Baba mkwe ndo mchawi wa mtoto wetu

Wiyelelee

JF-Expert Member
Nov 9, 2012
1,071
347
Jamani, nimejitokeza sana hapa. Kabla sijaendelea na kisa hiki, naomba nikuulize swali- Je unaamini kwamba uchawi upo? Mwenzenu imenibidi niamini tu pamoja na kashule kangu kadogo nilikokasotea pale Mlimani, na vyuo vingine. Ni hivi. Tangu tupate mtoto wetu wa kwanza miaka 5 iliyopita, amekuwa akiumwa kila siku. Kama ni hospitali zote za nguvu hapa amepita kwa kulazwa na si mara moja. Wazazi na mtoto wote hatuna ugonjwa wa kisasa. Ugonjwa huo wa ajabu, unamfanya mtoto apoteze fahamu.

Kwa kifupi, hospitali walishindwa. Nikaamua kusafiri zangu mwaka jana baada ya ushauri kwa rafiki yangu anaetoka Nyanda za Juu Kusini! Tukaenda nae kwao. Tulipita kwa watu tofauti wanne tena wanaishi umbali wa kilo mita karibu 60 au 70 kutoka kwa mwingine. Kila tulipofika tu bila kueleza chochote, walisema - "Mmeleta shida ya mtoto huyu". Kila mmoja wa "watalaam hao" alimtaja baba mkwe kwamba yeye ndo chanzo cha matatizo ya mtoto wetu.

Sikuamini moja kwa moja. Nilipata safari ya kikazi ya kwenda hapo Kigoma, nikambeba mtoto pia, nako nikaambiwa yale yale yanayofanana na wale wa Nyanda za Juu kusini (Mbeya na Rukwa).

Cha ajabu, mtoto akiumwa, baba mkwe anakuwa wa kwanza kufika hosp, na kutoa ushauri wake. Tena anahuruma sana, wakati mwingine huwa anaomba kukaa na mtoto karibu mwezi mzima! Kumbe kupindi mtoto akilazwa yeye ndo furaha yake!

Ni kweli nasalimiana nae, nacheka nae, ila namjua kwamba ni mbaya wangu. Hadi leo mtoto hawezi hata kuembea. Amenitia hofu ya kupata hata mtoto wa pili. Mke wangu tumeonge nae sana, nae anasema anamjua baba yake ila hakujua kwamba anaweza kuwa mbaya kiasi hicho! Jamani kuoa tuwe tunauliza, hasa tunaooa hapa Salidalama! Tunakutana tu kwenye daladala au kwenye FB!

Nikimuona baba mkwe, moyo wangu unakuwa mweusi sana! Sijui nifanyeje....
 
Biblia huandika ya kwamba, amelaaniwa mtu yule mwenye kumtegemea mwanadamu...

Yeremia 17:5 Bwana asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha Bwana.
 
Nakumbuka kuna siku nilimtazama hadi machozi yalinitoka, aliinamisha kichwa chini tu bila kusema kitu. Kweli ananikosea sana. Mama mkwe hana tatizo lolote. Tatizo ni huyu baba.
 
Biblia huandika ya kwamba, amelaaniwa mtu yule mwenye kumtegemea mwanadamu...

Yeremia 17:5 Bwana asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha Bwana.


Hapa bado hujanisaidia sana, naomba ushauri. Ni kweli nakuelewa na kusali nasali pia, tena sana. Ila ilinibidi niache kwa muda nishughulikie swala la mtoto.
 
Aisee sasa we mura umeamua kwenda kwa wataalam wa dunia si wakupe dawa?

Dah ila inauma sana aisee, pole
 
mchawi mpe mtoto akulele mwambie baba nimegundua wewe ndio chanzo cha mtoto huyu kuugua namna hii sasa nakuachia asipopona utanijua nakuhakikishia atajuta
 
Ni kweli kabla ya kuoa ni vyema kuzingatia huyo bint pamoja na ukali wa sura, umbo na shule kichwani anatokea wapi. Wadogo zetu mjifunze jamani hivi vingine vinaepukika, brother usife Moyo hilo litapita na ni vyema kukaa na kuongea na mkwe vzr, km hana nyimba au umeme muwekee tu afurahi. Ukute wewe unaishi vzr sana wkt yeye anaish vby sana
 
Hapa bado hujanisaidia sana, naomba ushauri. Ni kweli nakuelewa na kusali nasali pia, tena sana. Ila ilinibidi niache kwa muda nishughulikie swala la mtoto.

