Bajeti ya harusi

wimbi la mbele

JF-Expert Member
Jan 4, 2011
647
266
hivi sasa hivi standard bajet ya harusi ambayo si kubwa na modest ni kiasi gani?

naomba mchakato tafadhali
 
Dah swali general sana.........labda tufanye hivi!!

1. Ukumbi Unadhani iwe Ukumbi upi? Mji gani?
Au kama ni gArden
2. Pombe inahusika au ni ya Ki -SDA?
3. Magari ya Maharusi unakodi au? na aina gani?
4. Una plan wageni wangapi?
5. ...........
6..........
 
naombea nikipata wangu basi tusiwaingieze au nisimuingize gharama,tutafunga kanisani tutarudi nyumbani na kulala baaasi
 
naombea nikipata wangu basi tusiwaingieze au nisimuingize gharama,tutafunga kanisani tutarudi nyumbani na kulala baaasi

duh manake mtaenda kubarikiwa na 'baba padiri',kwisha kazi!sisemi ushereheshe kwa 50M,lakini siku muhimu kama hii bibiye walau ungejitahidi hata wajomba na mashangazi wapate soda moja moja basi!
 
Kama unadhani kuna ugumu sana, ita washiriki wachache na mchoma ubani, then andaa unga wa ngano kilo mbili choma maandazi na kisha anzisha familia
 
Ndugu ya Harusi ni nzuri sana ..na pia najua uko excited sana... Lakini kama atatokea mtu na kuniambia nirudie tena harusi yangu..nitafanya kila njia niepuke gharama na pia nikubali lawama, kashfa na kila kitu kwa manufaa ya baadaye ya familia yangu.

Unless otherwise, uchumi wako uko imara sana, au umezungukwa na mtandao wa mafisadi ambao wako tayari choma moto hela ambazo hawana uchungu nazo ..Please go with my advice..hebu fikiri ..miaka kumi ijayo unaweza kuwa na familia, watoto watataenda shule n.k. Kwa nini hizo hela usizifanyie namna..

Ningekushauri kuwa fanya harusi ya bei ya chee sana kama symbolic, utamaduni au kuwa karibu na familia & marafiki.. na sio lazima uamishe ukoo mzima toka kule kwenu..kwa watani zangu.....yaani..kikubwa ni ukumbi wa bei rahisi, kama unayo plot ushwahilini weka tent ...vyakula vya kawaida na madoido ya kawaida....yaani kwa fanya harusi ya kichovu kwa lugha nyingine... kwangu mimi maximum ningeweka less than 5 million..au chini ya hapo kutegemea wigo wa watu wanaokuzunguka.. lakini kumbuka si lazima kumwalika kila mtu..

Najua kuwa watu watachonga sana eti ..lazima nichangiwe..kama mimi niliwachangia watu..si lazima wao wanichangie.. nitawapa mwaliko at vey short notice kama symbolic ili wanichangie kidogo..sina haja ya kuwaumiza na ugumu huu wa maisha..kikubwa waje kwanye hivyo vikao visivyozidi 4..sitampa ndugu yangu yeyote au rafiki haiki na jukumu la kuburuta vikao viwe virefu ili watu wanywe sana na wachangie sana uchakavu..vikao vifupi na maana yake ni just kuwa pamoja kimawazo, symbolic na kuonyesha nawajali ndugu na jamaa.. muda uliobaki waendelee na shughuli zaooo na walee familia zao..

Anyway.. in short napinga sana matumizi makubwa ya harusi kwa watanzania wasio mafisadi kwa kisingizio eti,,jamii haitanielewa ..wakati jamii yenyewe yetu Watanzania , ndugu, jamaa ni wachovu na masikini kama walivyo asilimia kubwa ya watanzania..kumbuka wewe Bwana Harusi na wife wako mtarajia ndio waamuzi..na ndio mtakao face reality baadaye...hata yeye aepuke hizo Vikitchen party vya gharama,...Najua watu wanaweza piga lakini ..wakitaka sherehe wasitumie kizingizio cha harusi yenu...kumbuka nyinyi maharusi mnaweza amua kufunga harusi basi kama wanataka sherehe wafanye bila wewe..

Anyway, Najua hapa kuna wana JF watao argue..lakini kumbuka hayo ni mawazo yangu..labda kwa sababu mimi ni zumbukuku..
 
Ndugu ya Harusi ni nzuri sana ..na pia najua uko excited sana... Lakini kama atatokea mtu na kuniambia nirudie tena harusi yangu..nitafanya kila njia niepuke gharama na pia nikubali lawama, kashfa na kila kitu kwa manufaa ya baadaye ya familia yangu.

Unless otherwise, uchumi wako uko imara sana, au umezungukwa na mtandao wa mafisadi ambao wako tayari choma moto hela ambazo hawana uchungu nazo ..Please go with my advice..hebu fikiri ..miaka kumi ijayo unaweza kuwa na familia, watoto watataenda shule n.k. Kwa nini hizo hela usizifanyie namna..

Ningekushauri kuwa fanya harusi ya bei ya chee sana kama symbolic, utamaduni au kuwa karibu na familia & marafiki.. na sio lazima uamishe ukoo mzima toka kule kwenu..kwa watani zangu.....yaani..kikubwa ni ukumbi wa bei rahisi, kama unayo plot ushwahilini weka tent ...vyakula vya kawaida na madoido ya kawaida....yaani kwa fanya harusi ya kichovu kwa lugha nyingine... kwangu mimi maximum ningeweka less than 5 million..au chini ya hapo kutegemea wigo wa watu wanaokuzunguka.. lakini kumbuka si lazima kumwalika kila mtu..

