Bakhresa achangia bajeti $800k

Bakhresa achangia bajeti $800k

Anatafuta misamaha ya kodi huyu maana ni nadra kwa mtu kufanya hivo bure

Upo utaratibu wa kuwapunguzia kodi au msamaha kwa makapuni ambayo yanarudisha faida kwa jamii kwa maana ya kutoa misaada mikubwa!
 
muwe mnasoma bajeti vizuri na kuelewa bakhera hajachangia hata kumi.. Waziri kaeleza hivi nanukuu
napenda kuchukua fursa hii kuipongeza kwa dhati kampuni ya kitanzania ya s.s bakhresa kwa kuitikia mpango huo na kutoa dola laki 8 ambazo zimetumika kukarabati vichwa 2 vya train aina ya 73xx. Vichwa hivo vinatumika pamoja na kazi nyingine kusafirishia ngano kutoka dsm mpaka mwanza kwa ajili ya soko la s s bakhresa la uganda. Vile vile kampuni ya ticts ltd imeonesha nia ya kutoa kiasi hicho hicho cha fedh kukarabati vichwa 2 vya injine aina ya 64xx na mabehewa 20 kwa ajili ya kusafirishia makasha kutoka bandari ya dsm kwenda kituo cha makasha cha ubungo
hakuna tofauti yyte ni marekebisho madogo tu
 
Kwa akili yako wewe unaweza kuniambia nisome kitu muda huo tautoa wapi.

Hapa unapochangia muda umeutoa wapi? Sema umesoma umeona ujinga wako. Hiyo ndio CCM bwana, na amini nakuambia, udhalimu una mwisho.
 
Upo utaratibu wa kuwapunguzia kodi au msamaha kwa makapuni ambayo yanarudisha faida kwa jamii kwa maana ya kutoa misaada mikubwa!

hajachangia baeti ila katoa fedha kwa ajili ya kukarabati injini 1 na mabehewa kwa ajili ya kubebea ngano zake kutoka dsm kwenda mwanza kwa ajili ya soko lake la Uganda..
 
Kafanya vema kuirudishia jamii japo sehemu ya mavuno yake.
 
Ni kampuni ya SSB imechangia wizara ya uchukuzi USD800,000 ili mabehewa ya treni yatengenezwe.

Anastahili pongezi.

Source: TBC jana.

hell NO!

this is NOT correct and in fact UNETHICAL........what's the PPP model for then?
 
Anatafuta misamaha ya kodi huyu maana ni nadra kwa mtu kufanya hivo bure
Yawezekana uko sahihi, lakini kama ukifika pale Isaka (Bandari ya Nchi kavu) na kuona hali halisi na performance ya hiyo bandari na jinsi huyu jamaa alivyo na nia ya kuona reli hii inakuwa imara naamini utakuja ku-edit post yako
 
Sawa....lakini kuna ulazima wa kuandika kutumia dola? sisi hatuna pesa? ukiaandikwa kama Tshs..itapungua?.....
 
Kudadeki hii ndio bongo. Mtu kama huyo Mwana Mtoka Pabaya anatoka mipovu na miharo ka chemba bovu kisa hela katoa bakhresa,angetoa mengi ungeanza kumsifia.we unachangia nini nchii hii zaidi ya ushuzi,hongera BAKHRESSA
 
Last edited by a moderator:
Bakharesa = NMC,Bakharesa anatumia majengo na mitambo ya NMC ambayo ilikuwa chini ya serikali,fedha za ununuzi alilipa lini?na kama bado... Alipaswa kuilipa serikali kwa matumizi ya majengo na mitambo,Je serikali inapata faida gani kwake kwa mfumo wa Dividend au return yoyote kwa matumizi haya?.
Swali la msingi kwa msaada huu ambao ameipa serikali binafsi naona kama ni kuifunga mikono na mdomo,je kwa msingi huu serikali itatoa wapi msuli wa kumkemea au kumdhibiti pale atakapo kwenda kinyume?under good governance alipaswa kuwekeza kwenye Government Private Partnership ambapo serikali ingekuwa na Full Control.bado tukumbuke amlipaye mpiga zumari ndiye apigiwaye wimbo aupendao.... Alilofanya halina tofauti na tunalopigia kelele kwa nchi za magharibi walau moja tu ni kwamba yeye hata hamisha na atawekeza hapa nchini.
 
hajachangia baeti ila katoa fedha kwa ajili ya kukarabati injini 1 na mabehewa kwa ajili ya kubebea ngano zake kutoka dsm kwenda mwanza kwa ajili ya soko lake la Uganda..