Yaani ni hivi, hao vigagula ni binadamu na baba mkwe naye ni binadamu lakini MUngu ni mkuu juu ya hao wote.

Kama aliweza kukupa mtoto atashindwaje kumfanya apone kwa hayo yanayomsibu?

Hivyo sidhani kama kweli huyo ndugu au wewe alisali kwa kumaanisha
 
Sikia jamaa kwa swala la mtoto acha ujinga mfuate mueleze ukweli na ikiwezeka safiri nae mpaka kwa huyo mtaalam. Ila usimwambie kwa njia ya upole uwe mkali kwelikweli ili ajue na umwambie njia zote ulizopita. Njia nyingine nenda mtoto wako wake mwambie wewe ndio tatizo kwa mwana na umuachie kwa huyo mtoto kwa mkwara mzito, umwambie nitarudi baada ya siku tatu nikute mwanangu mzima. La sivyo kinachofuata atavunja na ndoa yako.
 
Nianze kwa kukupa pole sana kwa utata huu mkubwa ambao kwa kweli unakuweka ktk njiapanda ya kufanya maamuzi.
Ila ushauri wangu ni huu, kama ww ni mkristo na unaamini ktk nguvu ya Mungu kupitia maombi basi jawabu la matatizo yako ni MAOMBI tu ila yawe serious na yanoaambatana na imani kwamba Mungu anaweza kila jambo na hili ni dogo sana kwake. Hakika ndani ya muda mfupi tu utauona mkno wa Mungu na mchawi huyo ataumbuka na ndo itakuwa mwisho wake pengne kukuchezea. Ninavyosikia mm ni kwamba mchawi ukimwendea kwa mganga akazidiwa nguvu basi kama kweli amedhamiria kukutesa basi bado ataenda tu kutafuta mbinu nyingne ya kupamabana na ww hadi akamilishe adhma yake.
Lkn kwa Mungu ni uhakika na kuna majibu ya kudumu.
Pole sana ndugu.



Jamani, nimejitokeza sana hapa. Kabla sijaendelea na kisa hiki, naomba nikuulize swali- Je unaamini kwamba uchawi upo? Mwenzenu imenibidi niamini tu pamoja na kashule kangu kadogo nilikokasotea pale Mlimani, na vyuo vingine. Ni hivi. Tangu tupate mtoto wetu wa kwanza miaka 5 iliyopita, amekuwa akiumwa kila siku. Kama ni hospitali zote za nguvu hapa amepita kwa kulazwa na si mara moja. Wazazi na mtoto wote hatuna ugonjwa wa kisasa. Ugonjwa huo wa ajabu, unamfanya mtoto apoteze fahamu.

Kwa kifupi, hospitali walishindwa. Nikaamua kusafiri zangu mwaka jana baada ya ushauri kwa rafiki yangu anaetoka Nyanda za Juu Kusini! Tukaenda nae kwao. Tulipita kwa watu tofauti wanne tena wanaishi umbali wa kilo mita karibu 60 au 70 kutoka kwa mwingine. Kila tulipofika tu bila kueleza chochote, walisema - "Mmeleta shida ya mtoto huyu". Kila mmoja wa "watalaam hao" alimtaja baba mkwe kwamba yeye ndo chanzo cha matatizo ya mtoto wetu.

Sikuamini moja kwa moja. Nilipata safari ya kikazi ya kwenda hapo Kigoma, nikambeba mtoto pia, nako nikaambiwa yale yale yanayofanana na wale wa Nyanda za Juu kusini (Mbeya na Rukwa).

