Gustavo Gaviria
JF-Expert Member
- Nov 19, 2018
- 630
- 1,109
Wakuu za mida hii.
Nina mchumba wangu ambaye nilimtolea kishika uchumba, tulibahatika kupata mtoto wa kiume, alijifungulia nyumbani kwetu(Kazi zangu nafanya sehemu ambayo haikumruhusu kujifungulia kwangu) mtoto nikampa jina(la baba yangu mzazi), basi baada ya mwezi mmoja alikwenda kusalimia kwao.
Alipo kaa week mbili mchumba akapiga simu kwangu akasema baba yake anasema anahitaji kumbatiza mtoto siku ya pasaka, kwa jina lake(yaani jina la baba mkwe) na hiyo siku inabidi niwepo kanisani kwao, je ninasemaje? nikamwambia hapana mtoto anatakiwa afate mahali ninakosali mimi hivyo aache tu mtoto atakuja kuwekewa wakfu atakaporudi, maana tutarudi kumchukua binti na kumtolea mahari ili arudi kuendelea na malezi nyumbani kwetu, maana utaratibu wa dini yangu sio ya kule kwao binti akasema sawa.
Jioni ya leo hii baba mkwe kapiga simu kwa mama yangu akisema kwamba anambatiza mtoto pasaka hii, nilipigiwa simu na mama kuniuliza kama hicho kitu nimeambiwa, nikamwambia hapana, nilikataa na nilimueleza kuwa asifanye hivyo.
Nikamrudia binti kumuukiza imekuwaje maagizo niliyoyatoa yamepuuziwa, akaniambia kuwa baba yake amekataa amesema kuwa hawezi kukubali kwa sababu sijamtolea chochote binti yaani mahari, kwa hiyo maamuzi hayo ndio ya mwisho na nyumbani amepiga tu kutoa taarifa.
kwa sasa bado sijafanikisha kutoa mahari, bado naitafuta na nyumbani kwao niliwaeleza kuwa ninajipanga ili nimtolee binti chochote aje kwangu, hivyo nadhani hapo ndio weakness yangu ilipo.
Wakuu hii kitu imekaaje.
Mbona kama nachanganywa,
Ushauri wenu ni wa muhimu.
Nina mchumba wangu ambaye nilimtolea kishika uchumba, tulibahatika kupata mtoto wa kiume, alijifungulia nyumbani kwetu(Kazi zangu nafanya sehemu ambayo haikumruhusu kujifungulia kwangu) mtoto nikampa jina(la baba yangu mzazi), basi baada ya mwezi mmoja alikwenda kusalimia kwao.
Alipo kaa week mbili mchumba akapiga simu kwangu akasema baba yake anasema anahitaji kumbatiza mtoto siku ya pasaka, kwa jina lake(yaani jina la baba mkwe) na hiyo siku inabidi niwepo kanisani kwao, je ninasemaje? nikamwambia hapana mtoto anatakiwa afate mahali ninakosali mimi hivyo aache tu mtoto atakuja kuwekewa wakfu atakaporudi, maana tutarudi kumchukua binti na kumtolea mahari ili arudi kuendelea na malezi nyumbani kwetu, maana utaratibu wa dini yangu sio ya kule kwao binti akasema sawa.
Jioni ya leo hii baba mkwe kapiga simu kwa mama yangu akisema kwamba anambatiza mtoto pasaka hii, nilipigiwa simu na mama kuniuliza kama hicho kitu nimeambiwa, nikamwambia hapana, nilikataa na nilimueleza kuwa asifanye hivyo.
Nikamrudia binti kumuukiza imekuwaje maagizo niliyoyatoa yamepuuziwa, akaniambia kuwa baba yake amekataa amesema kuwa hawezi kukubali kwa sababu sijamtolea chochote binti yaani mahari, kwa hiyo maamuzi hayo ndio ya mwisho na nyumbani amepiga tu kutoa taarifa.
kwa sasa bado sijafanikisha kutoa mahari, bado naitafuta na nyumbani kwao niliwaeleza kuwa ninajipanga ili nimtolee binti chochote aje kwangu, hivyo nadhani hapo ndio weakness yangu ilipo.
Wakuu hii kitu imekaaje.
Mbona kama nachanganywa,
Ushauri wenu ni wa muhimu.