Anaendelea kutimiza jukumu lake kama serikali, kwani serikali ni mimi na wewe!
 
Muwe mnasoma bajeti vizuri na kuelewa Bakhera hajachangia hata kumi.. waziri kaeleza hivi NANUKUU
Napenda kuchukua fursa hii kuipongeza kwa dhati kampuni ya kitanzania ya S.S Bakhresa kwa kuitikia mpango huo na kutoa dola laki 8 ambazo zimetumika kukarabati vichwa 2 vya train aina ya 73xx. vichwa hivo vinatumika pamoja na kazi nyingine kusafirishia ngano kutoka DSM mpaka mwanza kwa ajili ya soko la S S Bakhresa la Uganda. vile vile kampuni ya TICTS ltd imeonesha nia ya kutoa kiasi hicho hicho cha fedh kukarabati vichwa 2 vya injine aina ya 64xx na mabehewa 20 kwa ajili ya kusafirishia makasha kutoka bandari ya dsm kwenda kituo cha makasha cha Ubungo
Twashukuru kwa kuliweka sawa hili ili watu wajue why alitoa izo ela it was purely kuboost mzigo wake uende no wonder mzigo ukasafiri bure for sometimes ili kufidia izo ela.
No free lunch wajameni.
Ingawa hii inaweza kuwa pia ni rushwa ili apitishwe kwende Tender kama mwekezaji katika harakati za kubinafsisha huduma za reli inchini.
Na pia awe anawajari wafanyakazi wake mtu kibarua for years as if sheria ya ajira haifahamu!
 
wewe umesoma wapi??, ni product ya shule za kata nini?

mtu mmoja kuchangia bajeti? alafu unashangilia kama zuzu,

zipo taratibu za kichumi za kuchangia bajeti kwa kila mwananchi, kampuni mashirika na taasisi mbali mbali kupitia kodi, nje ya mfumo huu ni vurugu, rushwa na kutokuwajibika kwa serikali. kukusanya kodi

hivi? akichangia bajeti? tutamdai vipi kodi yetu??, je? kama amechangia atalipa kodi stahiki? na je? kama alichokichangia ni pungufu au zaidi ya kodi hesabu zitakaa vipi?

Ni kampuni ya SSB imechangia wizara ya uchukuzi USD800,000 ili mabehewa ya treni yatengenezwe.

Anastahili pongezi.

Source: TBC jana.
 
Ni kampuni ya SSB imechangia wizara ya uchukuzi USD800,000 ili mabehewa ya treni yatengenezwe.

Anastahili pongezi.

Source: TBC jana.

Wakuu,
Huo ni mwanzo mzuri na wengine watafuata... WaTanzania tuwe na moyo riadha na moyo wa kutoa (kujitolea) siyo kuweka Dhana mbovu na kupakizia, Mtu kama huwezi kupongeza au kusifu au hata kuComment mazuri basi bora
mezea tu na utuliye..... jamani kutoa msaada ni MOYO siyo !! ( kwa chochote) huo ni uzalendo na encouragment ili azidi kutoa siku zi jazo. " kila mTanzania aweza toa hata kwa Maneno mema pia ni Sadaka. inakubalika
shukraan SSB tafadhali kesho ukipata nafasi toa tena..plz come again. Good luck na mungu akuengezee.
 
Hata Tembo akonde vipi, hawezi kumfikia Sungura!
 
Anatafuta misamaha ya kodi huyu maana ni nadra kwa mtu kufanya hivo bure

Ubishi tu ndio mliojaliwa nao! sasa hilo la misamaha ya kodi umelipata wapi? acheni kuishi kwa hisia na kupiga ramli!
 
Bora apewe kwani moja ya Kampuni yake (Azam) ndio inayosafirisha Bidhaa za ngano katika Reli ya kati kuliko mizigo yeote kwani mpaka ana behewa zake.
Ni vizuri akapewa na Usafiri wa treni katika Jiji la DSM
 
Back
Top Bottom