GE2025 Baba Levo VS Zitto Kabwe naomba qualification/CV zao

GE2025 Baba Levo VS Zitto Kabwe naomba qualification/CV zao

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025
Baba Levo ni mtu na nusu.Waulize Kata ya Mwanga Kaskazini.Baba Levo akiwa mbunge Kigoma itaendelea.
 
Ingekuwa CV ya elimu kubwa ndio inakupa ubunge. Walioishia Darasa la saba Kina Msukuma, shigongo,babu tale, tajiri kishimba wasingekuwepo bungeni.

Pia hata mama samia na division four yake hasingeupata urais.. bali u rais wangepewa ma professor na A zao za masomo yote

Uzuri Life ina rewards watu wa aina zote, hata ambao hawajasoma sana wapo ambao wanafanikiwa sana
Naheshimu maoni yako.
 
Ni Majimbo mawili tofauti , Dalali ZZK yupo Kigoma Kaskazini, Baba Levo atavaana na Abdul Nondo Kigoma Mjini
 
Naomba qualification/CV zao.

Bila Shaka kwenye Elimu na Uzoefu wa siasa, ZITTO atakuwa anamzidi Baba LEVO.

Sifa zingine:
Baba LEVO ni CHAWA

ZITTO ni mnafiki na opportunist.
Baba Levo anaangushwa na Zitto saa nane mchana.
 
Baba levo ni mgombea mgumu sana kwa zitto.

Kwenye siasa ogopa sana nguvu ya umaarufu.

Kumbuka baba levo alishakuwa diwani hapo kigoma mjini.
Na zito alikuwa mbunge hapo kigoma mjini, ingawa naamini levo atapita kwakuwa ccm haitegemei kura kushinda.
 
Nani zaidi kwenye huu mchuano?
Tuna Massacre .....Hakuna anayetaka kujua nani aliyepewa Ubunge,udiwani na Tume ya CCM.

Kulikuwa hakuna uchaguzi bali ni MAIGIZO ya NECCM.

Barua kwa Ocampo - Juliani(Bahasha ya Ocampo).
 
Back
Top Bottom