Bajeti ya harusi ya gharama ndogo

Bajeti ya harusi ya gharama ndogo

Katika harusi yangu nilifanya hivi, nilifanya 201O ilikua hivi

1.Budget haikuzidi milioni 4, nyingi zilienda kwenye chakula
2.Sikutoa kadi hata moja ya mchango
2. niliamua iwe casual, kwa hiyo sikuhangaika kutauta profesional MCs, badala ya kuchangisha afu kumlipa MC, tulitengeneza ratiba kisha marafiki zangu wachache, wakasaidia kusema chochote kwa kupokezana.
3. Badala ya kuchanga pesa kukodi magari, tulitumia magari ya friends, niliomba rafiki zangu wengine wachukue maids, mwingine bibi harusi, mwingine mama mkwe..kwa gari zetu hizi hizi za kawaida.

One of the BEST! BESTER! BESTEST! advice ever!
I salute you!
Igweeeeeeee!!!!
 
labda isiwe na kamati...maana wanakamati tu watataka kujilipa
 
1.Ukumbi=1,000,000

2.Mapambo=1,000,000

3.Vinywaji bia 3@=330,000

4.Chakula plate 12000=600,000

Mc & Music=600,000

Magari-
Wazazi pande zote mbili=300,000

Gari-Maharusi=400,000

Coaster(Waalikwa)=
150,000.

Jumla kuu=4,380,000
Balance=620,000(Dharura)
NAWATAKIA MAANDALIZI MEMA.

Big up mkubwa.... Nimeipenda. naiweka sehemu kwa matumizi ya baadae.
 
Ushauri mzuri. Kingine Ni gaharama isiyo ya msingi ya keki na mapambo. Weka ndafu hata 2 ama 3, watu watakula nyama na kufurahi. Weka chakula na vinywaji. Wekeza kwenye mziki lakini achana na mc.


King'asti, na sisi wasema chochote tukale wapi jamani mkiwa mnatutenga hivyo.
 
Last edited by a moderator:
Daaah nlisahau hela ya keki, sasa tusiivuruge hela ya dharura; twende tuvunje pale kwenye gari ya naharusi, chanja laki mbili hapo afu tuitupie kwenye cake.
 
1.Ukumbi=1,000,000

2.Mapambo=1,000,000

3.Vinywaji bia 3@=330,000

4.Chakula plate 12000=600,000

5.Mc & Music=600,000

6.Magari-
Wazazi pande zote mbili=300,000

7.Gari-Maharusi=400,000

8.Coaster(Waalikwa)=
150,000.

Daaah nlisahau hela ya keki, sasa tusiivuruge hela ya dharura; twende tuvunje pale kwenye gari ya Maharusi, chanja 200,000 hapo afu tuitupie kwenye cake, ibaki 200,000 Gari safi na simple

Jumla kuu=4,380,000
Balance=620,000(Dharura)
NAWATAKIA MAANDALIZI MEMA.
 
Wewe una watu 50 and 5,000,000 hemu study the numbers above an stop asking stupid questions hapa! Find a peace of paper and do the budget! Kama unakaa Biharamulo nitakupa ushauri wakati gharama za vitu na maeneo ni tofauti? Kwa kweli kutumia 5M kwenye harusi ya watu 50 ni kukosa focus! Make it simple and use only 2m na umpe bwana mdogo 3m zikamsaidie huko mbele

Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums
 
Tena mawazo...jiandae mkuu..!!

kwani ndoa za kiserikali hazipo?...

mkishasaini tu ruksa kuanza maisha kama mume na mke... mahari angalau 60% is substantial
 
Mkuu!
Gharama ya harusi inategemea mahali ulipo na namna gani hiyo harusi ifanyike.
Kumbuka kwa mtu aliyeko sinza - Dar anafunga harusi kwa gharama tofauti na mtu aliyeko kijiji cha Mkili kule Ruvuma au Buswelu - mwanza.
Mimi niliwahi kuandaa harusi ya ndugu yangu tukialika watu 120 + watoto 30 na ilifana sana kwa gharama ya M3.2 tu lakini ni maeneo ya pale songea mjini.
Hebu tanabaisha uko wapi wewe nikupe mchanganuo wa harusi ya 5M.
 
Habari za leo wana JF. Mdogo wangu anatarajia kufunga ndoa mwaka huu mwezi wa sita mwishoni. Mimi ndio kaka yake na mimi ndio msimamizi wake. Ninataka nimsaidie aweze kufanya harusi kwa gharama ndogo kwa kadri iwezekanavyo. Idadi ya watu watakao alikwa ni hamsini. Ninataka gharama ya harusi iwe shilingi Milioni Tano. Kwa walio na uzoefu na suala hili, mnadhani kwa bajeti hiyo hapo na kwa idadi hiyo ya watu, inaweza kufanyika sherehe ya harusi ambayo itapendeza? Na je inaweza kutumika chini ya gharama hiyo hapo juu?

Ninaomba maoni na ushauri wenu please.

Kaka mimi nilishawahi kualikwa kwenye harusi ya Ki-Ghana, hawa jamaa wapo simple balaa.

Baada ya ndoa pale kanisani mnakusanyika nje ya kanisa, mnapewa bites na vinywaji halafu mnaachana.

Hakuna complications.
 
Kaka mimi nilishawahi kualikwa kwenye harusi ya Ki-Ghana, hawa jamaa wapo simple balaa.

Baada ya ndoa pale kanisani mnakusanyika nje ya kanisa, mnapewa bites na vinywaji halafu mnaachana.

Hakuna complications.

..humpati wa hivyo hapa...
 
Back
Top Bottom