Babu yangu..

Babu yangu..

Mentor

JF-Expert Member
Joined
Oct 14, 2008
Posts
20,334
Reaction score
23,941
Sijui kama ni wote tulikuwa na babu wenye vituko hivi..ila mi babu yangu alikuwa amewazidi wote..
Mzee Nyela aliitwa...
siku moja kasafiri kaenda Mombasa. kurudi akaja na chumvi ile ya mabonge..
akawaita wamama wa jirani akawaambia ana chumvi kali sana na nzuri from Mombasa.
Walipokuja ikabidi awape darasa jinsi ya kuitumia maana matumizi yake ni tofauti na chumvi walizozoea.
Akaanza;
"(kwa kichagga) Chumvi hii ni kali sana, yani kuitumia inabidi uipake mikononi ndo uanze kumenya ndizi. USIjaribu kuiweka kwenye chakula direct..maana utaachika kwani chakula kitakuwa na chumvi sana. Na hata ukimaliza kumenya, inabidi uzioshe sana kwa maji.."
Basi, wamama wa watu wakanunua chumvi ya mzee...wacha usiku aanze kusikia wamama wa watu wakilia kwa vipigo..kisa: chakula hakina chumvi!!!!

Huyo ni babu yangu..babu yako alikuwa na vituko gani unavyokumbuka?!
 
Siku nyingine tumetoka kumchukua dukani kwake (alikuwa mshonaji mzuri sana wa nguo)..na amelewa si kichezo,
sasa tukawa tunashuka kilima cha kuelekea nyumbani (kichumi). Akatuambia, "wajukuu zangue, nyie tangulieni mbele, ili mkiteleza nije nikiwaokota"lol
Kumbe huku nyuma yeye ndo alikuwa akiteleza na kuanguka kila saa. Yani trick yake ni ili tusimuone anavyoanguka...
Mzee Nyella huyo!
 
Babu yangu alikuwa na vitu sana, mtaani walikuwa wanamwita pilipili jinsi alivyokuwa mkali, katika vitu alivyokuwa anachukia ni akukute unaonea....awe mtu ...mnyama au mdudu, siku moja siafu wakaingia jikoni kwake, akaja akatukuta tunazichoma akatuletea noma kinoma yaani na kusema acheni wadudu wa Mungu, kuna siafu alipandia akamng'ata nyuma ya goti.... aliruka na bakora ikarushwa pembeni.....alipomtoa alisema "lazima nikushome...."akamtupia kwenye moto....na akaturuhusu kuchoma wote....


Siku nyingine tukawa tunaua panya buku, tukaziba njia zake zote za kutokea shimoni na kubakiza shimo moja tulilolitumia kuingiza maji ya mfereji.... kadri tulivyokuwa tunajaza maji na panya buku kuonyesha dalili zote za kutoka ndivyo babu yangu alivyokuwa anatutaka kuwa wajasiri...kila mtu alisimama kwenye shimo lake... panya buku akatoka speed shimo alilokuwa kasimama babu...Babu alishtuka badala ya kumpiga akabaki akisema huyu hapa huyu hapa huku anasogea pembeni....
 
mi babu yangu ni mzee sana maana alizaliwa kipindi kile ule uwanja wa man u unaitwa Old traphod enzi hizo ulikuwa unaitwa NEW TRAPHOD
 
mi babu yangu ni mzee sana maana alizaliwa kipindi kile ule uwanja wa man u unaitwa Old traphod enzi hizo ulikuwa unaitwa NEW TRAPHOD
Du Samito, mbona unatulisha matango pori aisee!???
 
Babu yangu alikuwa anaitwa Tondoloveta(nadhani ni tusi la kijerumani).tafuta Yeye alikuwa anatuhimiza kutafuta mademu
 
Babu yangu yupo humu humu jf. Ngoja aseme mwenyewe vituko vyake.
 
Babu yangu alikuwa anaitwa Tondoloveta(nadhani ni tusi la kijerumani).tafuta Yeye alikuwa anatuhimiza kutafuta mademu

Hahahahahahahaha...kaka, kama babu yako ni mchaga basi wala si tusi la kijerumani ni kichaga...hahahahaahah!
tondoloveta==mjinga wa veta!!lol
itondo=mjinga
lo=wa
veta=veta!
Alifeligi veta nini!???teh teh teh....du, kweli babu yako nyi itondo kapisa!!!
 
