Baba wa taifa Mwalimu JK Nyerere aliwahi kuvuta sigara?

Baba wa taifa Mwalimu JK Nyerere aliwahi kuvuta sigara?

asante mi navuta nimeanza mkakati wa kuacha ila nakuwa kama naumwa na viungo vinavuta kama nimetoka mazoezini. Pia ni kiongozi wa kisiasa wafuasi wangu wananishauri niache fegi sasa sijui nikivuta wao wanaona inanipunguzia nini.ila nimeacha mvinyo kwa lengo la kuacha fegi nasoma sana vitabu na kusoma majadiliano hapa JF

Mimi Nataka Nianze Kuvuta Nikimalza Chuo, Of Koz nataman sana fegi ila naona kama nitawakwaza wadau wang hapa mliman
 
Mkuu Msulibasi nina audio niliirekodi kutoka kipindi cha wosia wa baba cha Tbccm.Ndani yake Mwl Nyerere kakiri kuwa alitumiaga sigara ila akaacha Hii speech kiufupi kasema hivi(ni ndefu lakini)"Mimi ninatumia kila kitu cha serikali...navaa nguo za serikali...natembelea motokari ya serikali..HATA WAKATI NAVUTA SIGARA NILIKUWA NAVUTA ZA SERIKALI..''
Binafsi nilishangaa sana kumsikia kuwa Mzee alitumiaga fegi enzi hizo.
Kama unaihitaji ama yeyote aitakaye ani PM namba zake za whattsapp nimrushie.
 
Last edited by a moderator:
Jbu Ni Ndiyo Alishawahi Kuvuta, Marxists ilikua n kama principle kuvuta, ndio maana hata mm mwenye imani ya mlengo wa kushoto najiona cjitendei haki kutovuta, yan nikimalza chuo n mwendo wa fegi
 
Nilikua napitia gazeti la Drum la nikaona picha ya nyerere akiwa ameshika sigara inawaka, jambo hili sikuwahi tena kusikia wala kuona pahala pengine. Huwa linanipa mawazo sana juu ya ni nini hasa nilichokiona.

Kwa uhakika wa 100%; ni kweli alikuwa anavuta sigara. Aliamua kuacha baada ya Dr kumshauri kuchagua kati ya uongozi na sigara maana vyote ni kazi ngumu na ya kuchukua muda.

Anjo.
 
Hata Soda yake ilikuwa ni Double Cola na juice ya Orange Squash
 
Nilikua napitia gazeti la Drum la nikaona picha ya nyerere akiwa ameshika sigara inawaka, jambo hili sikuwahi tena kusikia wala kuona pahala pengine. Huwa linanipa mawazo sana juu ya ni nini hasa nilichokiona.

Mimi binafsi yangu nimeshamuuzia sigara karata. Alikuwa anavuta.

Wakati wa ujana wa akina Nyerere ilikuwa kuvuta sigara ni kuonekana umeendelea kwani hilo lililetwa na wazungu na unajuwa tena Miafrika kwa wazungu, hatuna ujanja. Hata baya mradi anafanya mzungu au aliyetoka kwa wazungu basi kwetu ni "cool" hadi hii leo. Hujaziona KK wewe mitaani?
 
Ivi kuna mtu wa ukanda wa pwani ambaye sio teja wa sembe?
 
Mimi binafsi yangu nimeshamuuzia sigara karata. Alikuwa anavuta.

Wakati wa ujana wa akina Nyerere ilikuwa kuvuta sigara ni kuonekana umeendelea kwani hilo lililetwa na wazungu na unajuwa tena Miafrika kwa wazungu, hatuna ujanja. Hata baya mradi anafanya mzungu au aliyetoka kwa wazungu basi kwetu ni "cool" hadi hii leo. Hujaziona KK wewe mitaani?

Ukiamuwa kufunguka ongea yote acha kuficha wakati hata papuchi ulimuuzia pia.
 
Back
Top Bottom