Bagamoyo: Watu wawili wafariki kwa mlipuko wa bomu, mmoja ajeruhiwa

Bagamoyo: Watu wawili wafariki kwa mlipuko wa bomu, mmoja ajeruhiwa

Kurunzi

Platinum Member
Joined
Jul 31, 2009
Posts
10,175
Reaction score
11,571
Watu wawili wamefariki papo hapo na mmoja kujeruhiwa vibaya huku nyumba kadhaa zikiharibiwa kufuatia mlipuko mkubwa uliotokea kwenye banda la kuchomelea vyuma chakavu, Mtaa wa Magomeni, Wilaya ya Bagamoyo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Salim Morcase, amethibitisha kuwa tukio hilo la kushtusha lilitokea Agosti 31 na Mlipuko huo unadaiwa kutokea baada ya mmoja wa waathirika kujaribu kukata kipande cha chuma, na kusababisha mlipuko uliokuwa na nguvu kubwa.

Kamanda Morcase amesema mbali na kusababisha vifo na majeraha, mlipuko huo pia umeharibu baadhi ya nyumba zilizokuwa karibu na eneo la tukio, na kusababisha hasara kubwa ya mali na pia imeleta taharuki kwa wakazi wa eneo hilo.

Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa kina kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama ili kubaini chanzo kamili cha mlipuko huo.

Kamanda Morcase amesema kuwa taarifa kamili itatolewa hivi karibuni baada ya uchunguzi kukamilika.

 
Duh!!!
Inachekesha lakini inasikitisha.....

Pole kwa wafiwa
Pole kwa majeruhi...
images (63).jpeg
 
Hii kitu iliwahi kutokea kwa mtu ninomjua kabisaaa Zanzibar

Lile eneo Zamani majeshi walikua wakilitumia ila wakaja kuacha sasa kipindi kimepita mvuvi mmoja akaja kuokota chuma icho anataka kufanya nanga ya boti yake akapeleka kwa fundi welding ngoma kumbe bomu likaripuka na kuua na kujeruhi kama hivi ilivotokea hii dah namkumbuka mpaka leo fundi yule Allah amjaalie kheri huko alipo
 
Epukeni kuingia kiholela maeneo yanayotumika katika mazoezi ya kijeshi au maeneo yaliyowahi kufanyiwa operation za kijeshi.
Sasa mtoto wa 2000 atafahamu ayo unoyasema
 
Back
Top Bottom