jmushi1
Platinum Member
- Nov 2, 2007
- 24,989
- 22,521
Uliambiwa na nani kuwa kama mtu ukiwa upinzani huwezi kusema mazuri ambayo yanafanywa na wana ccm? Wewe unadhani bila ya wana ccm hii miziki yote iliyowekwa humu jamvini ilivujishwa na nani toka serikalini.
Mimi kama kuna mtu anafanya kazi nzuri Tanzania atapata support yangu hapa hata kama mtu huyo ni mwanaccm. Wapinzani wengi wako nje ya serikali na hawawezi kupata kila kitu kinachoendelea huko.
Kumbuka kuwa hapa hatupiganii vyama mkuu bali masilahi ya nchi yetu. Mtu yeyote anayepigania masilahi ya nchi yetu anapata support hapa JF kama kawa - awe mpinzani au mwana ccm.
Wajitokeze na waondoke huko!
HAKUFAI TENA...WESHAROGWA!
Mama alikuwa akipiga kelele kweli..Lakini ukisikiliza kwa makini unakuja kugundua kuwa ETI ANATAKA PESA ZA EPA ZIRUDISHWE!
PESA ZISHARUDISHWA TENA LABDA ZOTE NA NDIO MAANA WALIFANYA SIRI KUTOWEKA HADHARANI IN DETAILS!
HAKUKUWA NA JIPYA ALILOSEMA MAMA WA WATU ALIYETOKEA KWENYE VYOMBO VYA HABARI AKIONGEA KWA MACHUNGU HUKU ANACHOSEMA NI TOFAUTI!
KWANZA SERIKALI ISHAZITAKASA NA HIVYO KUWATAKASA WATUHUMIWA!
ALICHOTAKIWA MAMA KUSEMA NI....YES CCM TUNA TATIZO LA UFISADI NA WALIOMO WACHAFU WATOLEWE WAFIKISHWE KWENYE MKONO WA SHERIA!