Cha ajabu, mtoto akiumwa, baba mkwe anakuwa wa kwanza kufika hosp, na kutoa ushauri wake. Tena anahuruma sana, wakati mwingine huwa anaomba kukaa na mtoto karibu mwezi mzima! Kumbe kupindi mtoto akilazwa yeye ndo furaha yake!

Ni kweli nasalimiana nae, nacheka nae, ila namjua kwamba ni mbaya wangu. Hadi leo mtoto hawezi hata kuembea. Amenitia hofu ya kupata hata mtoto wa pili. Mke wangu tumeonge nae sana, nae anasema anamjua baba yake ila hakujua kwamba anaweza kuwa mbaya kiasi hicho! Jamani kuoa tuwe tunauliza, hasa tunaooa hapa Salidalama! Tunakutana tu kwenye daladala au kwenye FB!

Nikimuona baba mkwe, moyo wangu unakuwa mweusi sana! Sijui nifanyeje....
 
YESU NI JIBU!!!!!!!!!!!!!!!!!! Sali zaburi ya 35 na onana na padri/pastor utaona maajabu ya bwana! Uimpa BACK TO SENDER MOJA harudii tena.

Mimi akienitenda kunilaza bedrest mwezi mzima nimempa BACK TO SENDER nae yuko bedrest wiki 2, hoi an apata dripu double double! Nae mwezi kitandani utamhusu!

Akishanena kwa lughaa akaachia BACK TO SENDER!!!!!!!!!!!Game over!
 
Pole sana.


Inauma hakika maana kwaufupi nyumba
nzima mnapata tabu sana kutafuta nafuu
Ni vema basi ukasema hao jamaa uliokwenda
kwao wakasema mkweo ni tatizo

Hawajafanikiwa kukupatia ufumbuzi wa tatizo?
Maana kwasasa mnapoteza pesa nyingi
kutafuta tiba ya mtoto awe vizuri sana.

Msikate tamaa zaidi endeleeni kutafuta tiba
maana Baba Mkwe hata ukimwambia hawezi
kukubali kuwa ndiyo chanzo cha ugonjwa
wa mtoto.
 
Mimi siamini uchawi,mwambie baba mkwe wako aniloge,na tena kamwambie TUKUTUKU anasema wewe ni mjinga sana na tena ni mzigo kwa taifa hili!
 
Ni kweli kabla ya kuoa ni vyema kuzingatia huyo bint pamoja na ukali wa sura, umbo na shule kichwani anatokea wapi. Wadogo zetu mjifunze jamani hivi vingine vinaepukika, brother usife Moyo hilo litapita na ni vyema kukaa na kuongea na mkwe vzr, km hana nyimba au umeme muwekee tu afurahi. Ukute wewe unaishi vzr sana wkt yeye anaish vby sana

Ni kweli, ila huwezi kuamini. Baba Mkwe ni msomi mzuri tu, tena mstaafu wa mashirika ya umma
 
Na akiendelea kumroga akafa je?
ajue tu kwamba umejua yeye ndio chanzo ,ngoja nikusimulie kitu nilipomaliza chuo sikutafuta ajira nikajiajiri huko upanga -mazengonilikuwa na biashara yangu ilikuwa inalipa sana sasa mhindi mmja akafungua na yeye vimbwanga vikaanza hapo leo dawa mlangoni kesho kishimo hella ikaanza kupotea na kupotea biashara ikaniendea vibaya renew capita na wewe sasa alikuwa amezoea natumia gari fulani siku hiyo nikaja na gari nyingine tena tinted nikamsubiria wee kama 3hrs kweli akaja akakaa pale mlangoni akaanza kuchimba nikashuka paaaaap nilimlamba makofi nikamjazia na watu pale nikamchamba kisawasawa nakuhakikishia hakuendelea kunichawia haya mambo usiyaogope mpe laive.
ila kwa huyu AMPELEKE AKAOMBEWE ATAPONA KWA IMANI ,PIA AMWAMBIE HUYO BABA MTOTO WANGU AKIFA ATAMLA NYAMA PIGA BIT
 
Back
Top Bottom