Shost alikuwa na mapenzi kwa boy friend wake, alikuwa anakwenda for a week, wakati huo ni mwanafunzi. Majibu yalipotoka amepiga chini, basi aliamua kuhamia kwa jamaa mazima. Walianza kuishi kama mume na mke na kufanikiwa kupata watoto wawili.
Jamaa ni mchacharikaji hasa, anapigana mpaka nchi jirani kwenye biashara. Amejenga nyumba ya kawaida, kuna usafiri wa kupeleka watoto shule, mama ana ka usafiri kake. Shost yangu hafanyi kazi, ni mama wa nyumbani.
Sasa hivi hawana maelewano kabisa na mwanaume huyu. Yaani yule mwanaume anakuja pale nyumbani kuangalia watoto wake tu, anaishi na shost kama yuko na shemeji yake. Zaidi ya salamu hakuna hata kiss, hii hali imekua inamfustruate shost yangu tangu January mwaka huu. Kumbuka hajaolewa wala kutolewa mahari. Sasa nilimpa ushauri aende kwao kidogo ampe jamaa nafasi ya kumiss.
Kilichotokea, shost alikwenda kwao, jamaa wala hajapiga hata simu, sasa kinachomuuma aliacha watoto akitegemea baada tu ya siku mbili atapigiwa simu arudi, kimya. Baba yake ameamua kumpigia simu baba watoto, anamuuliza unafahamu kuwa mwenzio yuko hapa, akasema anafahamu ndio maana hakumtafuta. Baba akauliza tena hujiulizi kwanini amekuja bila kukuaga? Alijibu, baba niko busy nikipata nafasi tutaongea vizuri.