Huyu Mdada Bukuku namjua vizuri sana, kipindi anakaa kinondoni Mkwajuni , niliwahi kwenda nyumbani kwake alikuwa hapendi ndugu wala marafiki wa mme wake. aliwafukuza shemeji zake wote wote, akiwasingizia eti wanamtaka ,jamani !!! ,Baadaye wakahamia kijito nyama, karibu na shule ya Masijidi Ghuba. pale alikimbia familia yake kutokana na Choyo aliyokuwa nayo. " JE utamtambuaje Mtu aliyeokoka"? Mme wake aliwachukua Wadogo zake akaanza kuishi nao. Hana lolote huyu
Inaonekana unaagenda yako ya siri juu ya kutaka kumchafua Bahati Bukuku, sio vizuri kila mtu ana mapungufu yake, kwa kawaida katika ndoa mwanamke ndiye anayeonekana mdhambi hata kama mwanaume ndiyo mbaya, mfano, katika ndoa unaweza kumkuta mwanamume anakuletea nyumba ndogo chumbani mwako wakati wakitakana kufanya mambo yao wewe mke wa ndoa unaambiwa ushuke kitandani ukalale sebuleni!.
Hivyo basi mambo ya kutuletea habari kuwa alikuwa mchoyo huwezi jua chanzo nini, wakati wanapendana wanachumbiana hadi wanaoana sidhani kama ulijua mchakato mazima.Hadi Bukuku anaamua kuingia ndani ya familia ya mumewe lazima alishajua baadhi ya maisha aliokuwa akishi mumewe Basila, mfano kama kuishi na ndugu zake!
Hana lolote sasa, kuhusu nini, wokovu.... nadhani hata wewe hapo ulipo unapambana na maisha yote mawili ya kutafuta mali ili uweze kuishi maisha mazuri na pili kupalilia roho yako kila siku ili siku ya mwisho uweze kunyakuliwa mbinguni.
Nadhani hakuna anayejua sababu ya yeye kuambua kumwimbia Lowasa huo wimbo, hakuna anayejua mapatano yao, labda anelipwa hela... huwezi jua,.....
Hapo ulipo wewe nadhani ungepata hiyo fursa sidhani kama ungekataa.Ni vema tukiri kuwa kila mtu hapa duniani ana njaa ya fedha si Bahati Bukuku tu.
Hivyo, pamoja na r oho yake mbaya, uchoyo wake, ubaya wake, mwombee kwa Mungu.