Badili mkao wa kitanda chumbani

Badili mkao wa kitanda chumbani

Sababu ni ipi sasa kitanda kikiinama unaota? Na unaota ndoto za namna gani?
Sababu ni za kimwili tu wala si uchawi wala nguvu za giza.
Nadhani damu inapokuwa imehamia kichwani/ubongo ndio sababu za ndoto kuja kwa mfululizo.

Na unaota ndoto za namna gani?


Ndoto huwa mchanganyiko
 
Naamini huu ni wakati muafaka wa kusoma huu uzi...!kama uko chumbani kwako angalia position ya kitanda chako na jiulize kama una amani...!!!

Wengi wetu hupenda kubadili position ya kitanda chumbani kila baada ya muda fulani...hii ni natural attraction ambayo huleta mtazamo mpya na mvuto pia.

Lakini kama wewe ni mfuatiliaji lazima Ulishawahi kukumbana na hiki kisanga kwamba baada tu ya kubadili mkao wa kitanda chumbani basi maruerue ndoto za kutisha na majinamizi vimekuwa havikomi usiku chumbani

Wengi bila kujua asili ya tatizo wamejikuta wakikimbilia kwa waganga wa kienyeji na kupoteza pesa nyingi lakini ukweli ni huu hapa

Ndani ya vyumba vyetu vya kulala kuna kona au upande ni mapito ya nguvu za giza

.Ndani ya vyumba vyetu vya kulala kuna kona au upande ni makazi ya roho chafu

Ndani ya vyumba vyetu vya kulala kuna kona au upande ni centre ya mawasiliano kati ya nguvu za giza na ulimwengu wa roho

Ndani ya vyumba vyetu vya kulala kuna kona au upande ni makazi ya roho za uharibifu

Hivyo basi unapobadili position ya kitanda na usiku wa kwanza au wiki ya kwanza ukaanza kupata mambo mageni usihangaike wala kupata shida na waganga wa kienyeji ama fikra za kufanyiwa ushirikina peleka kitanda chako upande mwingine utakuwa umesolve tatizo ambalo lingekugharimu pesa mingi.

Angalizo;
Si wote wanaokutana na hizi hali na kwa wale wanaosali na kufanya dua kabla ya kulala ni mara chache mno kukutana na hizi hali
Mimi ni mwaminio na YESU KIRSTO NDIO MUNGU WANGU hata ivo naliamini neno na ndo chakula cha uzima maana kumkiri KRISTO lazima ulishike neno,nauliza tu wewe una elewa vipi kuhusiana naWAAMINI/WAAMINIO
 
Nyongeza kwa wasomaji. Hata siku moja usiweke kitanda sehemu ya kichwa ikaelekezwa kaskazini. Elekeza sehemu yoyote isipokuwa kaskazini tu. Sababu za kutoelekeza kichwa kaskazini ni kwa sababu zifuatazo. Kwanza kwenye damu ya mwanadamu kuna kitu kinaitwa Haemoglobin ambayo ina madini ya iron ambayo ndiyo utumika kusafirisha oxygen kwenye mwili wa binadamu. Dunia pia imejazwa na magnetic field ambazo ambazo sifa zake ni kwamba siku zote ni kwamba nguvu za uvutano uelekea kazikanini. Hivyo basi u napolala wakati kichwa kimelekea kazikazini madhara yake ni kwamba nguvu ya uvutano ya sumaku (magnetic field) itavuta ubongo wako uliona madini ya chuma (iron) na kukusababishia mgandamizo (pressure) kwenye ubongo wako ambao unaweza kukusababisha stroke.

Nataka kukubaliana na wewe. Mie mara nyingi nikilala kichwa kaskazini au kusini usiku kucha ni majinamizi! mara uote unakula minyama michafu, mara unaua, ili mradi ni shida. Na hii hubadilika kila baada ya vipindi vya majira yaani summer au winter na hususani kuelekea September na March. Hivyo kwa mwaka naweza kubadili ulalaji ( welekeo wa kichwa) mara nne......kuelekea September, December, March na June. Bila hivyo nitaweweseka usiku kucha na kama ni mgeni utanikimbia. Ila nikibadili tu mambo yanakaa sawa!!! mshana jr r Invisble275
 
Mimi ni mwaminio na YESU KIRSTO NDIO MUNGU WANGU hata ivo naliamini neno na ndo chakula cha uzima maana kumkiri KRISTO lazima ulishike neno,nauliza tu wewe una elewa vipi kuhusiana naWAAMINI/WAAMINIO
Mimi nami ni kana wewe tuu. . . nami ni wa Kristo nikiwa na imani thabiti isiyotetereka
 
Nataka kukubaliana na wewe. Mie mara nyingi nikilala kichwa kaskazini au kusini usiku kucha ni majinamizi! mara uote unakula minyama michafu, mara unaua, ili mradi ni shida. Na hii hubadilika kila baada ya vipindi vya majira yaani summer au winter na hususani kuelekea September na March. Hivyo kwa mwaka naweza kubadili ulalaji ( welekeo wa kichwa) mara nne......kuelekea September, December, March na June. Bila hivyo nitaweweseka usiku kucha na kama ni mgeni utanikimbia. Ila nikibadili tu mambo yanakaa sawa!!! mshana jr r Invisble275
Unajua kwakuwa kuna watu aidha kwa kukosa tafakuri au kwa kutojua au vinginevyo waliona kama hii mada ni kitu tu cha kufikirika toka kichwani mwangu kama mmoja alivyochangia....siwezi kuwalaumu kwakuwa dunia yao iko chini ya mwamvuli
 
mshana jr Leo umenifungua macho mkuu. Kuna wakati ilikua ikifikasaa nane usiku lazima niweweseke au kuamka Kwa mshtuko sometimes nahisi kuna mtu ndani zaidi ya sisi wawili kitandani ikafikia hatua tunahama chumba ikawa kitu kinaniambia kitanda mwelekeo wake so mzuri badili mpaka nikaamua rasmi kubadili Toka hapo sjaweweseka hata kidogo
 
Back
Top Bottom