwanzo mwisho,siwapendi Ccm hata kidogo yani
 
Wazalendo wote tuimbeni wimbo huuu ccm ikifa mimi siwezi kulia kwani miaka hamsini taifa lango heri ya mkoloni
 
Back
Top Bottom