Babu alikuwa anapenda sana sigara kalì nyota, sijui bado zipo
Du, hizi nadhani itabidi ujitengenezee mwenyewe...customized...na majani ya mpapai!Lol
Babu yangu ndo alitufunza hivo...hahahah, #gud old days
 
me babu yangu akiwa mzee kabisa alini2ma viagra,nashukuru mwenye duka alinikatalia sababu ya udogo wangu sasa nimekuwa ndo nimejua alikuwa ana maanisha nn!
 
Siku nyingine tumetoka kumchukua dukani kwake (alikuwa mshonaji mzuri sana wa nguo)..na amelewa si kichezo,
sasa tukawa tunashuka kilima cha kuelekea nyumbani (kichumi). Akatuambia, "wajukuu zangue, nyie tangulieni mbele, ili mkiteleza nije nikiwaokota"lol
Kumbe huku nyuma yeye ndo alikuwa akiteleza na kuanguka kila saa. Yani trick yake ni ili tusimuone anavyoanguka...
Mzee Nyella huyo!

Babu yangu Meku Serya...

Siku mvua inanyesha sie tunaota moto huku tukichoma maindi, akaachia ushuzi kwa bahati mbaya....nilisikia nikauchuna naye akauchuna. Ushuzi ulipotoa harufu mbaya, kaka yangu akala makwenzi na kupigwa mkwala "wanaume huwa hawajambi hovyo"........Kaka akitaka kujitetea babu akamkatiza "Nyamaza, malabuku" Akala kwenzi jingine.

dah! Ushuzi aachie babu, kwenzi atiwe bradha.............nlitoka nje nikacheka sana.....ningechekea pale nami ningekula kwenzi.......!

RIP my dear Babu.... I miss you vibaya sana!
 
me babu yangu akiwa mzee kabisa alini2ma viagra,nashukuru mwenye duka alinikatalia sababu ya udogo wangu sasa nimekuwa ndo nimejua alikuwa ana maanisha nn!

Du Mdau, hope hiyo tabia hujaiiga!
 
Babu yangu alikuwa na vitu sana, mtaani walikuwa wanamwita pilipili jinsi alivyokuwa mkali, katika vitu alivyokuwa anachukia ni akukute unaonea....awe mtu ...mnyama au mdudu, siku moja siafu wakaingia jikoni kwake, akaja akatukuta tunazichoma akatuletea noma kinoma yaani na kusema acheni wadudu wa Mungu, kuna siafu alipandia akamng'ata nyuma ya goti.... aliruka na bakora ikarushwa pembeni.....alipomtoa alisema "lazima nikushome...."akamtupia kwenye moto....na akaturuhusu kuchoma wote....


Siku nyingine tukawa tunaua panya buku, tukaziba njia zake zote za kutokea shimoni na kubakiza shimo moja tulilolitumia kuingiza maji ya mfereji.... kadri tulivyokuwa tunajaza maji na panya buku kuonyesha dalili zote za kutoka ndivyo babu yangu alivyokuwa anatutaka kuwa wajasiri...kila mtu alisimama kwenye shimo lake... panya buku akatoka speed shimo alilokuwa kasimama babu...Babu alishtuka badala ya kumpiga akabaki akisema huyu hapa huyu hapa huku anasogea pembeni....

umenikumbusha enzi za fuko na ngawa na vilochindi na makoru na nduu na sowe na mafido na pichini na nuka na kiumbo na visoia na masale na mawiri n.k n.k
 
umenikumbusha enzi za fuko na ngawa na vilochindi na makoru na nduu na sowe na mafido na pichini na nuka na kiumbo na visoia na masale na mawiri n.k n.k
aisee...we m2 wa wapi raia??
 
Babu yangu Meku Serya...

Siku mvua inanyesha sie tunaota moto huku tukichoma maindi, akaachia ushuzi kwa bahati mbaya....nilisikia nikauchuna naye akauchuna. Ushuzi ulipotoa harufu mbaya, kaka yangu akala makwenzi na kupigwa mkwala "wanaume huwa hawajambi hovyo"........Kaka akitaka kujitetea babu akamkatiza "Nyamaza, malabuku" Akala kwenzi jingine.

dah! Ushuzi aachie babu, kwenzi atiwe bradha.............nlitoka nje nikacheka sana.....ningechekea pale nami ningekula kwenzi.......!

RIP my dear Babu.... I miss you vibaya sana!
RIP babu Asprin ila nna hakika utakuwa umemsingzia..,lol.
 
Back
Top Bottom