Bagamoyo Road au Morogoro Road: Wapi bora kununua kiwanja?

Bagamoyo Road au Morogoro Road: Wapi bora kununua kiwanja?

Morogoro Road ___ Uswazi.Com

Bagamoyo Road ___ Ushuani.Com

Fursa Kibiashara ___ Morogoro Road

Maisha Tulivu na Uwekezaji ___ Bagamoyo Road

Kelele Nyingi ___ Morogoro Road

Utulivu kama Wodi ya Upasuaji wa MOYO ___ Bagamoyo Road

Nunua Eneo uje uliuze baada ya miaka mi 5 au ujenge frem za biashara/Nyumba za Biashara ___ MoroGoro Road

Nunua Eneo Uje uishi Baadae huku ukiwa na utulivu wa NAFSI ___ BAGAMOYO ROAD

Binafsi nimedokoa Kote na sababu nakwambia haya nilishawahi kuwa na eneo Mlandizi nilinunua 600k 2021 nmekuja Uza kwa 20m mwaka Jana 2025 (nlieka kajumba ka kulindia kiwanja tu room 3) eneo la heka 2 tu.

Nikatoa 10m ikabaki 10m nikanunua tena eneo huko huko Porini ndani ndani.

Sasa hivi eneo nililopo Heka ni 4m na mimi nlinunua kwa 1m (8 acre)

Bagamoyo Huku ndio Ntazeeekea na Kufia, na bei za Bagamoyo ni nzuri.

KWA BEI :

MOROGORO ROAD ___ BEI JUU
BAGAMOYO ROAD ___ BEI CHINI (na itakua chini zaidi ukiuziwa eneo na MZAWA sio haya makampuni) japo hata makampuni bei zao n rafiki sana ACRE 1 wanaanzia 1.5m mpk 2m na unalipa kwa instalment.

Kama pesa ipo usichukue sehem 1 Chukua POTE...

HATA 20 X 20 Morogoro road sio ndogo baadae ni pesaaaa (hakikisha umepoint pazuri pakujenga nyumba za biashara na frem sio sehem ya kujenga nyumba tu)

Ila ukienda Bagamoyo Road usijibane Kama unazomba Zomba maeneo makubwaaaaa...

Binafsi naogelea kwenye BONGE moja la PORI sijui hata ntafanyaje akili za Kufuga ndio zimekuja Juzi.

Yote kwa Yote...Popote Kambi Ardhi haimtupi Mtu

MUHIMU : NUNUA ENEO KWA MTU SAHIHI OTHERWISE UTAKUJA KUJUTA NA KUCHUKIA UWEKEZAJI ARDHINI.
Ulinunua 600k umeuza 20M au ilikua hekari ?
 
Kule alikojenga Dr chenza.... kasomba heka 100+
ndiyo mkuu kule ardhi ni cheap sana. 50*100 kama ni kiwanja unapata kwa 3m
na kama ukohitaji pori unaweza pata 60k hadi 100k kwa hekari moja, bei hutofautiana kulingana na eneo mf eneo lenye vyanzo vya maji bei inakuwa juu kidogo.
 
Penda
ndiyo mkuu kule ardhi ni cheap sana. 50*100 kama ni kiwanja unapata kwa 3m
na kama ukohitaji pori unaweza pata 60k hadi 100k kwa hekari moja, bei hutofautiana kulingana na eneo mf eneo lenye vyanzo vya maji bei inakuwa juu kidogo.
Mkuu mimi nataka sana ila sijui napataje kama una weza niongoza nisaidie tu kwakweli nahtaji pori langu zuri Maji nitajichimbia maana hata ivyo kule WATER TABLE yake ipo juu sana.

Kisima cha mashine sidhani kama kitazidi 7m..sidhani

Tafadhali mkuu naomba kama kuna yeyote/mwenyeji umjuae kule niunganishe nae niende nahtaji Eneo kwakweli.
 
Penda

Mkuu mimi nataka sana ila sijui napataje kama una weza niongoza nisaidie tu kwakweli nahtaji pori langu zuri Maji nitajichimbia maana hata ivyo kule WATER TABLE yake ipo juu sana.

Kisima cha mashine sidhani kama kitazidi 7m..sidhani

Tafadhali mkuu naomba kama kuna yeyote/mwenyeji umjuae kule niunganishe nae niende nahtaji Eneo kwakweli.
Nitaenda next weekend kuonana na mwenyeji wangu alafu nitakufata dm kwa mawasiliano zaidi.
 
ndiyo mkuu kule ardhi ni cheap sana. 50*100 kama ni kiwanja unapata kwa 3m
na kama ukohitaji pori unaweza pata 60k hadi 100k kwa hekari moja, bei hutofautiana kulingana na eneo mf eneo lenye vyanzo vya maji bei inakuwa juu kidogo.
Huku panaitwaje aisee. naomba jina.la hii sehemu
 
Nyie vijana huko Kibaha tangu miaka ya 90 tulikuwa tunasema patakuwa Hot, ila hadi leo hapaeleweki.
Viwanja bado vipo vingi mjini acheni uoga wa maisha, kununua kiwanja na kujenga nje ya mji hizo ni akili za uoga na kizee, na mwisho wa siku unatumia pesa nyingi kwenda mjini kazini kwako
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom