ERoni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2013
- 52,498
- 119,304
Mkuu milioni tano kwa harusi ya kualika watu 50 inatosha sana na hela ingine inabaki!
Tunaomba mchanganuo wa hiyo mil.5. Ukumbi, mapambo, chakula, usafiri, na mengineyo!!
Mkuu milioni tano kwa harusi ya kualika watu 50 inatosha sana na hela ingine inabaki!
Wewe ni Muongo!
Katika harusi yangu nilifanya hivi, nilifanya 201O ilikua hivi
1.Budget haikuzidi milioni 4, nyingi zilienda kwenye chakula
2.Sikutoa kadi hata moja ya mchango
2. niliamua iwe casual, kwa hiyo sikuhangaika kutauta profesional MCs, badala ya kuchangisha afu kumlipa MC, tulitengeneza ratiba kisha marafiki zangu wachache, wakasaidia kusema chochote kwa kupokezana.
3. Badala ya kuchanga pesa kukodi magari, tulitumia magari ya friends, niliomba rafiki zangu wengine wachukue maids, mwingine bibi harusi, mwingine mama mkwe..kwa gari zetu hizi hizi za kawaida.
Acha kumwingiza mwenzio kwenye matatizo. Kwa ukumbi huo na idadi hiyo ya watu andaa pesa isiyopungua milioni 12Mkuu, hiyo hela inatosha kufanya harusi kubwa sana ya watu 120 hadi 150. Kuna harusi ilifanyika 22.02.2014 jamaa walitumia 9.2million harusi ya watu around 300 ilikua bomba balaa. tulikunywa na kula nyama mwanzo mwisho na kamati yao ikatoa zawadi fedha taslim 1.270m kama zawadi. Mimi mwenyewe nilikua impressed sana maana nategemea kufunga ndoa mwaka huu na niliambiwa ukionanan na wenye ukumbi wanaweza kukupangia kila kitu. Ukumbi wenyewe Princess hall Sinza.
Tunaomba mchanganuo wa hiyo mil.5. Ukumbi, mapambo, chakula, usafiri, na mengineyo!!
Mkuu usikremu, ili kutoa mchanganuo rasmi, ni lazima jamaa adisclose baadhi ya vitu, wapi anaishi, kuna umbali gani na hotel or ukumbi atakaochukua, cost za hotel or ukumbi uliokusudiwa ni upi nk, nk!
...
Akidisclose yote haya naweza kumpigia hesabu na kumuekea na dots!
...
General overview milioni tano inatosha na kubaki!
Kwa mfano:
hoteli= mill 1
chakula= laki 5
Usafiri na malazi ya wageni= mill 1 na nusu
na hiyo mill 2 iliyobaki kwa vikorombwezo vingine!
...
Usifanye mchezo na mill 5 kwa watu 50 wewe!
Hiyo hela ni kubwa sana!
Mkuu usikremu, ili kutoa mchanganuo rasmi, ni lazima jamaa adisclose baadhi ya vitu, wapi anaishi, kuna umbali gani na hotel or ukumbi atakaochukua, cost za hotel or ukumbi uliokusudiwa ni upi nk, nk!
...
Akidisclose yote haya naweza kumpigia hesabu na kumuekea na dots!
...
General overview milioni tano inatosha na kubaki!
Kwa mfano:
hoteli= mill 1
chakula= laki 5
Usafiri na malazi ya wageni= mill 1 na nusu
na hiyo mill 2 iliyobaki kwa vikorombwezo vingine!
...
Usifanye mchezo na mill 5 kwa watu 50 wewe!
Hiyo hela ni kubwa sana!
Habari za leo wana JF. Mdogo wangu anatarajia kufunga ndoa mwaka huu mwezi wa sita mwishoni. Mimi ndio kaka yake na mimi ndio msimamizi wake. Ninataka nimsaidie aweze kufanya harusi kwa gharama ndogo kwa kadri iwezekanavyo. Idadi ya watu watakao alikwa ni hamsini. Ninataka gharama ya harusi iwe shilingi Milioni Tano. Kwa walio na uzoefu na suala hili, mnadhani kwa bajeti hiyo hapo na kwa idadi hiyo ya watu, inaweza kufanyika sherehe ya harusi ambayo itapendeza? Na je inaweza kutumika chini ya gharama hiyo hapo juu?
Ninaomba maoni na ushauri wenu please.
Usafiri na malazi ya wageni?! Kwa nini uwalipie wewe hoteli? SI wafikie kwa mabinamu zao?
Wewe ni Muongo!