Baadhi ya Vyuo Vikuu vinazalisha Wasomi bomu

BOB LUSE

JF-Expert Member
Jan 25, 2014
3,646
3,041
Nafuatilia mijadala na maoni ya wahitimu wa vyuo vikuu hapa nchini baadhi yao ni sheedah! wanadhalilisha vyeti vya degree! hata humu jf unakuta mtu anajinasibu anasoma/amemaliza.degree lakini anaomba ushauri wa jambo analopaswa kulipatia ufumbuzi bila kuomba ushauri.

Nailewa takwimu zinathibitisha kuwa asilimia 60 ya wenye degree hawaajiriki/not competent for jobs.pia nawaelewa wale vijana wa chuo kikuu kilichofunga compus ya Songea na Arusha.Wakaomba na Dar compus pia ifungwe ili wahamie vyuo vikuu ambavyo angalau taaluma yake inasifa na vigezo.

Naona wanasiasa wame focus sana huko shule za msingi na shule upili wamesahau advanced na university product zao.wamejikita kwenye quantity kuliko quality.ukiuliza jibu jepesi wanafunzi wakimaliza vyuo wafikirie kujiajiri! kisa kuna katopic ka entrepreneur kapo kwenye hiyo programme.kwanini huko kujiajiri kusifanyike kwa vitendo japo miezi sita/mwaka ndio degree zitolewe kwa atakayefuzu.

wenye masikio wasikie baadhi ya wenye degree hazina msaada kwao.
 
Asilimia kubwa ya vyuo hapa Tz wanazalisha vilaza, utaona tu watu walivyo bize kuajiriwa! Ukimwambia fanya mpango tumia elimu yako kujiajiri atasema hana mtaji, ukimuuliza endapo utapewa mtaji utajiajiri?? NDIO. Unataka ujiajiri kufanya shughuli gani?? HAJUI.
 
Tatizo wenye akili nyingi walishakatwa majina yao tangu o-level wakachaguliwa vilaza.

Mhhh!! wamekatwa na nani tena huko o level? na necta? hapana kwa kweli! mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Nakubaliana na mtoa mada ya kuwa elimu yetu inahitaji mabadiliko ya kwenda na wakati na pia maendeleo ya sayansi na teknolojia.
 
Ukilaza ni shida ya mwanafunzi, ingawa mazingira ya chuo yanachangia sana! Ila kuna wanafunzi wako vzr sana hata kwenye hivyo vyuo vya kata!

Wanafunzi wanajisahau sana, wanajua kufaulu mtihan pekee kutawatoa mtaani, hata ukasome Harvard kama concept yako ya shule n kufaulu mtihan tu, utakuwa wa kawaida na utarudi ajiriwa wakati dropout wanaanzisha makampuni makubwa makubwa
 
Ruco ihusike walio somea iringa wanajua ha ha ha cut off points ingawa sio kigezo sana ingawa bongo tunapima cognition.
 
Hawa jamaa wengi wanabebwa na status, ila hawajiamini kabisa! Ukimbana umweke kwenue kona atakwambia mie UDSM bhana.

fikiri kabla kuposti na kushabikia ujinga ukiambiwa leta ushahidi unaanza kuropoka!! chunga sana upumbavu wako unakupeleka kusiko!!
Huyo jamaa ndio aliyepata EEE A level akaenda s.t kunani chuo. Muonee huruma tu usimchambe
 
Back
Top Bottom