Bakhresa achangia bajeti $800k

Bakhresa achangia bajeti $800k

Ni kampuni ya SSB imechangia wizara ya uchukuzi USD800,000 ili mabehewa ya treni yatengenezwe.

Anastahili pongezi.

Source: TBC jana.

Kukarabati mabehewa hakuhakikishii kuwa mizigo itafika kule iendako iwapo reli pia haitatengenezwa!! Unaweza kuwa na mabehewa lakini kama erli haipitiki ni kazi bure and vice versa, hivyo basi sambamba na ukarabati wa mabehewa utengenezwaji wa reli pia ufanywe!!! Bakhressa hawezi kuwapa hizo pesa bure ni lazima amewakopesha ila watamlipa kwa kusafirisha mizigo yake kwa makubaliano maalum. Huyo ni mfanyabiashara sio charitable organization.
 
jamani tuwe makini na michango kama hii naona dk.Mwakyembe anapoteza umakini

Dk anaelekea kwenye kashfa nzito, kampni ya biashara kuchangia serikali nje ya mfumo wa kawaida wa mapato ya nchi ni rushwa, hapo kuna comflict of interest,

kama ni kutoa msaada waielekeze kwenye charity organization siyo siyo kuchangia kwa interest zao za kibiashara, bila (MOU)"memorandum of understanding" hiyo ni rushwa tu.

Muwe mnasoma bajeti vizuri na kuelewa Bakhera hajachangia hata kumi.. waziri kaeleza hivi NANUKUU
Napenda kuchukua fursa hii kuipongeza kwa dhati kampuni ya kitanzania ya S.S Bakhresa kwa kuitikia mpango huo na kutoa dola laki 8 ambazo zimetumika kukarabati vichwa 2 vya train aina ya 73xx. vichwa hivo vinatumika pamoja na kazi nyingine kusafirishia ngano kutoka DSM mpaka mwanza kwa ajili ya soko la S S Bakhresa la Uganda. vile vile kampuni ya TICTS ltd imeonesha nia ya kutoa kiasi hicho hicho cha fedh kukarabati vichwa 2 vya injine aina ya 64xx na mabehewa 20 kwa ajili ya kusafirishia makasha kutoka bandari ya dsm kwenda kituo cha makasha cha Ubungo
 
[Anatafuta misamaha ya kodi huyu maana ni nadra kwa mtu kufanya hivo bure[/QUOTE]

Kama anapewa msamaha au punguzo la kodi na kiasi anachozalishja analipa fadhira sioni tatizo hapo ni wangapi wanasamehewa kodi na hawafanyi hivyo....?

na hiyo ndiyo moja ya maana ya misamaha wa kodi..either utoe huduma kwa jamii au uuze bidhaa yako ka bei pungufu...!!
 
Hawa ndio huwa wana kurupuka tu. Hajui kua S.S.B imeongoza kwa miaka kadhaa kwa ulipaji wa kodi hapa Tanzania.
 
Heee, limeisha ingia suala la dini tena humu? Kazi kweli kweli, nadhani Bakheresa kachangia kama mfanya biashara na sio kama mwislam tena ili kurahisisha soko lake la kule Mwanza, dini inaingiaje hapa jamani!? Mh, Nyerere was right, "vi nchi vidogo na masiki kama hizi, ukiingiza udini na ukabila unasamba kwa kasi sana". By Mwl Nyerere 1995
 
loh! Sijui kafanywa nini asubuhi yote hii. Yaani kafunguka as if tuna mjadala wa hayo mambo yake. Tayari keshamporomoshea mitusi mango pickle halafu anajinadi eti ana dini.

Ana lake huyu wallah
akikuambia utumbo wake mwambie hivi '''''kumjibu mjinga yahitaji busara sana ujinga ni nusu ya mauti'''''
 
Anatafuta misamaha ya kodi huyu maana ni nadra kwa mtu kufanya hivo bure

Yes it is true that there is no free lunch...kama akipewa misamaha ya kodi na matunda ya misamaha kama hii tunayaona kwangu sioni tatizo ili mradi misaada ipitie channel zinazojulikana kisheria....na pia natumaini kuwa hadi waziri aseme publically imepitia channel hizo...!!

