Habarin wana JamiiForums,
Kwanza niweke wazi mm ndio nilikuwa wale waumini hatuamini km uchawi upo lakini now nimeamini. Pia niweke wazi familia yangu iko very structured, hata nikisema nichore family tree basi ni issue.
Ebu twende sasa kwenye mada. Baba yangu ana wake atatu wanaofahamika, mmoja alishafariki zamani sn hata mimi ckuwah kumuona na mdie aliemzalia mtoto wa kwanza, kaka yetu mkubwa. Mke wake wa pili ni mama yangu mimi ana watoto wanne; wawili wa kwanza ni wa kike. Hawa kila mtu na baba yake lakini sio baba yangu mimi, yaan apa namanisha tume-share mama ila wana baba zao ila wawili wa mwisho ndio sisi wa kiume, mimi na mdogo wangu ambaye baba yetu ndio main character hapo juu.
Sasa kimbembe kipo kwa huyo mke wa tatu ambae upo nae mpaka sasa kazaa watoto 6 wote wa kike huyu mama sijui kamfanya nn mzee maana mzee upo busy na io familia kuliko upande huu wetu mara ya kwanza niliona kam ni masihara haya mambo na mama alishanipiga marufuku kula kitu chochote nitachopewa na huyo mama maana anaweza hata kuniua na sababu kubwa ni kwamba yeye hana mtoto wa kiume.
Sasa maisha yamesonga nikawa nadhani labda mzee hajali hii familia sababu mama ana watoto ambao sio wa kwake lakini nikajaribu kuchunguza nikagundua mzee ana limbwata moja matata sana, yaani si la nchi hii.
Yaani unakuta huku kwetu kuna mtu ambae ni damu yake anaweza kuumwa na kuna hitaji sh laki 3 utasikia sina hela lakini huko kwake ukisikia mtu anaumwa utashangaa anaenda kutibiwa Ujeruman mara India tena kwa gharama zake sio msaada wala wadhamini.
Yaan karibu kila anachoambiwa na familia hii huku hasikilizi, yaani kila utachomwambia jibu ni rahisi: "Pesa hamna". Ukimwambia kuna biashara nataka nifanye, jibu ni rahii: "Pesa hamna". Kitu pekee anachoweza kutoa pesa ni chakula, maji na umeme kwishaaaa.
Sasa mtu unajiuliza huyu si binadamu siku akifumba macho itakuwaje kuna haja ya kuwa na miradi mikubwa ili tuwe na pesa zetu na sio kwamba hela hana, tatizo pesa zote anaweka kwa familia nyingine wanaishi kitajiri, wanaishi kifahari Sabasaba wanaingia mpaka na gari. Wanamilik miradi ming tu sitoitaja hapa kwa sababu za kimaadili. Mkewe licha ya kuwa hajasoma kampa na kazi ofisini kwake. Ngoja niishie hapo. Kifupi ni kwamba kule anafanya vurugu za pesa lakini familia ya huku inaishi kimaskini sana.
Sasa yote tisa miaka ya apo nyuma kidogo kuna siku nilimwambia mzee nataka nikapige
shopping ya nguo akaniambia hana pesa, sikujali maana hilo jibu nishalizoea. Sasa nikasikia mzee anaenda Norway kwenye biashara zake na matembezi humo humo ataenda na mkewe. Sikujali akiwa Norway alinichek kwa Whatsapp nimtumie namba ya kiuno na shati nikamtumia baadae aliporud Bongo akabipigia simu niende kwake kuna nguo kaniletea.
Nilipofika nikaenda mpaka chumbani kwake nikaonana naye tukaongea mawili matatu akaniambia begi la nguo lipo hapo sebuleni kachukue uondoke nalo. Sasa kipindi natoka ndiyo nakutana na huyo mke wake alikuwa kavaa kanga; alikuwa katoka kuoga sikujali mimi nikaelekea sebulen nikafungua begi nikachek pamba nikawa najipanga nilibebe nisepe nalo. He! ghafla nashangaa mzee na yule mkewe wanatoka chumbani wanakuja kwa kasi kama mshale. Niikashangaa wakaniambia chukua suruali moja na shati moja, zengine ziache hapo. Pia mchukulie mdogo wako suruali moja na shati moja.
Sasa nikagundua kuwa mzee alishavurugwa; yaani kipindi natoka pale chumbani yule maza aliwaka. Kingine cha ajabu, yule mama hana mtoto wa kiume. Hizi nguo za kiume za nini? Sasa kipindi nazuga zuga pale sebulen nikawa nasikia hizi tumpe fulani zile fulani na wote aliowataja apo nawajua ni kaka za huyo mama na wafanyakazi wake wa kiume hapo kwake.
Sasa baada ya kujiuliza maswali mengi yasiyo na majibu, kuna siku nikamuuliza dereva wa gari anaye-mdrive huyo mama. Vipi haya mambo mbona sielewi? Akaniambia mdogo wangu sikia nikwambie kitu, unafikir mm sijui kama baba yenu kawatelekeza? Najua sana tu sema nimekaa kimya. Akaniambia huyo mama ni mshirikina na mganga wake yupo Vingunguti, tena akamtaja na dada yake, wote wameolewa ila ndio michezo yao na ajabu ni kwamba kila Jumapili unawakuta church. Mzee wako kafungwa hajielewi.
Duh! Niliona maisha kama movie vile; nilitamani niwe kama
Mshana Jr. Nilitamani niwe mganga; nilitamani iniwe mlokole mwenye nguvu; nilitamani niwe hata shehe nikamnasue mzee huko aliponasa.
Naombeni ushauri nifanye nini maana nimefuatilia ni kweli anaenda kwa mganga. Hata pale ofisini kwake nilimweka chemba secretary anieleze ukweli akaniambia ni kweli huyu mmama ni mshirikina, kamfunga vilivyo baba yako.