Mwanaukweli
JF-Expert Member
- May 18, 2007
- 4,786
- 1,710
Ama kwa hakika kweli kufa ni kufaana kikabisa-kabisa
Yawaje haya yawasibu wajane ambao kilio chao ni kanisa lao?
Nilifikiri wajane ni wa kuwaangalia kwa jicho la huruma.,.
Kumbe huyu Baba Askofu kaona ni kivuno...
Wajamani Baba Askofu acha kushughulikia wajane.........
Kiama kimetufika na wanaumme tunateketea.......
Kiama cha wanaumme sasa harusi ya Baba Askofu..........
Kiama cha wanaumme chadhoofisha familia......
Kiama cha wanaumme chazalisha wajane........
Wajamani Baba Askofu acha kushughulikia wajane............
Waumme wanapotoweka si kilio tu huacha bali familia huyumba.......
Yule "bread winner" akiwa kapuni mjane humlazimu kurithi mikoba yake.....
Lishe, pango, matibabu, karo na usafiri ni baadhi ya kero zake.....
Sasa kero za mjane Baba Askofu kwake ni kitoweo.........
Wajamani Baba Askofu acha kushughulikia wajane.............
Pesa za wafadhili za kuhudumia wajane sasa hutolewa kwa masharti.....
Masharti ya Baba Askofu ni moto na mchezo hataki............
Bila ya wajane kumtuliza kiu yake, patupu huambulia mgao wao.......
Kwa kubanwa kila upande wajane waona bora wamtumikie kafiri wapate mradi wao.....
Wajamani Baba Askofu acha kuwashughulikia wajane.........
Ruta umetumia lugha ya ushairi ambayo ujumbe wake unahitaji tafakari.
Baadhi ya wachangiaji hapa hawakukupata vizuri. Hasa maana ya Baba Askofu uliyotumia hapa.