Najua kuwa watu watachonga sana eti ..lazima nichangiwe..kama mimi niliwachangia watu..si lazima wao wanichangie.. nitawapa mwaliko at vey short notice kama symbolic ili wanichangie kidogo..sina haja ya kuwaumiza na ugumu huu wa maisha..kikubwa waje kwanye hivyo vikao visivyozidi 4..sitampa ndugu yangu yeyote au rafiki haiki na jukumu la kuburuta vikao viwe virefu ili watu wanywe sana na wachangie sana uchakavu..vikao vifupi na maana yake ni just kuwa pamoja kimawazo, symbolic na kuonyesha nawajali ndugu na jamaa.. muda uliobaki waendelee na shughuli zaooo na walee familia zao..

Anyway.. in short napinga sana matumizi makubwa ya harusi kwa watanzania wasio mafisadi kwa kisingizio eti,,jamii haitanielewa ..wakati jamii yenyewe yetu Watanzania , ndugu, jamaa ni wachovu na masikini kama walivyo asilimia kubwa ya watanzania..kumbuka wewe Bwana Harusi na wife wako mtarajia ndio waamuzi..na ndio mtakao face reality baadaye...hata yeye aepuke hizo Vikitchen party vya gharama,...Najua watu wanaweza piga lakini ..wakitaka sherehe wasitumie kizingizio cha harusi yenu...kumbuka nyinyi maharusi mnaweza amua kufunga harusi basi kama wanataka sherehe wafanye bila wewe..

Anyway, Najua hapa kuna wana JF watao argue..lakini kumbuka hayo ni mawazo yangu..labda kwa sababu mimi ni zumbukuku..

Natamani nikuoni nikupe tano kabisa! Kuna ndugu yangu yeye anafanya harusi, unaambiwa bajeti eti milioni 17!! Mtu ukimuuliza mshahara wake, hata kama unafika mil 1 kwa mwezi, hii sio pesa anayoweza kutengeneza kwa mwaka au hata miaka miwili. Unajua kwa mfano sisi tulio nje, harusi unaweza kukuta ni $10,000 to $20,000. Ni ghali ukifikiria kwa pesa za Tanzania. Lakini kumbuka kwa mwaka nina mshahara usiopungua $60,000. Kwa hiyo hiyo harusi ipo ndani ya bejeti yangu. Isitoshe, huku naweza kuchukua mkopo benki kirahisi nikalipa taratibu, kitu ambacho hakipo bongo, au ni kigumu kweli.
Harusi bongo zimekuwa blown out of proportion kabisa. Ni aibu kwa mtu wa mshahara wa laki kadhaa kufanya harusi ya mamilioni! It simply doesnt add up!!! Nadhani tuna mentality ya kuwa tegemezi. Bajeti yangu isipotosha, nitaongezewa na ndugu. Hivi hivi ndio maana hata bajeti ya serikali inategemea donors. Maana wanaweka expenses wasizoweza kuzimudu wao binafsi! UJINGA!!
 
Vitu vya msingi ni

  1. Usafiri
  2. Ukumbi
  3. Chakula
  4. Vinywaji
  5. MC/MUSIC/VIDEO
Gharama ya hivyo vitu vinategemea na harusi unayotaka kuifunga ni ya kiwango gani na idadi ya watu watakaohudhuria
 
Ukumbi 500,000/=
chakula na keki na champagne 2,000,000/=
vinywaji 2,000,000/=
mc & music 400'000/=
video camera & steel picture 400'000/=
Transpot 300,000/=

Total 5,600,000/=

Harusi ikizidi pesa hiyo basi wakati wewe unakwenda honey moon na mwenyekiti wa kamati ya harusi ujuwe anakwenda showroom kununuwa gari lake kutokana na michango ya harusi yako. kila kila kitu hapo wanakidoubble price.
N:b, Hiyo ni bajeti ya harusi ya wageni 400.
Anaebisha hilo basi na yeye ni mmoja wa wanufaika wa wizi wa michango ya Harusi, vitu sio vigumu kivile ila watu wanaweka maslahi sana.
 
Kanisani inafungwa BURE !!

Gharama zingine unajitakia mwenyewe.
Wewe yako umefanya bure maana usiongee tu kuongeza muda
Ukumbi 500,000/=
chakula na keki na champagne 2,000,000/=
vinywaji 2,000,000/=
mc & music 400'000/=
video camera & steel picture 400'000/=
Transpot 300,000/=

Total 5,600,000/=

Harusi ikizidi pesa hiyo basi wakati wewe unakwenda honey moon na mwenyekiti wa kamati ya harusi ujuwe anakwenda showroom kununuwa gari lake kutokana na michango ya harusi yako. kila kila kitu hapo wanakidoubble price.
N:b, Hiyo ni bajeti ya harusi ya wageni 400.
Anaebisha hilo basi na yeye ni mmoja wa wanufaika wa wizi wa michango ya Harusi, vitu sio vigumu kivile ila watu wanaweka maslahi sana.
 
Back
Top Bottom