Kuna wanaosema eti bila MoU ni rushwa mbona tunayotangaziwa na kuonyeshwa kwenye TV wanaposaini MoU hawatuambiwi kwenye MoU wamesema au wamekubaliana nini...?
 
Serikali legelege haiwezi kukusanya Kodi.

By JK Nyerere
 
Mkuu kumbe Allah anatetewa kwa mitusi?

Mpuuzi huyu achana naye, Waislam nawajua na hawa vimeo nawajua. Wenye dini yao saa hizi wapo msikitini wanaswali leo ijumaa, hivi vimeo ni masalia ya utu wa kale wa mwanadamu. Mtu anaporomosha mitusi halafu anakwambia yeye Muislam. Ningemuelewa kama angeporomosha hiyo mitusi yake lakini asiihusishe na dini
 
Jamani hivi gharama ya kukarabati vichwa viwili unagharimu USD 800,000 (Tshs 1.2 billion equivalent)? Hata hivyo apongezwe tu. Hata kama wengine wakisema anataka msamaha wa kodi mbona wengi tu hawalipi kodi kabisa na hawachangii hata dawati la moja shule?
 
bidhaa zake kwenye soko ni pungufu kwa mfano juice ya box ya azam ni pungufu kwa sh 600|:kwa juice ya splash hilo ni punguzo linaloonyesha msamaha mkubwa wa kodi je ana bidhaa ngapi kwenye soko kwa hiyo huo sio msaada bali ni sehemu tu ya kodi yetu
 
Kachangia sawa kwanini katoa masharti zitengeneze vichwa vya treni ya kusafirisha shehena zake.angetoa mchango na kuwaachia wahusika waamue.hapo sijaona mchango,ila ni kwamba katoa malipo ya kusafirisha bidhaa zake huko mbeleni.ni km misaada ya wachina
 
Serikali ingeona msaada wake ktk bajeti haufai na unataka uinufaishe kampuni yake basi wasingeupokea.
 
Hizo ngano anazozisafirisha huwa zinalipiwa???
 
CCM oyeee!

Mada inahusu Salum Bakhresa kuchangia fedha kwa ajili ya ukarabati wa reli, hakuna mahala walikosema amechangia kwa sababu ya CCM acha kuota mchana. CCM unaipa hongera ya nini? Reli hiyo ilijengwa na mkoloni na tangu hapo iko mikononi mwa serikali ya CCM na ndiyo iliyoua reli hiyo. Wewe unawapa hongera ya kuiawa reli? au hongera ya kitu gani?

Wa kumpa hongera ni Bakhresa japo naye katazama mbali zaidi kwa sababu gharama ya kusafirisha bidhaa zake anazouza ndani na nje ya nchi ni kubwa sana akitumia barabara. Hivyo katoa msaada kwa manufaa au faida kubwa ya biashara zake lakini hapo hapo katusaidia na sisi walalahoi
 
Pia amejenga passenger terminal bandarini kuhudumia wasafiri wa zanzibar. Deserves credit.
 
tunashukuru ingawaje umepotoa ili kusafirisha bidhaa zako kama ungekuepo humu jamvini ningekuuliza je ni kweli hutoi msaada katika majanga yanayotokea humu nchini? au unatoa ila hutaki kutangazwa na wanahabari?
 
Kama ametoa kwa nia njema aongezewe... ila kama kuna hila ndani yake basi iwekwe wazi..
 
Mkuu MJIMPYA

Ni matumaini yangu hiyo donation inafanyakazi iliyokusudiwa,lakini pia kampuni ya S S Bakhresa itapata nafuu ya kodi na wakati huo huo itafaidika na mchango wake kwa kutumia miundombinu ya reli.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom